Fursa gani zinadharauliwa lakini zinaweza kukutoa kimaisha?

Fursa gani zinadharauliwa lakini zinaweza kukutoa kimaisha?

Kuna jamaa aliacha kazi ya ualimu tena sayansi sekondari na kufanya kazi ya genge. Wazee wake wakamuita bonge la TAAHIRA " alitengwa kwa ujinga wake. Hakika leo ametoboa ana duka la uhakika na kodi zote analipa. Kwa kuwa ni mtu wa hesabu aliangalia tu mwisho wa siku unaingiza ngapi akagundua ni nyingi kuliko mshahara. Familia sasa inamheshimu .
 
Nikumbushe kisa kimoja cha ukweli kabisa ingawa ni cha siku nyingi. Yupo mchaga mmoja
ambaye alikuwa amebahatika kupata ajira hapa Jijini, baada ya muda fulani akaamua
kutafuta sehemu ambayo alifungua banda la chipsi. Alimwita mdogo wake kutoka nyumbani
Moshi akamweka hapo. Baada ya Muda fulani yule bwana akapata Likizo, akaamua kumsaidia
mdogo wake shuguli za chips.

Kwa mapato aliyoyaona muda huo mfupi akashtuka sana, akaamua kuacha kazi ili afanye
biashara hiyo ya Chipsi jambo ambalo lilileta mzozo na baba yake mzazi ambaye hakukubaliana
kabisa na mpango huo huku akisisitiza kuwa yeye hakumsomesha aje kuuza chipsi.

Yule Mchaga hakukubali, akaacha kazi na akafungua 'senta' nyingine ya Chipsi.....

Tuachane na huyo mchaga hebu nirudi kwenu wadau naomba tupeane uzoefu hapa
ni fursa gani ambazo macho ya kawaida haizioni kuwa Fursa za maana lakini zinaweza
kukupaisha Kimaisha?
Ni shughuli yeyote inayozarauliwa na wasomi ukiifanya kisomi ni rahisi kutoka,kuanzia kuuza chips,takeaway,kuuza Mihogo, Viazi,mkaa, nk,unaweza fanikiwa
 
Haha ha ha ha ha Watu wanawachukulia kuku Rahisi sana!! Kuku wanalipa sana lakini
sio mtaji wa kitoto ule, Inatakiwa ukaze msuli kwelikweli uache mambo yako mengi na
uwe na 'usiriasi' hautaki masihara, nikianza kuelezea hapa ninavyowajua wanJF wataanza
kuniuliza kwanini umeacha kufuga.
Umejiandaa vizuri hela ya chakula?
Na hapo nyuma umeshawahi jaribu kufuga?
Nakazia
 
Yaani mkuu kila ninapofikiria kuhusu hiyo Project naiona kama ngumu sana
nimewahi kuwaza kujaribu lakini naiona kama inahitaji utaalamu mkubwa
lakini nitaifuatilia.
Kama huna utaalamu ajiri, au tafuta mtaalamu mshirikiane yeye atoe usimamizi na ujuzi wwe toa mtaji.faida mgawane nusu kwa nusu.
 
Kufuga n'nge
Ile sumu yake ni dili watu tunauza hiyo
Try that u will be a billionea just like me
 
Haswaa GAZETI hata mwenyewe nilikuwa nashangaa ni kitu gani kimemkuta huyu legendary wa ufugaji wa kuku? wakati hapa karibuni nimeubamba uzi fulani wa miaka ya nyuma huko wa kuku wa kienyeji na uliplay part kubwa sana kutoa elimu hiyo ya ufugaji,basi sasa amani imerejea maana hapa nipo kudraft wazo la ufugaji kuku wa kienyeji kwa kutumia madini yako na ya bwana Kubota naimani kwa elimu yenu ile iliyotukuka hakika mwezi kama huu nitakuwa mtu tofauti na mwaka huu.
Mkuu kwenye ufugaji ninarudi tofauti sana mara hii, nimepata eneo la kutosha ambalo naweza kulima na kufuga.
 
