FT: Agosto 1-3 Simba | CAF Champions League | Estádio 11 de Novembro | 9-10-22

FT: Agosto 1-3 Simba | CAF Champions League | Estádio 11 de Novembro | 9-10-22

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
FULL TIME
90' Zinaongezwa dakika 3 za nyongeza
78' Agosto wanapata goli la kwanza
GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
76' Agosto wanapata penati baada ya beki wa Simba kuushika mpira
Phiri anafunga goli zuri akimalizia pasi ya Chama
75' GOOOOOOOOOOOOOOOO
72' Agosto wanaweka mpira wavuni, lakini mwamuzi anasema ni offside
70' Simba wanamtoa Kibu Denis anaingia Bocco
65' Simba wanaongoza kwa magoli 2-0
Israel Patrick anaipatia Simba goli la pili kwa shuti kali akimalizia pasi nzuri ya Kanoute
62' GOOOOOOOOOOOOOOOO
56' Phiri anapata nafasi, shuti lake linatoka nje la lango
50' Agosto wanalazimisha mashambulizi lakini walinzi wa Simba wapo imara
47' Mchezo umeanza kwa kasi ya wastani

Kipindi cha pili kimeanza

MAPUMZIKO

45' Shambulizi langoni mwa Simba, lakini mpira unatoka nje
40' Israel anacheza faulo dhidi ya mshambuliaji aliyekuwa anaelekea langoni mwa Simba
31' Agosto wanapata nafasi ya wazi lakini shuti linadakwa na Manula
25' Agosto wanaendeleza kasi ya kushambulia
18' Agosto wanapata kona
17' Simba wanaanzisha mipango kutokea kwa safu yao ya ulinzi
15' Timu zote zinashambuliana, Agosto wamefanya shambulizi kali Manula akaokoa hatari
10' Kasi ya mchezo imeongezeka, wenyeji wanapambana kutafuta bao
Chama anaipatia Simba goli la kwanza
7' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

5' Timu zinapokezana kumiliki mpira, Simba wamepata kona moja na wamefanya shambulizi moja kali
Mchezo umeanza
Timu zimeshaingia uwanjani, Simba wamevaa jezi nyeupe

FeofxPfXkAIXDBw.jpg
Kikosi cha Simba kitakachoanza kimewekwa hadharani, ni hiki hapa...

Kikosi cha Simba kimeshawasili uwanjani
Feoc5bLXoAk3FcK.jpg
============

Wana bodi...

Simba a.k.a Mnyama a.k.a Lunyasi wawakilishi pekee wenye uzoefu katika michuano ya kimatifa toka Tanzania leo wanashuka dimbani huko Estadio General Franca Ndalu, jijini Luanda nchini Angola.

Ni Primeiro de Agosto Vs Simba Sc katika mchezo wa kufuzu makundi ya Klabu Bingwa Afrika mchezo wa kwanza. Simba itashuka dimbani ikijaribu kulinda heshima ya nchi, ambapo watakuwa ugenini kujaribu kusaka ushindi au droo kabla ya kurudiana jijini Dar Es Salaam wiki moja baadae. Kikosi cha Simba kipo tayari kupambana kwani wachezaji karibia wote wako fit kwa ajili ya mchezo wa leo.

Primeiro Agosto ni timu inayomilikuwa na Jeshi la Angola imefuzu hatua hii baada ya kuwatoa Red Arrows ya Zambia huku Simba ikiwa imeitoa Nyasa Big Bullets.

Mchezo utapigwa saa 12:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki na utakuwa mubashara kupitia Azam Sports HD1.

Tukutane hapa...mje twisheni muone jinsi mechi za Kimataifa zinavyochezwa!!
 
Hz timu za jeshi Mara nyingi hazina maajabu Simba atajipigia boya wake pale pale nyumbani

Hyo premiro Ni Kama ruvu shooting na jkt Tanzania sas hawa wanna jipya ganj katk Soko la nnchi hi hvyo simba imalabue vzr San hcho kitimu Cha kijeshi na kikija hapa mjin dsm bas wapewe kipigo kizito

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Mpira ni uwekezaji, Leo tutashuhudia uwekezaji wa Simba, Nawaombea wapate kile wanacho stahili, wasizidishiwe Wala wasipunguziwe.
Hii game ya leo ni ngumu na Simba SC tunamuheshimu mpinzani kwa kuchukua tahadhari zote.

Hivyo tutapambana kutafuta sare au ushindi ili kutengeneza mazingira ya kuifanya game ya marudio iwe nyepesi.

Yale mambo ya Ali Kamwe ya kusema kwamba Yanga ina Quality na Uwekezaji na fedha kuliko Al Hilal, tuawaachia wao Gongowazi.
 
Wadau wanasema Dauda ameshawauza Simba kule angola
 
Tusiwazalau Agosto muhimu kuomba Dua tushinde au iwe sare.

Tukitoka Agosto 1-0 sio mbaya
Agosto 2-1 sio mbaya
Maana kazi tutamalizia Taifa
 
Back
Top Bottom