Fursa gani zinadharauliwa lakini zinaweza kukutoa kimaisha?

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,286
Reaction score
6,736
Nikumbushe kisa kimoja cha ukweli kabisa ingawa ni cha siku nyingi. Yupo mchaga mmoja ambaye alikuwa amebahatika kupata ajira hapa Jijini, baada ya muda fulani akaamua kutafuta sehemu ambayo alifungua banda la chipsi. Alimwita mdogo wake kutoka nyumbani Moshi akamweka hapo. Baada ya Muda fulani yule bwana akapata Likizo, akaamua kumsaidia mdogo wake shuguli za chips.

Kwa mapato aliyoyaona muda huo mfupi akashtuka sana, akaamua kuacha kazi ili afanye
biashara hiyo ya Chipsi jambo ambalo lilileta mzozo na baba yake mzazi ambaye hakukubaliana kabisa na mpango huo huku akisisitiza kuwa yeye hakumsomesha aje kuuza chipsi.

Yule mchaga hakukubali, akaacha kazi na akafungua 'senta' nyingine ya Chipsi.....

Tuachane na huyo mchaga hebu nirudi kwenu wadau naomba tupeane uzoefu hapa
ni fursa gani ambazo macho ya kawaida haizioni kuwa Fursa za maana lakini zinaweza
kukupaisha Kimaisha?
 
Kweli mkuu, kuna vitu vya ajabu sana nimeviona ambavyo unaweza kuvifanya maeneo
ambayo watu hawafikirii kabisa na ukaingiza pesa nyingi sana.
Sasa Mbona Unataja Tuu Fursa umeziona lakini Huzitaji?
Taja Mkuu tuchangie Hapa,unasema umeviona vitu unavyoweza kuvifanya maeneo ambayo Watu hawafikirii Kabisa sema basi Mkuu Nasi tutoe Mawazo yetu huenda Tukachangia nawe ukafaidika!
 
Umejiandaa vizuri hela ya chakula?
Na hapo nyuma umeshawahi jaribu kufuga?
Haha ha ha ha ha Watu wanawachukulia kuku Rahisi sana!! Kuku wanalipa sana lakini
sio mtaji wa kitoto ule, Inatakiwa ukaze msuli kwelikweli uache mambo yako mengi na
uwe na 'usiriasi' hautaki masihara, nikianza kuelezea hapa ninavyowajua wanJF wataanza
kuniuliza kwanini umeacha kufuga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…