FULL TEXT: Maelezo ya Ushahidi wa Luhaga Mpina kwa Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson juu ya Waziri Hussein Bashe kusema Uongo Bungeni kuhusu Sukari

FULL TEXT: Maelezo ya Ushahidi wa Luhaga Mpina kwa Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson juu ya Waziri Hussein Bashe kusema Uongo Bungeni kuhusu Sukari

Hahaaa!! Mahakama ni kuthibitisha uhuni, unayo macho so ona acha kujizipa macho.
Baadhi ya wahuni hupendelea issue hata kama ni ya wazi kiasi gani ipelekwe kule, kwa sababu ya fedha inakuwa rahisi kutoa hukumu yoyote ile kwa mujibu wa fungu la mafedhwa.
 
MAELEZO MBUNGE WA JIMBO LA KISESA, MHE. LUHAGA JOELSON MPINA (MB) AKIWASILISHA USHAHIDI WA VIELELEZO KWA Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Tulia Ackon (Mb) kwa agizo lake la kunitaka mimi Luhaga Joelson Mpina, Mbunge wa Jimbo la Kisesa kutoa maelezo na ushahidi wa vielelezo bungeni ili kuthibitisha uongo uliosemwa Bungeni na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Mohamed Bashe Mnamo tarehe 4 Juni 2024. Lakini pia kuweka wazi ukweli uliofichwa na Waziri huyo kwa
View attachment 3019869
Spika alifanya unforgivable mistake ya kumtaka Mpina athibitishe uongo wa waziri tena akampa na muda kabisaa(kama sheria inavyotaka kwa mujibu wa maelezo yake spika)!

That was a colossal mistake,sometimes akili nyingi mbele giza kama wasemavyo waswahili.Spika alijitia kujua sana kumbe matokeo ya ujuaji yanakuja kumwaga unga wa waziri😂😂😂😂
 
Bashe wakati yupo nje alikuwa anaona kweli....kaingia uwanjani katoa assist kwa Mpinzani...kachoma
 
MAELEZO MBUNGE WA JIMBO LA KISESA, MHE. LUHAGA JOELSON MPINA (MB) AKIWASILISHA USHAHIDI WA VIELELEZO KWA SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. DKT. TULIA ACKSON (MB) KUHUSU WAZIRI WA KILIMO Mbunge wa Jimbo la Kisesa kutoa maelezo na ushahidi wa vielelezo bungeni ili kuthibitisha uongo uliosemwa Bungeni na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Mohamed Bashe Mnamo tarehe 4 Juni 2024. Lakini pia kuweka wazi ukweli uliofichwa na Waziri huyo kwa
View attachment 3019869
Kwa haya madudu kampuni za namna hii zikipata Viongozi makini wanaosimamia Sheria kama John Magufuli au Luhaga Mpina lazima watafute huruma kwa Wananachi ( walalamike ) kuwa wanaonewa.
 
Mbunge Luhaga Mpina kafanya kazi aliyo elekezwa aifanye.Ni kazi nzuri inayostahili pongezi.

Sasa sijui ni wabunge wangapi ndani ya Bunge hili wenye uwezo wa kufanya kama alivyofanya mbunge huyu.
 
Moderator mbona mmeunganisha uzi wa figganigga na huu??

Ingekua vyema uzi wa figganigga ukawa peke yake.
Mbona kama kuna kitu mnaficha??
Maana huu uzi ndio kosa la Mpina mpaka kaitwa, ila ule wa jamaa umechimba kilichokusudiwa na Mpina kifike kwa hadhira na bunge.

Ila ninyi JamiiForums mmeupachika huku ili usionekane bali lionekane kosa
Mngekua waungwana kama uzi wa figganigga ukawekwa pale chini ya video
 
Hahaaa!! Rudia kusikiliza vzr. Mpina alitoa kauli bungeni kuwa waziri bashe kalidanganya bunge, spika akamuomba kuleta ushahidi kwake kuthibitisha kuwa bashe alilidanganya bunge!! Wapi kuna jambo la mahakama hpo?
Mpina alitoa kauli bungeni kuwa waziri bashe kalidanganya bunge, spika akamuomba kuleta ushahidi
 
3.3.3 Kampuni ya Yasser Provision Store

Baada ya kufanya upekuzi wa ZBPRA na BRELA (Kiambatisho Na. 23) tarehe 13 Juni 2024 ilibainika yafuatayo:-

Kampuni hii imesajiliwa Wakala wa Usajili Biashara na Mali Zanzibar (ZBPRA) Tarehe 5 Januari 2016 na baadaye ilisajiliwa na BRELA na tarehe 4 Januari 2024 na kufungua Ofisi Mtaa wa Nyasubi, Kahama, Shinyanga.

Baada ya kupata usajili wa BRELA tarehe 4 Januari 2024, tarehe 29 Aprili 2024 akapewa kibali cha kuingiza tani 10,000 za sukari.

