Full Time: Mwadui FC 2 - 2 Simba SC kutoka dimba la CCM Kambarage, Sinyanga

Full Time: Mwadui FC 2 - 2 Simba SC kutoka dimba la CCM Kambarage, Sinyanga

Niko hapa uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga ambapo leo timu ya Mwadui FC inamkaribisha mnyama mkali wa mwituni, Simba SC na nitakuwa nakuletea mubashara yale yanayojiri mpaka pale mchuano huu utapoenda kuisha.

Tuwe pamoja kwa updates: Mwadui VS Simba

Kikosi cha Mwadui FC: Anold Massawe, Revocatus Richard, David Luhende, Joram Mgeveke, Iddy Mfaume, Awesu Awesu, Jean-Marie Girukwishaka, Paul Nonga, Evarigestus Mjwahuki, Miraji Athuman.

SUB: Dionis, Malaki, Salum, Matogolo, Rajabu, Mathias, Salvatory.

Kikosi cha Simba SC: Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohamed Hussein, Juuko Murshid, Yusuph Mlipili, Erasto Nyoni, Shiza Kichuya, Said Ndemla, Emmanuel Okwi, John Bocco, James Kotei.

SUB: Mseja, Ally Shomary, Mavugo, Gyan, Kazimoto, Yassin, Bukaba.

View attachment 696007
Muonekano wa dimba la CCM Kambarage


01' Mpira umeanza

02' Simba wanaendelea kupandisha mashambulizi kwenye lango la Mwadui

03' Timu zote zina uchu wa kufunga magoli lakini mara nyingi wanajikuta ktk kuotea

04'Mwadui wanashambulia lango la simba kupitia kwa Awesu.

05' Mpaka sasa hakuna shambulizi kali kwani timu zinacheza kwa umakini mkubwa hasa safu za ulinzi.

08'Beki wa Mwadui anatoa boko kwa kumpasia John Bocco mpira anadhibitiwa hapa.

09' Faul inapigwa kwenye lango la Mwadui
Goooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo
John Bocco anaipatia simba goli la kwanza baada ya faul iliyopigwa na Shiza Ramadhani Kichuya na Bocco akaiunganisha kwa kichwa ikajaa moja kwa moja golini.

10'Mpira unachangamka hapa baada ya simba kupata goli la kuongoza, okwi amekuwa naingia ndani lakini anadhibitiwa inakuwa ni kona, kona imepigwa lakini haijakuwa na madhara.

15'Mwadui wanafanya shambulizi lakini wanatoa nje

17'Okwi anambabatiza beki wa mwadui inakuwa ni kona, Kichuya anapiga kona fupi lakini haina madhara.

20' Kona inapigwa kwa mwadui, inatoka nje na inapigwa tena lakini haina madhara

23'Ndemla anapiga krosi lakini inawapita wenzake na kutoka nje.
25' Bocco kaumia na anagangwagangwa
26'Ndemla anapiga faul, kipa anadaka.

27'Mohamed Hussein anaoneshwa kadi ya njano kwa kuchelewesha mpira

28'Aweso amechezewa faul, faul inapigwa kuelekea lango la Simba.

29'John Bocco anatoka anaingia Mavugo.

31'Faul inapigwa kwenye lango la simba lakini inakuwa haina madhara

32'Miraji athumani anapata nafasi ya wazi baada ya kubakia na kipa lakini anashindwa kufunga.

33'Bocco anapokea shuti lilipigwa kama faul lakini anashindwa kufunga na kujikuta yupo offside.

36' Okwi anapga shuti moja kali lakini kipa analitema.

37'Simba wanaendelea kulisakama lango la Mwadui.

38'Okwi anamchezea beki wa Mwadui faul. Faul inapigwa kwenda lango la simba.

41'Awadhi Juma anapiga shuti kali kuelekea lango la Simba lakini linatoka nje.

44'Simba wanaanzisha tena mashambulizi kwenda lango la Mwadui

45'Kichuya anapiga shuti lakini kipa anaidaka.

45+1' Mwadui wanafanya shambulizi ila wanadhibitiwa

45+3' Mpira ni Mapumziko

Kipindi cha pili
45'Kipinidi cha pili kinaanza.

46' Kapombe anarusha mpira kuelekea Mwadui

50'Mwadui wanaongeza mashambulizi, na sasa wanapiga kona lakini inakuwa haina madadhara.

51'Mwadui wanashambulia lakini wanajikuta wapo offside.

55' Miraji Athumani anafanya shambulizi lakini mabeki wa Simba wanamdhibiti.

56'Paul Nonga ameitoa nje baada ya kupigiwa pasi ndeefu

57'Faul inapigwa lango la simba ni karibu kabisa na 18.

59' Gooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo
Duh!
 
Back
Top Bottom