msimamiakucha
Member
- Aug 24, 2016
- 18
- 7
Bora aende zake! Ametusaidia kiasi cha kutosha ila kama simba wamempa pesa nzuri ni jambo jema! Yanga ilikuwepo, ipo na itakuwepo! Ngoja tuomboleze kwanza msiba wa Alli Yanga!
Safi sana Yanga hii ndio yanga ninayoijua hakunaga kuremba
Habari iliyovunjikavunjika ninayoweza kuwapeni kwa sasa.
Haruna Niyonzima amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Simba. Yanga wameshindwa kumshawishi Niyonzima abaki kwa kuwa fedha aliyoitaka wameshindwa kumpa.
======
Klabu ya Yanga SC kupitia kwa Katibu Mkuu Boniface Mkwasa inapenda kuwajulisha wanachama, wapenzi na washabiki wa Yanga juu Mchezaji raia wa Rwanda Haruna Niyonzima ambaye amekua Mchezaji wetu kwa misimu 6 mfululizo katika kiwango cha juu.
TAARIFA KWA UMMA
Hata hivyo Haruna Niyonzima bado ana mkataba mpaka mwezi Julai na Yanga Sc, lakini hatutaweza kuendelea kuwa nae kwa msimu ujao kwani hatukuweza kufikia mwafaka katika mazungumzo yetu na yeye licha ya timu yetu kuwa na nia za kuendelea nae kwa misimu miwili ijayo.
Klabu inamtakia kila la kheri katika maisha yake na soka kwa ujumla.
Imetolewa na Idara ya Habari na Maelezo
Young Africans Sports club.
21-06-2017.
Mkuu ilikuwepo hiyo m 70,mwisho wa siku akapandisha m 120,juzi usiku ndio uongozi ulipong`amua alishasaini upande wa pili muda sana,alikuwa anasumbua tu!jana ndio wakaamua kuachana,binafsi namtakia kila la heri huko aendako
Kila la kheri, ana uwezo mkubwa ila sio waku demand 70/= Milioni.....
Kwani Ajibu kapewa ngap na Yanga..?Mkuu hakuna mchezaji Eastern Africa wa kustahil M 70/=
Licha ya kuwa uwezo anao
Sasa iyo pesa unatoa wewe adi upate maumivu?Safi sana.
Ni mchezaji mzuri lakini hana thamani ya Mil 70/= alizokuwa akizihitaji....
Umenena! Sio hao wengine wanakoment majungu tuNi haki yake jamani ingawa inauma.Acha akajaribu maisha kwingine!
Ukiachana na uwezo wa Haruna..Kwani Ajibu kapewa ngap na Yanga..?
Wachezaji ni wajanja sana. Niyo anaijua vyema tension ya suala la usajili lilivyo akaona ni opportunity ya kujenga fedha....Yaaani naukubali sana uongozi wa Yanga Sc, huwa hawana papara wala mihemko ya ajabu ajabu.
Wanaongoza club kisayansi zaidi (katika sauti ya Mwl kashasha)
3 times undisputed champion
Childish argument.Sasa iyo pesa unatoa wewe adi upate maumivu?
Ukiachana na uwezo wa Haruna..
Bila shaka ana uwezo wenye kupendeza, ila ni bora kuwekeza 70 MILIONI kwa Ajibu kuliko kwa Niyonzima
1. There is still untapped potential kwa Ajibu
2. He's still young ukimlinganisha na Niyo.
3. He's a local ..so it paves a way to recruit foreign player in the club.
4. In terms of final result productivity in midfield area, they equals in terms of goal capability.
Kama Ajibu atahusika msimu ujao, bado silioni pengo la Niyo.
Shukrani ya nini kiongozi .....Chirwa naye ameandika barua ya kuomba kuvunja mkataba, Ngoma haeleweki tangu katikati ya msimu, Tambwe eti naye anataka 80M ili asaini, daah hawa mapro hawana shukrani
Kwa miaka ya karibuni, siku Lunyamila alipoihama Yanga nilijua ndio mwisho wa Yanga...
Lakini haikuwa hivyo, nadhani hata kuondoka kwa fundi huyu hakutaiyumbisha timu.
Niyo kama mchezaji kashafanikiwa kwa karibu kila kitu Yanga, hakukuwa na challenges mpya zaidi ya makombe ya kimataifa ya CAF (ambayo of course hata akienda Simba hatapata)...
Hivyo kwake huu ndio muda wa kupiga mpunga wakati umri na kiwango vinaruhusu...
Sasa itakuwa zamu yao kumsubiri arudi kila akienda kwao.
Alikuwa mchezaji mzuri lakini value ya mchezaji inaendana na umri wake. Je kocha wa Simba atamkubali?
Haruna ni aina hiyo ya mchezaji ambaye suala la Ku turn up kwenye big games ....sanasana vs Simba amekuwa si wakutegemewa sana.Hayuko kwenye mipango ya mwalimu ..mechi za kimataifa anacheza chini ya kiwango..anashine mechi za jk ruvu.majimaji nk