3.3.4 Kampuni ya ZENJ GENERAL MERCHANDISE COMPANY LIMITED

Baada ya kufanya upekuzi wa BRELA (Kiambatisho Na. 25) tarehe 10 Juni 2024 ilibainika yafuatayo:-

Kampuni hii haijawasilisha BRELA Financial Statements tangu mwaka 2016 hadi 2023 miaka 8 sasa. Kiufupi kampuni hili haliko hai na haliwezi kufanya biashara na Serikali.

Kampuni hii imesajiliwa Zanzibar lakini haijahuisha taarifa zake katika Mfumo wa Online Registration System (ORS) wa BRELA.

Kampuni hii imepewa vibali zaidi ya viwanda vyote 5 vinavyozalisha sukari nchini ambavyo vilipewa tani 10,000 kila kiwanda. Lakini pia uwezo wa kifedha wa kampuni hii ni wa kutilia mashaka kupewa kazi ya zaidi ya Bilioni 160.
Kama kawaida yao, Wazanzibar wanatumia vikampuni uchwara kufanya ufisadi Tanganyika
 
Yani kampuni inasajiliwa january 2024 halafu baada ya mwezi inapewa kibali cha kuagiza sukari tena kuwashinda viwanda ambavyo vipo toka miaka ya 60😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂!
Kwenye hili ni wazi hii ni kampuni ya Bashe😂😂😂😂 au ya mtu mkubwa
 
Moderator mbona mmeunganisha uzi wa figganigga na huu??

Ingekua vyema uzi wa figganigga ukawa peke yake.
Mbona kama kuna kitu mnaficha??
Maana huu uzi ndio kosa la Mpina mpaka kaitwa, ila ule wa jamaa umechimba kilichokusudiwa na Mpina kifike kwa hadhira na bunge.

Ila ninyi JamiiForums mmeupachika huku ili usionekane bali lionekane kosa
Mngekua waungwana kama uzi wa figganigga ukawekwa pale chini ya video
Correct
 
Kuna watu waliaema humu kuwa Mpina hana ushahidi, anabwabwaja tu.

Kashuka nondo hadi mimi darasa la saba nimeelewa.

Sukari Tanzania si tatizo. Tatizo ni serikali haitaki tupate sukari ya kutosha na kwa bei nafuu.
Halafu jitu linakuja hapa eti hoo mama amefungua nchi wakati anashinda angani huku tukiteseka kulipa kodi kubwa za mapato, halafu wajanja wanazitafuna kirahisi hivi.
Kwa summary yako mzee wa la saba kweli umeelewa. Bottom line ni kwamba wanatengeneza tatizo la uhaba wa Sukari kwa kuchelewesha vibali huku wakijua kitakuwa kipindi cha mvua, hivyo watengenezaji watashindwa kutenegeneza Sukari kumeet demand ya nchi, then baadae wakatengeneza mazingira ya wale walioruhusiwa kisheria kuagiza sukari nje (wale wenye viwanda vya sukari) wapewe short deadline ya kuagiza na kuingiza Sukari (almost two weeks wakati inatakiwa more than a month). Waliposhindwa the planned deadline, ikajengwa hoja sasa turuhusu privates waagize, na sio tu waagize kiasi stahili bali kiasi cha kuagiza kikawa inflated na kuzidishwa kuliko estimate sahihi iliyotolewa na mamlaka husika.

Kama haitoshi akaelezea financial implication ya vitendo hivyo. Kwa hiyo mzee wa la saba nakukubali umeweza kugundua in summary the real cause. Hii sukari kama wakitaka inaweza kuuzwa hata shillingi 1,500 Tsh kwa kilo ila ni watu wachache wanainflate price ili kupiga mabillioni hayo.Nchi ya ajabu sana. Kibaya anayewafumbua macho ndiye anahangamizwa kama mhalifu
 
Protectionism 101, jamaa si wazalendo kabisa. Hakuna nchi yeyote iliyowahi kuendelea kwa kutokulinda viwanda vya ndani. Ni mambo ya ajabu sana kwa kweli.
Bashe anasema, ni sawa mashamba ya miwa yakibadilishwa kuwa ya mpunga, hajui ajira za Watz zitakuwaje viwanda vikifungwa, haangalii quality ya sukari yetu Kwa AFYA ya Watz ukilinganisha na sukari fake ya GMO inayoongeza magonjwa ya ini na cancer Kwa Watz,

Alitakiwa awe lockup Kwa kauli hizo, lakini anakingiwa kifua.
 
Taarifa za ndani, kutoka jumba jeupe Hussein Bashe atakiwa kujiuzuru, lakini yeye amegoma hivyo mkeka muda wowote unatoka, pia Kinana anamkingia kifua lakini soon majibu yatapatikana.
Tuwe watulivu kipindiiki iki kigumu ambapo nchi inapita katika tanuru la moto.
nasimama na mpina ni wa moto,majizi ya ccm bado yanajiuliza hivi kweli huyu ni mwenzetu
 
Hili tatizo la sukari lipo miaka mingi sana nchini. Nakumbuka hata waziri Idi Simba lilimsumbua wakati wa Mkapa. Kuna hela nyingi sana kwenye hii kitu.

Dawa yake ni sisi wananchi kuacha kutumia sukari. Tutafute alternative yake.
 
Back
Top Bottom