FT: Al-Hilal 1-0 Yanga (Agg 2-1), Yanga yaondolewa Ligi ya Mabingwa Afrika

FT: Al-Hilal 1-0 Yanga (Agg 2-1), Yanga yaondolewa Ligi ya Mabingwa Afrika

Execute

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
3,000
Reaction score
7,336
FULL TIME
90+1' Zinaongezwa dakika 4 za nyongeza
90' Wenyeji wanaweka mpira wavuni lakini mwamuzi anasema mfungaji aliotea
81' Farid Mussa anaingia, anatoka Fei Toto kwa Yanga
76' Yanga wanamtoa Morrison anaingia Makambo
70' Mchezo umesimama kwa muda, mchezaji wa Al Hilal ameumia
60' Fei Toto anapiga shuti linatoka na kuwa kona
53' Yanga wanamiliki mpira muda mwingi
50' Al-Hilal wanafanya shambulizi kali langoni mwa Yanga
Kipindi cha pili kimeanza

MAPUMZIKO
45' Mwamuzi anamaliza kipindi cha kwanza
40' Timu zote zimefanya mashambulizi makali kwa kupokezana
37' Mwamnyeto anacheza faulo, inapigwa kuelekea kwa Yanga
36' Yanga wanaendelea kuweka presha langoni mwa wenyeji wao
30' Kasi inaongezeka na Yanga wanaonekana kujiamini
20' Yanga wanafanya shambulizi lakini mpira unatoka nje
15' Kocha wa Al-Hilal, Ibenge anasimama kutoa maelekezo
10' Yanga wanaonesha utulivu na kujipanga
Mohamed Abdelrahman anaipatia Al-Hilal bao la kuongoza
3' GOOOOO!
2' Wenyeji wanafika langoni mwa Yanga
Mchezo unaanza
Timu zinaingia uwanjani

Yanga kikosi.jpg

Kikosi cha Yanga dhidi ya Al-Hilal katika mchezo wa marudio.
========

Ni siku iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu sana na mashabiki hapa Tanzania na kule Sudan.

Yanga inashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu ya sare ya 1-1 aliyoipata nyumbani pale uwanja wa Mkapa wiki iliyopita.

Je, hii itakuwa mechi ya mwisho kwa Yanga msimu huu kwenye Klabu Bingwa Afrika au anaenda kuvunja rekodi yake kwa kufuzu makundi tangu 1998?

Tutakuwa hapa tukipeana taarifa mubashara. Mechi inaanza saa tatu kamili usiku.
 
KAPINDUA MEZAA MWANAUME LEOO
KALA 3-1 UGENINI..HME KAKOMAA
 

Attachments

  • Screenshot_20221016-002452.png
    Screenshot_20221016-002452.png
    238.1 KB · Views: 9
Huu uzi hauna hadhi ya kuwa uzi rasmi wa mechi ..
 
CAF na Karia wana hujuma na Yanga,kwanini mechi ya kwanza wameweka ya Simba saa kumi jioni alafu Yanga yetu saa tatu usiku?

Huku ni kupanga matokeo.Yanga tukifungwa na Al hilal Simba nao wakishinda tunaenda kumuona Rais,Yanga tunaonewa na kunyanyaswa sana.

Mungu mbariki mzee Mpili na Mandonga[emoji120]
 
Uto mtaukimbia huu uzi kabla ya saa 3:15 usiku
 
Back
Top Bottom