Championship
JF-Expert Member
- Aug 7, 2019
- 5,500
- 10,616
Timu zote zimeshaingia uwanjani.
Mchezo umeanza
01' Yanga wanamiliki mpira wakipiga pasi kadhaa.
11' Kibu Denis anaachia mkwaju na kuishia kwenye nyevu za pembeni
15' ⚽Gooooooal, Pape Sakho anaweka kimiani goli la kwanza la mchezo, krosi maridadi kutoka kwa Chama
19' 🟨Aucho anapewa kadi ya njano
22' Kona ya kwanza ya mchezo inachongwa na Yanga, almanusura Aziz Ki aweke uwanja sawa
23' Inonga anamjaribu Diarra kutoka nje ya 18 lakini anakuwa makini na kuupangua nje
24' Mohammed Hussein anachonga kona ya kwanza ya Simba, mpira unakosa manufaa
33' Feisal anaenda chini baada ya kukwatuana na Mkude, free kick ya Yanga inashindwa kuleta matokeo kwa kuleta offside
37' Simba wanapata freekick nje kidogo ya 18, Kanoute anajaribu kuunganisha krosi ya Chama lakini Diarra yuko makini.
42' Mlinda mlango wa Simba yuko chini akitibiwa maumivu ya misuli
45+1' Inonga anainua kiatu juu ya Sureboy, inapulizwa filimbi na zogo linatokea
45+4' 🟨Sureboy anapewa kadi ya njano kwa kumletea ubabe Inonga
45+4' 🟨Inonga anapewa kadi ya njano kwa kumchezea ndivyo sivyo Abubakar Sureboy
49' ⚽ Mayeleeee anafanikiwa kutetema mapemaa kipindi cha pili, Yanga 1-1 Simba
55' Sakho anaachia mkwaju na kumgonga Dickson Job, mkwaju wa kona wa Simba unashindwa kubadili matokeo
57' Morisson na Ki wanacheza gonga langoni kwa Simba lakini beki wa Simba anatbua mipango
59' Inonga yuko chini baada ya kukwatuana na Aziz Ki
59' SUB: Simba wanafanya mabadiliko, Mzamiru na Okra wanaingia, Chama na Kanoute wanaenda nje
65' Yanga wanasaidiwa na mtambaa wa panya kuokoa mpira, jaribio zuri kwa Simba SC
69' SUB: 'Mzungu wa Simba' Dejan Georgijevićanaingia kuchukua nafasi ya Habib Kyombo
70' Almanusura Fiston aandikishe bao la pili, Quatarra anaweka mguu na kuhamisha mpira
72' Mayele anaukosa mpira, pasi ya wazi kutoka kwa Aziz Ki
78' Simba wanapata kona ya nne ya mchezo, Quatarra anapiga juuu
80' ⚽ Siku ya Kutetema, Fiston Mayele anaweka tena... Yanga 2-1 Simba
80' Dickson Job alimpa Mayele na Fiston akaachia mkwaju kwenye msitu wa wachezaji watatu wa Simba
83' Mayele anajaribu tena lakini Beno anakaa imara
84' SUB: Makambo Ebenezer anaingia kuchukua nafasi ya Fiston Mayele. Upande wa Simba Bocco anaingia
89' Morisson anaachia mkwaju unaopanguliwa na Beno Kakolaya
90+4' Kipenga kinapulizwa kuashiria mwisho wa mchezo. Mayele anawalaza na viatu Simba SC
Yanga SC anatwaa ngao ya Jamii na pazia la ligi kuu linafunguliwa rasmi. Yanga 2-1 Simba
=========
Tarehe imewadia.
Klabu mbili kubwa hapa nchini zinaenda kukiwasha uwanja wa Mkapa Dar es salaam.
Ikumbukwe kwamba mwaka jana walipokutana kwenye ngao ya jamii Yanga alipata ushindi wa goli moja lililofungwa na Fiston Mayele.
Je, mnyama mkali atalipiza kisasi au Yanga ataendeleza ubabe? Tutakuwa hapa kupeana taarifa.
Mchezo utaanza saa moja kamili jioni.
=============
Timu zote zimeshawasili Uwanja wa Mkapa.