Kila sIku nafikiria kuanzisha biashara ya kukaanga mihogo maeneo ya Posta. Mihogo yenyewe inaweza kuwa sio fursa sana ila fursa itakuwa kwenye matangazo ya hiyo muhogo.Nitatangaza kuwa mihogo hii inaongeza nguvu za kiume. Halo ndipo fursa ilipo..
Ha ha ha ha Kuna dada nilimkuta anazunguka na beseni lenye muhogo na kipande
cha nazi, tukapanda basi moja la kuelekea stesheni. Akaanza kusifia jinsi Muhogo na
nazi ukitafuna kwa pamoja unavyoleta heshima huko nani...... Ile tunasimama tu niliona
jinsi wanaume walivyokua wananunua muhogo na kipande cha nazi.....
 
Tafuta kijiji chenye shida ya maji na kiwe karibu na vijiji vingine ambavyo vina tatizo kama hilo,, fanya upelelezi kuhusu mpango wa Serikali kwenye suala la maji kwa maeneo hayo.. kama haina mpango wa kuleta maji au mipango yao ni ya muda mrefu sana basi piga makofi kwa visigino..
Tafuta wataalam wa uchimbaji wa visima virefu wafanye survey kama eneo hilo lina uwezo wa kupatikana maji basi chimba na anza kupiga pesa.
NB: Uwe na mtaji wa kutosha kuweza kununua eneo, kuchimba kisima na ikiwezekana uwe na gari la kusupply maji kwenye vijiji vya jirani.
Hii nimeifanyia kazi mkuu, sijachimba kisima ile nimenunua lile simtank napakiza
kwenye Pickup.
 
Ha ha ha ha Kama utani lakini ni kweli kabisa ingawa kwa upande fulani ile
ni biashara ya Kamari.
Maisha kwa ujumla ni kamari kuna kupata na kuna kuchana mkeka.mwezi mmoja kabla ya msimu kuanza nitakuwa huko kusini kwa ajili ya kubeti.
 
GAZETI nikumbushe kidogo kama hutajali,hivi ulikuwa unafuga kuku wa kienyeji? kama ndio uliwafuga kwa njia ipi? binafsi baada ya kuwa well equiped na elimu yenu ile na Kubota naanzisha mradi wa kuku 50 mitetea ifikapo JULY na projection yangu mwakani mwezi JULY niwe na kuku wa kuuza wasiopungua 1500.
 
GAZETI nikumbushe kidogo kama hutajali,hivi ulikuwa unafuga kuku wa kienyeji? kama ndio uliwafuga kwa njia ipi? binafsi baada ya kuwa well equiped na elimu yenu ile na Kubota naanzisha mradi wa kuku 50 mitetea ifikapo JULY na projection yangu mwakani mwezi JULY niwe na kuku wa kuuza wasiopungua 1500.
Kwanza niweke wazi, sijawahi kufuga wa kisasa. Niliwafuga kwa mfumo mchanganyiko
wapo niliowafuga Nusu huria, huria na wa kuwafungia moja kwa moja. baada ya mavuno
ya ule mradi mkubwa nikaanza kamradi kadogo sana, nilianza na kuku 11... Niamini
kuku ni kuku tu hawadanganyi, huko walikuwa wananiambia nina mkono wa Kuku lakini
si kweli ni uangalizi tu. kuku 11 ambao niliwanunua kwa Tsh Elfu 10 mpaka Elfu 14 nilikuja kuvuna
Kuku 378. kuna mtetea mmoja huyo alikuwa balaa, watoto wake niliwaweka humu Jf nikiwa
nimewapaka Rangi. Yaani huyo sijamuuza nimempa tu mtu amfuge na asipoteze mbegu yake.
Alikuwa na uwezo wa kutotoa vifaranga 16 na vyote vikapona na kizazi chake kilikuja
na mtindo huohuo.
 
Back
Top Bottom