FT: Simba 2 Geita Gold 1 NBC Premier League

FT: Simba 2 Geita Gold 1 NBC Premier League

Mnazi wa makolo Leo ,mbebwa live bila chenga , ww msimu huu utapata presha wallah hahahaha maana c kwa unazi huu
Ni makosa ya kibinadamu yanaweza kumkuta mtu yeyote tumsamehe refa
 
Ukiupenda mpira kabla ya timu zetu, utakubali leo tumebebwa.

Anyway kapombe amekuwa mchezaji wa kawaida, Gadiel Michael sijui kwa nini kakaa humo hadi tamati.
Tunaongea na wanaojua mpira kama wewe Mkuu. Kitendo alichofanya Kapombe ni uhuni na kwa kocha aliye serious anapaswa ampumzishe kabisa. Beki unaguswa mgongoni unaruka kama umechomwa kisu?
 
Naona una halalisha mbeleko yako dhidi ya namungo kwa kutumia faulo ili ionekane halali

Mbona hata mazingira ya goli la leo unaweza uka apply sheria hiyo hiyo kwa kusema mchezaji aliyeanguka kabla ya goli kuingia alifanyiwa faulo na ika-make sense tu?
Hajaguswa hata kwa uzi wa nguo au hata upepo. Utasemaje ni faulo.?

Mwenye replay jama aiweke humu.
 
Ni makosa ya kibinadamu yanaweza kumkuta mtu yeyote tumsamehe refa
Mbona upande wa pili husemi kua ni makosa ya kibinadam , ulisema ni mbeleko na Leo ni mbeleko live bila chenga , huyu refa na yy lazima apewe adhabu c kwa ujinga huu wanaofanya uwanjani
 
Sielewi kwa vipi hawa makocha wote watatu wanashindwa kujua kama Kapombe na Boko sio First 11 tena. Israh Mwenda ndio habari ya mjini now.
Huwezi kuchezesha first eleven kila mechi
Leo wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza wamepumzishwa kwa ajili ya mechi mbili zijazo muhimu sana
 
Hii ni aibu kwa soka letu. Kwa issue ya yanga na Namungo unaweza singiziaa kua Feisal alichezewa faulo na ukaning'inia hapo. Hii ya kapombe watu wataning'inia wapi?

Mpira wa tz ni aibu sana. Aibu kubwa sana.
Matukio yote mawili hayana tofauti.
 
Ni kwamba Geita Gold wamefunga, goli likakataliwa

Ilikua hivi, mchezaji wa Geita aliyefunga alikua nyuma ya Kapombe, Kapombe aliruka akaukosa mpira, ikabidi ajiangushe, Refa akatafsri amesukumwa ilihali hakusukumwa alijirusha tu mwenyewe na ubwege wake

Na mfungaji wala hakutumia nguvu kuruka, yaani ni aibu kukataa lile goli, ila ndio hivo tena!!!
Urefa unasomwa. Hiyo ni tafsiri yako. Refa alikua eneo la tukio na alitafsiri alivyoona.
 
Ni makosa ya kibinadamu yanaweza kumkuta mtu yeyote tumsamehe refa
Namungo na Yanga ilichezeshwa na Robot? Wenye akili tulisema marefa wa Tanzania hata wasipohongwa ni wabovu kwa asili, lakini kila ikitokea upande wa pili mnakimbilia hongo.
 
Bora point 3 zimepatikana.
Ndio cha muhimu haya mambo ya refa sijui hivi mara vile ni ukuda unaotufanya tutoke nje ya misingi ya utanzania kuwa wote sisi hapa ni ndugu kwa hiyo matokeo uwanjani yasitutie kwenye reli
 
Back
Top Bottom