Funzo la mapinduzi toka nchini Mali: Maafisa waaandamizi wa Serikali ya Tanzania tendeni haki na kwa usawa kwani hamuijui kesho yenu

Funzo la mapinduzi toka nchini Mali: Maafisa waaandamizi wa Serikali ya Tanzania tendeni haki na kwa usawa kwani hamuijui kesho yenu

CreativityCode

Senior Member
Joined
Aug 8, 2020
Posts
158
Reaction score
653
Kilichotokea nchini Mali na nchi mbalimbali duniani kuhusu viongozi madikteta kuondolewa madarakani kinatoa somo kwa maafisa waandamizi wa serikali ya Tanzania kwamba kwa kuwa hawaijui kesho yao basi ni vema kutenda haki na usawa kwa watu wote bila kujali vyama vyao vya siasa kwa kufuata katiba na sheria za nchi.

Ni bora kujiuzulu ikiwa agizo la Rais linapingana na katiba na sheria za nchi kuliko kushiriki katika uovu ambao utakuja kuwagharimu siku za usoni siku ambapo mnayemtetea mbele za watu hatokuwa na nguvu ya kuendelea kuwalinda.

Heshimuni vyama vyote vya siasa kwa mujibu wa katiba na sheria kwani leo ni CCM kesho ni CHADEMA. Dunia inakwenda kwa kasi sana na mabadiliko ya upepo wa kisiasa ni suala la siku moja tu.

KWA LEO NI HAYO TU, NAWATAKIA SIKU NJEMA
 
Haiwezekani ukatupa "full description" ya tukio zima ya nini kimetokea, kwa namna gani na mwisho ukawaje?
Jeshi la Mali Jana lilimkamata Rais wa Mali Aboubakar Keita na waziri wake mkuu na kuwalazimisha wajiuzulu Leo asubuhi , hii ni kufuatia maandamano ya nchi ya nguvu za umma kwa miezi isiyopungua mitatu, Rais kajiuzulu kavunja bunge na baraza la mawaziri , kitu cha kushangaza ambacho ni nadra kufanyika katika mapinduzi ni kwamba waliofanya mapinduzi ni Wanajeshi wa vyeo vya chini na wasiokuwa na vyeo kabisa , Wenye madaraka jifunzeni dunia inazunguka hasa Limbukeni wa kihutu ,Belarus nguvu ya umma inaendelea kumwondoa Lukashenko
Screenshot_20200819-113144.png
 
Jeshi la Mali Jana lilimkamata Rais wa Mali Aboubakar Keita na waziri wake mkuu na kuwalazimisha wajiuzulu Leo asubuhi , hii ni kufuatia maandamano ya nchi ya nguvu za umma kwa miezi isiyopungua mitatu, Rais kajiuzulu kavunja bunge na baraza la mawaziri , kitu cha kushangaza ambacho ni nadra kufanyika katika mapinduzi ni kwamba waliofanya mapinduzi ni Wanajeshi wa vyeo vya chini na wasiokuwa na vyeo kabisa , Wenye madaraka jifunzeni dunia inazunguka hasa Limbukeni wa kihutu ,Belarus nguvu ya umma inaendelea kumwondoa LukashenkoView attachment 1542089

Wooh, that's very good.

Asante kwa description nzuri na fupi.

Hata hapa Tanzania inawezekana kwa sababu wanaokula mema ya dikteta uchwara ni baadhi tu ya maafisa wa jeshi wa ngazi ya juu.

Hao ndiyo wanaohongwa vyeo na marupurupu ya fedha na vitu vingine kibao.

Hawa wa ngazi ya kati na chini kabisa "wanaisoma namba" kama ambavyo kila mmoja wetu anaisoma.
 
Jeshi huwa halina rafiki!

Wale wanaojifanya Jeshi wanalijua sana au wameliweka mfukoni wawe makini sana, maana wanaume wakiamua kuingia kitaa, ni hatari
Wanajeshi watakachofanya ni kukuheshimu.

Ila ikitikea wananchi wameandamana sana hawakutaki na maandamano yakiwa serious hao wanajeshi wanakugeuka dakika sifuri tu.
 
Wanajeshi watakachofanya ni kukuheshimu.

Ila ikitikea wananchi wameandamana sana hawakutaki na maandamano yakiwa serious hao wanajeshi wanakugeuka dakika sifuri tu.

Ndicho kilichotokea Misri 2011/2012...

Ilifikia hatua wanajeshi waliunga tela la waandamanaji...

Hosni Mubarak ilimlazimu kujisalimisha mwenyewe...

PEOPLE'S POWER (NGUVU YA UMMA) ni NGUVU YA MUNGU...
 
Haiwezekani ukatupa "full description" ya tukio zima ya nini kimetokea, kwa namna gani na mwisho ukawaje?
Mkuu, huyu ameshindwa kuandika ukweli, kilichomfurumusha huyo Raisi wa Mali ni kushindwa kudhibiti ufisadi ndani ya nchi yake, Jeshi likaona haina Maana kuwa wajeda waendelee kuona wizi ukitamalaki Wakati raia wengi wa nchi hiyo wanaishi maisha ya mateso na dhiki Ili Hali Utajiri wa nchi Yao ukigawanwa na wachache

Sasa anapokuja kulinganisha na hapa, Kwa kigezo kipi mpaka aseme Eti ni Bora hata hapa kufanyike kama Mali,

Nchi inavyojengwa kiasi hicho, kila mtu anaishi Kwa nguvu zake yeye mwenyewe, na Pesa inayopatikana inaonekana inafanya vitu, mafisadi wamebanwa mbavu hawapumui, Raisi aliyepo Sio pandikizi ni Mtanzania aliyewekwa na Watanzania,

Kwanza hao mapandikizi ndio inabidi wakataliwe kote Africa Ili Africa isonge mbele
 
Mali ni Mali na Tanzania ni Tanzania, hatuko hivyo!. Sisi ni watu piece sana!.
P
Kuna trend inajengeka katika nchi za Afrika, nchi ambazo viongozi wake wanaacha kuweka maslahi ya Taifa mbele. Mfano Mali, maelfu wanaandama kwa amani karibu miezi miwili, sasa ni bomu hili siku wakijaa jazaba nchi wataigawa damu itamwagika.

Wazalendo wa kweli wameingia, wameweka mambo sawa. Huendea tena baadhi wangeungana na wananchi na kwa vile wanasilaha, maandamano yangegeuka vikundi vya mapigano. Wamtoa kwa amani, wanaitisha uchaguzi, mali inaendelea kuwa salama.
 
Back
Top Bottom