Your Majesty
JF-Expert Member
- Aug 29, 2018
- 3,242
- 5,345
Ahsante mkuu kwa kuwakumbusha wadau....Mnyama anaingia mawindoni tena kwa mtego mkali.Mabingwa wa nchi ya Tanzania Simba Sports Club inatarajia kukwaruzana na Klabu ya Nyasa Big Bullets FC ambao ni vinara wa ligi kuu nchini Malawi Ijumaa ya Novemba 16, 2018 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Simba SC katika mchezo huo wa kirafiki na Nyasa Big Bullets FC, ni katika kuendelea kuwa sawa kwenye kikosi hicho, pia ni maandalizi ya kujiandaa katika michuano ya kimataifa kwa mchezo wa Novemba 27/28 dhidi Mbabane Swallows kutoka Swaziland, katika michuano ya klabu Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.View attachment 931240
Bwana Aussems alipendekeza timu ya nje moja na ya ndani moja.Sijajua ya ndani itakuwa ni ipi.Kama MBUTEMBUTE FC wangekubali, tungewanyoosha uzuuuri kabisa.Hizi sasa sifa jamanini..Yaani hata mechi ya kirafiki lazima timu itoke nje ya nchi [emoji3][emoji3][emoji3]
Chama kubwa...kikosi kipana.Yes..Mubashara kupitia Azam Sports 2..SimbaNguvuMoja
Leo linapigwa show la kibabe.Chama kubwa...kikosi kipana.
Watatoka nduki haoooo.Hali ni mbaya huko kwa jirani zetu.hivi mechi ya ndani si tuombe tucheze na Yanga jamani
Updates mwanangu15' mchezo wa kirafiki uwanja wa Taifa
Simba SC 0-0 Nyasa Big Bullets FC