From Karimjee Hall: Public Hearing ya Kamati ya Bunge toka kwa wadau wa Dar es Salaam


Nakubaliana kuwa mamlaka juu ya katiba mpya yawe kwa wananchi lakini siafiki kuwa kazi hiyo wananchi wakasimu kwa bunge hili ambalo wabunge wake wengi wanatoka chama cha mafisadi; kufanya hivyo ni sawa na kumuachia nyani akulindie shamba lako la mahindi!! The best way forward is to have a constituent assembly representing different stakeholders in our country ndio wafanye hiyo kazi kwa niaba ya wananchi.
 
kwa upande wangu nimesikitishwa sana na vyombo vya habari hapa Tz,jambo muhimu kama hili wanashindwa kuliweka live,ila watu wakifumaniana ktk ndoa Tv zetu ndizo za kwanza kuweka habari za kipuuzi
kwani huu mchakato wa katiba hautowagusa wamiliki wa vyombo vya habari?
kwani TBC ni chombo cha umma lakini kinafanya kazi kwa malengo ya watu wachache,na ndio maana walimtoa Tido mhando mzee wa uwazi na ukweli lengo ni kuendelea kuturudisha nyuma ktk zama zileeee

Hongereni wapigani wa Jf,
PAMOJA TUTAFIKA,TUSIPOFANYA SISI NANI ATATUFANYIA?
 
Pasco,
Ni masikitiko kuwa siku ya mapumziko inakubidi uingie mzigoni, hata hivyo tunashukuru kwa mchango wako kutuhabarisha sisi ambao hata FM ni baba mkwe huku village ya kijijini.
 
wakuu, ni kweli tulikuwepo ndani ya karimjee, vurugu zimetokea, kamati imeshindwa kumudu majukumu yake, public haikuwa tayari kuendelea kumsikiliza propagandist wa ccm (tambwe hiza) alipokuwa akimwaga pro. kamati ingeweza kuchukua written opinion ya tambwe aliyekuwa akiusifia saaana muswada, ikaonekana ilitaka aendelee kumwaga porojo, raia wakamnyima masikio kwa makofi mfululizo, mayowe, miluzi, almanusura ukumbi uwe uwanja waminyukano. kikao kikaahirishwa kutoka kama saa sita na........ hadi saa nane ambapo tuliambiwa kikao kimeahirishwa hadi kesho asubuhi.
 

Kwahiyo walifukuza umati wa watu wakabaki hawa wachache? Mmh hii kali ya mwa!
 
nimeangalia jicho la habari star tV leo asubuhi,nimesikitishwa na mwanaJF mmoja anaitwa Kigwangala(mbunge wa nzega) kuupotosha uma kwa makusudi kabisa. anaseme CHADEMA walisema wangeandika katiba mpya ndani ya siku 100.....na mbunge wa viti maalumu anaitwa BULAYA nae anaunga mkono kuwa ndivyo CDM walivyoahidi....waliahidiwa wapi hawa wenzetu????mbona uongozi wa CDM ulifafanua wakati wa kampeni kuwa wangeanzisha mchakato ndani ya siku 100 na siyo kumaliza kila kitu ndani ya siku hizo.....

nimekuwa nasoma mabandiko ya mheshimiwa huyu kwa umakini hapa jamvini nikiamini ni mtu makini sana kumbe ni another Tambo Hizi of its kind. kwa nini utumie muda mwingi kupotosha jamii ya watz wanaomuamini kiasi hicho??????
amenikera kwa kuwa anatumia propaganda hizo kujustify uharaka walionao CCM kuburuza wananchi kuhusu mchakato huu wa katiba kwa kulinganisha kuwa mtapata katiba nzuri kwa kuwa ccm itaandika kwa miaka minne mizima sio kama CDM waliosema siku 100!!!!

why?why? whyyyyyyyyyyyyyyyyy?
napata wasiwasi mtu akiwa ccm anazuiwa kufikiri kwa kina ila anaandaliwa cha kusema na akina Tambo Hizi.

......
 

Nadhani wanahabari wengi wanatokana na magazeti ya udaku ambayo huwajenga hivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…