'Friends of Raila'...(F.O.R.A.) watangaza kuwa bosi wao ameshinda kura za jumla nchi nzima

'Friends of Raila'...(F.O.R.A.) watangaza kuwa bosi wao ameshinda kura za jumla nchi nzima

Hapa ni lazima kuna tatizo tena kubwa, haiwezekana matokeo ya saa moja asubuhi yenye 30% ya kura yaendelee kuwepo hadi sasa saa nane.
Mkuu sasa hivi ni saa nane na dakika kumi uhuru 54. 06% na odinga 41.44%

Source citizen tv.

Ulipata wapi matokeo hayo?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kama wakikuyu walishinda uchaguzi wa 2007 na walikuwa kabila moja tu je sasa hvi wameungana na watu wa meru , bukusu , nusu ya watu wa kisii, nusu ya watu wa pwani pamoja na wamasai ndo wataacha kushinda. RAIS LAZIMA NI KENYATA PENDA MSIPENDE.
 
Friends of Raila Odinga wamesema kwamba matangazo yaliyoko citizen tv ni sahihi ila kwa bahati mbaya yameinvolve strong hold za Kenyatta kuliko Raila. That is the current news my friends ndo maana hata mods hawatoi hii thread yangu.

...Ebu angalia hizi Country, angalia matokeo ya hizo Country, angalia ngome za Uhuru, angalia Registered Votes, angalia kura zilizojumlishwa mpaka sasa, linganisha na ngome za Raila, alafu pata jibu....

...Nikupe mifano michachae...

1. Baringo: Uhuru ana 88%
Odinga ana 10%
Kura zilizojumlishwa mpaka sasa ni kama 75,000; Jumla ya Wapiga kura hapo ni 548,000

2. Bomet: Uhuru 93%
Odinga 4%
Kura zilizojumlishwa mpaka sasa ni kama 105,000; Jumla ya Wapiga kura hapo ni 730,000

3.Marakwet: Uhuru 92%
Odinga 5%
Kura zilizojumlishwa mpaka sasa ni kama 16,000; Jumla ya Wapiga kura hapo ni 346,000

4.Laikipia: Uhuru 87%
Odinga 11%
Kura zilizojumlishwa mpaka sasa ni kama 72,000; Jumla ya Wapiga kura hapo ni 621,000

5.Nandi Uhuru 85%
Odinga 6%
Kura zilizojumlishwa mpaka sasa ni kama 80,000; Jumla ya Wapiga kura hapo ni 417,000

SOURCE: Website ya Tume ya Uchaguzi: http://elections2013.nationmedia.com/president.html
 
Kwenye facebook na Radio za kenya friends of Raila Odinga wametangaza wazi kwamba bosi wao ameshinda nafasi ya Urais baada ya wao kujumlisha kura za nchi nzima za vituo vyote. Hii ndo habari mpya ya mchana huu. Hongera kwa Chadema waliomsapoti Odinga.

Source.
 
[]Ameshinda kwa mujibu gani sasa?, yale matokeo ya asubuhi ambayo ni asilimia 30 tu ya kura zilizohesabiwa?[waache waweseke...mimi ninachoona hapo ni kwamba, kura nyingi hazijahesabiwa, na niweze tu ku-declare interest, nam-support Raila Odinga kwa faida ya Wakenya...he is someone who is for the country and not personal gains]
 
sasa kama ni ukabila wakikuyu ni wengi kuliko makabila yaliyobakia? Na kama ni nusu ya vituo vimewasilisha matokeo, uwezekano wa kufungana kati ya Odinga na Uhuru ni mkubwa
 
usiwadharau, wanaweza kuwa na hoja. Hebu angalia hapa alafu kama ni hivi ina maana nusu ya vituo vya kupiga kura havijawakilisha matokeo;
13:19 IEBC provisional results: Mr Kenyatta 2,495,800, Mr Odinga 1,896,174. 12,254 of 31,981 polling stations have reported.
Eeeh, hapo kwenye blue, kumbe bado parefu. Mimi nilifikiri ndiyo wanakaribia mwisho kumbe hata katikati hawajafika? Basi ni mapema sana kusema lolote.
 
Tiba,
Umetujuza kuwa uko Kenya kama observer halafu unakuja na conclusion ya jumlajumla kiasi hiki!play your party.Leta hapa analysis zako za uchaguzi huu unaoendelea.Usiwawadhihaki Wakenya sio wote waliompigia Odinga ni wajaluo na wala sio wote waliompigia Kenyatta si Wajaluo.

Mkuu hayo ni mawazo yangu binafsi wala hayawakilishi mawazo ya aliyenituma hapa. Naomba Nieleweke hivyo!!! Frankly speaking kura bado zinahesabiwa halafu watu wanakuja na vitisho vya kusema wao wana tallying centre yao inayoonyesha kwamba mtu wao anafanya vizuri. Huu ni upuuzi na kutafuta kuja kuleta machafuko endapo at the end of the day Raila hatatangazwa mshindi!!!

Tiba
 
Hapo ni presha tu kwa wapiga kura la msingi tufanye subira matokeo ya mwisho ndio yataueleza uma nani mshindi na nadhani hakuna uchakachuaji hapa, wanaJF tupunguze munkhari mambo ndio yanaendelea kunoga hayo
 
Majumuisho kutoka Bomas of Kenya kufikia saa 7:30 mchana huu:
Uhuru kenyatta kura 2,521,601
Raila Odinga kura 1,926,588

Wahabarishe the so called friends of Raila.
 
Kwenye hii Thread kuhusiana na huu uchaguzi wa jirani zetu kuna watu humu ndani ni wabishi kama kina Lukuvi!
 
Iwapo Raila atatangazwa mshindi basi tume ya uchaguzi inatakiwa ijifunze jinsi ya kuwa inatoa matokeo. Haiwezekani mgombea mmoja yuko mbele kwa masaa zaidi ya 18 na gap imekuwa inaongezeka tu, halafu ghafla mambo yabadilike. Hapo itakuwa inamaanisha kuwa matokeo hayajatolewa randomly, sasa tume wataulizwa kwanini matokeo hayajatoloewa randomly???
 
Mkuu sasa hivi ni saa nane na dakika kumi uhuru 54. 06% na odinga 41.44%

Source citizen tv.

Ulipata wapi matokeo hayo?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Citizen Television ya Kenya! Unaswali lingine unataka kuuliza nikujibu faster?
 
Iwapo Raila atatangazwa mshindi basi tume ya uchaguzi inatakiwa ijifunze jinsi ya kuwa inatoa matokeo. Haiwezekani mgombea mmoja yuko mbele kwa masaa zaidi ya 18 na gap imekuwa inaongezeka tu, halafu ghafla mambo yabadilike. Hapo itakuwa inamaanisha kuwa matokeo hayajatolewa randomly, sasa tume wataulizwa kwanini matokeo hayajatoloewa randomly???
Kamanda usiwe nahofu! waliojiandikisha na kupiga kura ni Million 14, na mpaka sasa ni kura si zaidi ya Million 4 ndizo zilizohesabiwa! Tusubiri
 
Back
Top Bottom