FT: Ligi Kuu Bara: Kagera Sugar 1 -1 Simba SC | Kaitaba Stadium 21/12/2022

FT: Ligi Kuu Bara: Kagera Sugar 1 -1 Simba SC | Kaitaba Stadium 21/12/2022

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Mwendelezo wa Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Bara[emoji1241] kuendelea kupigwa leo Disemba 21, 2022 ambapo wenyeji Wanankurukumbi Kagera Sugar wanawakabili Wekundu wa Msimbazi Mnyama Mkali Mwituni Simba SC[emoji881] kwenye Uwanja wa Kaitaba[emoji2522] mkoani Kagera.🟢

Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1:00 Usiku. Usikose Yatakayojiri.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana

C262E929-7B4F-4324-81BC-B67DA4966383.jpeg

Kikosi cha Simba

44BF3B15-7432-4978-BBD1-B7C2EBF935A2.jpeg

Kikosi cha Kagera Sugar
Mchezo umeanza kwenye Uwanja wa Kaitaba

5' Simba wanafika langoni mwa Kagera lakini wanakosa umakini
10' Kagera nao wanajipanga taratibu
11' Shuti kali langoni kwa Simba, linaokolewa na Inonga
14’ Kagera wanapata kona mbili mfululizo
15’ Deus Bukenya anaipatia Kagera goli kutokana na mpira wa kona
20’ Kagera wanaonekana kujiamini zaidi na kumipiki mpira
23’ Kagera wameshapata kadi mbili za njano
30’ Simba wanamiliki mpira muda mwingi lakini Kagera wanakuwa makini kuzuia
32’ Shuti la Phiri linatoka nje ya lango
37’ Presha inaongezeka kwa Simba wakitafuta goli
38' Inonga anasawazisha goli kwa upande wa Simba, akimalizia mpira wa Zimbwe Jr
44' Kagera wanafanya shambulizi kali, almanusura wapate goli
45' Zinaongezwa dakika 2 za nyongeza

MAPUMZIKO

Kipindi cha pili kimeanza
48’ Phiri anachezewa faulo ndani ya boksi, mwamuzi anapeta
55' Timu zinapeana zamu kumiliki mpira na kushambuliana kwa zamu
60' Faulo karibu na lango la Kagera baada ya Phiri kuchezewa faulo
63' Mzamiru anacheza vizuri, anapiga shuti linatoka nje
70' Sakho anatoka anaingia Okrah, mabadiliko kwa Simba
75’ Chama anachezewa faulo
76’ Shuti la nje ya 18 la Kanoute linadakwa na kipa wa Kagera
78’ Mambo ni magumu kwa timu zote
79' Moses Phiri anatoka akiwa anachechemea, anaingia Kibu Denis
90' Mambo ni magumu kwa timu zote, zinaongezwa dakika 5

Full Time: Ngoma ni 1-1
 
Katika mchezo 11 waliyokutana Kati ya Simba SC na Kagera Sugar hakuna sare..!

Simba SC ameshinda 7 huku Kagera akishinda 4..Leo dakika 90 za Jasho na Damu Kuamua.
20221221_174949.jpg
 
Yaani leo hii ligi ya bongo mechi za mkoani baadhi zinapigwa hadi usiku..Ligi imepiga step..lakini bado nguvu kubwa inabidi itumike..kama mechi ya Kagera na Azam niliona kama bado uwanja una gizagiza.

Waweke taa nzuri.
 
Mwendelezo wa Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Bara[emoji1241] kuendelea kupigwa leo Disemba 21, 2022 ambapo wenyeji Wanankurukumbi Kagera Sugar wanawakabili Wekundu wa Msimbazi Mnyama Mkali Mwituni Simba SC[emoji881] kwenye Uwanja wa Kaitaba[emoji2522] mkoani Kagera.🟢

Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1:00[emoji354]Usiku. Usikose Yatakayojiri.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
Mikia buana,saizi wanapumulia machine na timu lao la kuunga unga
 
Yaani leo hii ligi ya bongo mechi za mkoani baadhi zinapigwa hadi usiku..Ligi imepiga step..lakini bado nguvu kubwa inabidi itumike..kama mechi ya Kagera na Azam niliona kama bado uwanja una gizagiza.

Waweke taa nzuri.
Ule ni uwanja wa Namungo,taa zinazingua muonekano unakuwa mbaya
 
Kauli ya Kocha wa Simba SC kuelekea mchezo dhidi ya Kagera Sugar.
Screenshot_20221221-174601~2.jpg
 
Back
Top Bottom