Kikosi cha Simba
Kikosi cha Yanga cha leo
Timu zilipokuwa zikiingia uwanjani mapema leo:
Mchezo umeanza
01' Yanga wanamiliki mpira wakipiga pasi kadhaa.
11' Kibu Denis anaachia mkwaju na kuishia kwenye nyevu za pembeni
15' ⚽Gooooooal, Pape Sakho anaweka kimiani goli la kwanza la mchezo, krosi maridadi kutoka kwa Chama
19' 🟨Aucho anapewa kadi ya njano
22' Kona ya kwanza ya mchezo inachongwa na Yanga, almanusura Aziz Ki aweke uwanja sawa
23' Inonga anamjaribu Diarra kutoka nje ya 18 lakini anakuwa makini na kuupangua nje
24' Mohammed Hussein anachonga kona ya kwanza ya Simba, mpira unakosa manufaa
33' Feisal anaenda chini baada ya kukwatuana na Mkude, free kick ya Yanga inashindwa kuleta matokeo kwa kuleta offside
37' Simba wanapata freekick nje kidogo ya 18, Kanoute anajaribu kuunganisha krosi ya Chama lakini Diarra yuko makini.
42' Mlinda mlango wa Simba yuko chini akitibiwa maumivu ya misuli
45+1' Inonga anainua kiatu juu ya Sureboy, inapulizwa filimbi na zogo linatokea
45+4' 🟨Sureboy anapewa kadi ya njano kwa kumletea ubabe Inonga
45+4' 🟨Inonga anapewa kadi ya njano kwa kumchezea ndivyo sivyo Abubakar Sureboy
49' ⚽ Mayeleeee anafanikiwa kutetema mapemaa kipindi cha pili, Yanga 1-1 Simba
55' Sakho anaachia mkwaju na kumgonga Dickson Job, mkwaju wa kona wa Simba unashindwa kubadili matokeo
57' Morisson na Ki wanacheza gonga langoni kwa Simba lakini beki wa Simba anatbua mipango
59' Inonga yuko chini baada ya kukwatuana na Aziz Ki
59' SUB: Simba wanafanya mabadiliko, Mzamiru na Okra wanaingia, Chama na Kanoute wanaenda nje
65' Yanga wanasaidiwa na mtambaa wa panya kuokoa mpira, jaribio zuri kwa Simba SC
69' SUB: 'Mzungu wa Simba' Dejan Georgijevićanaingia kuchukua nafasi ya Habib Kyombo
70' Almanusura Fiston aandikishe bao la pili, Quatarra anaweka mguu na kuhamisha mpira
72' Mayele anaukosa mpira, pasi ya wazi kutoka kwa Aziz Ki
78' Simba wanapata kona ya nne ya mchezo, Quatarra anapiga juuu
80' ⚽ Siku ya Kutetema, Fiston Mayele anaweka tena... Yanga 2-1 Simba
80' Dickson Job alimpa Mayele na Fiston akaachia mkwaju kwenye msitu wa wachezaji watatu wa Simba
83' Mayele anajaribu tena lakini Beno anakaa imara
84' SUB: Makambo Ebenezer anaingia kuchukua nafasi ya Fiston Mayele. Upande wa Simba Bocco anaingia
89' Morisson anaachia mkwaju unaopanguliwa na Beno Kakolaya
90+4' Kipenga kinapulizwa kuashiria mwisho wa mchezo. Mayele anawalaza na viatu Simba SC
Yanga SC anatwaa ngao ya Jamii na pazia la ligi kuu linafunguliwa rasmi. Yanga 2-1 Simba
=========
Tarehe imewadia.
Klabu mbili kubwa hapa nchini zinaenda kukiwasha uwanja wa Mkapa Dar es salaam.
Ikumbukwe kwamba mwaka jana walipokutana kwenye ngao ya jamii Yanga alipata ushindi wa goli moja lililofungwa na Fiston Mayele.
Je, mnyama mkali atalipiza kisasi au Yanga ataendeleza ubabe? Tutakuwa hapa kupeana taarifa.
Mchezo utaanza saa moja kamili jioni.
=============
Timu zote zimeshawasili Uwanja wa Mkapa.
Kikosi cha Simba
Timu zilipokuwa zikiingia uwanjani mapema leo: