FT: Uganda 0-1 Tanzania: Kufuzu Afcon 2023 group E

FT: Uganda 0-1 Tanzania: Kufuzu Afcon 2023 group E

Mimi mwenyewe kwakweli, niko mbalimbali na taifa stars, kuna ile timu ya serengeti boys ilifanyaga vizuri sana wakati fulani wakaenda sijui mashindano gani huko, wangekiendeleza kile kikosi kama taifa stars nadhani tungefika fika mbali kidogo
Kabisa sema kila kitu Tz ni siasa na upigaji.
Tungeanza tafuta vipaji, watoto toka shule za msingi. Tukawasomesha huku wako kwenye shule maalumu ya michezo.
Angalau tungepata kikosi, miaka ya baadaye tukajivunia nasisi, ila hivi huwa hatufiki mbali.
 
Kabisa sema kila kitu Tz ni siasa na upigaji.
Tungeanza tafuta vipaji, watoto toka shule za msingi. Tukawasomesha huku wako kwenye shule maalumu ya michezo.
Angalau tungepata kikosi, miaka ya baadaye tukajivunia nasisi, ila hivi huwa hatufiki mbali.
Unasema kweli academy sio kwamba hazipo huko Mwanza kwa mfano zipo academy Ila ni za watu binafsi wakishawakuza watoto wanawauza kwenye virabu au clubs, Ila Serikali haina hio taratibu, kuna mama nilimfuatilia yeye anafanya hio issue alikua anahojiwa anasema kinachokwamisha ni gharama za uendeshaji wazazi hawawezi kumudu gharama maana gharama ni kubwa sio NDOGO
 
Unasema kweli academy sio kwamba hazipo huko Mwanza kwa mfano zipo academy Ila ni za watu binafsi wakishawakuza watoto wanawauza kwenye virabu au clubs, Ila Serikali haina hio taratibu, kuna mama nilimfuatilia yeye anafanya hio issue alikua anahojiwa anasema kinachokwamisha ni gharama za uendeshaji wazazi hawawezi kumudu gharama maana gharama ni kubwa sio NDOGO
Yes zipo nyingi naona ni watu binafsi kweli. Sasa jukumu hili lingebebwa pia na wizara ya michezo.
Wangetengeneza Academy, mbili kubwa.
Sisi hatuna hata cha kujivunia, ikija michezo...

Tukija riadha huko, hivi tunashindwa kuwatrain jamii ya Kimasai na wanaotokea Singida. Maana wana urefu na wepesi. Kinachotakiwa mazoezi kwa sana na ari ya kushinda.
 
Tukija riadha huko, hivi tunashindwa kuwatrain jamii ya Kimasai na wanaotokea Singida. Maana wana urefu na wepesi. Kinachotakiwa mazoezi kwa sana na ari ya kushinda.
Hapa kwenye riadha chama Cha riadha Tanzania focus yao ni kwa watu wa kasikazini hususani Arusha huko ndio sana sana, mfano mzuri Felix Simbu na wengineo, Ila mikoa mingine hawajafocus chochote Sana sana mara labda marathon za ndani na East Africa labda
Yes zipo nyingi naona ni watu binafsi kweli. Sasa jukumu hili lingebebwa pia na wizara ya michezo.
Wangetengeneza Academy, mbili kubwa.
Sisi hatuna hata cha kujivunia, ikija michezo...
Kuhusu hili linahitaji Waziri mwenye malengo ya muda mrefu Ila wengi huja na malengo ya mda mfupi kwa hio hawaliangalii hilo nilipoona wanajenga ile JK nini sijui kule Gymkhana nikajua wamelenga hayo masuala kumbe wamelenga watoto wa upanga waende kucheza tennis na basketball na cricket kwa mbali hawakufocus masuala ya academy, pia Nchengwera kabla hajaondolewa alikua na mkakati wa kujenga sports arena kule Kawe na akasema inaanza kujengwa mwezi March na itachukua miezi 8 kukamilika sijajua km itajengwa kweli au ndio eeh hivyo, kwa hio kila Waziri ana malengo yake Ila sio ya miaka 20/50 kuendelea ni miaka 5/10 mbele basi
 
Maajabu wanaweza kuja tugonga lupaso

Karibuni tena katika mechi kubwa ya kimataifa baina ya miamba wa soka hapa Afrika ya Mashariki, Uganda dhidi ya Tanzania katika kutafuta nafasi ya kufuzu Afcon 2023.

Mechi hii itapigwa kuanzia mida ya saa 11 jioni katika dimba la Suez Canal Jijini Ismailia na itarushwa na Azam sports kupitia chanel ya ZBC2

Kuwa nami paka mwisho...

=============

Mpira Umeisha: Tanzania yashinda kwa goli 1-0 dhidi ya Uganda, mfungaji wa goli hilo ni Simon Msuva

Tanzania inaongoza kwa goli 1 , goli limefungwa na Simon Msuva katika dakika ya 68
go
 
Back
Top Bottom