Fursa gani zinadharauliwa lakini zinaweza kukutoa kimaisha?

Kuna jamaa aliacha kazi ya ualimu tena sayansi sekondari na kufanya kazi ya genge. Wazee wake wakamuita bonge la TAAHIRA " alitengwa kwa ujinga wake. Hakika leo ametoboa ana duka la uhakika na kodi zote analipa. Kwa kuwa ni mtu wa hesabu aliangalia tu mwisho wa siku unaingiza ngapi akagundua ni nyingi kuliko mshahara. Familia sasa inamheshimu .
 
Ni shughuli yeyote inayozarauliwa na wasomi ukiifanya kisomi ni rahisi kutoka,kuanzia kuuza chips,takeaway,kuuza Mihogo, Viazi,mkaa, nk,unaweza fanikiwa
 
Umejiandaa vizuri hela ya chakula?
Na hapo nyuma umeshawahi jaribu kufuga?
Nakazia
 
Yaani mkuu kila ninapofikiria kuhusu hiyo Project naiona kama ngumu sana
nimewahi kuwaza kujaribu lakini naiona kama inahitaji utaalamu mkubwa
lakini nitaifuatilia.
Kama huna utaalamu ajiri, au tafuta mtaalamu mshirikiane yeye atoe usimamizi na ujuzi wwe toa mtaji.faida mgawane nusu kwa nusu.
 
Kufuga n'nge
Ile sumu yake ni dili watu tunauza hiyo
Try that u will be a billionea just like me
 
Mkuu kwenye ufugaji ninarudi tofauti sana mara hii, nimepata eneo la kutosha ambalo naweza kulima na kufuga.
 
Kila sIku nafikiria kuanzisha biashara ya kukaanga mihogo maeneo ya Posta. Mihogo yenyewe inaweza kuwa sio fursa sana ila fursa itakuwa kwenye matangazo ya hiyo muhogo.Nitatangaza kuwa mihogo hii inaongeza nguvu za kiume. Halo ndipo fursa ilipo..
Ha ha ha ha Kuna dada nilimkuta anazunguka na beseni lenye muhogo na kipande
cha nazi, tukapanda basi moja la kuelekea stesheni. Akaanza kusifia jinsi Muhogo na
nazi ukitafuna kwa pamoja unavyoleta heshima huko nani...... Ile tunasimama tu niliona
jinsi wanaume walivyokua wananunua muhogo na kipande cha nazi.....
 
Hii nimeifanyia kazi mkuu, sijachimba kisima ile nimenunua lile simtank napakiza
kwenye Pickup.
 
Ha ha ha ha Kama utani lakini ni kweli kabisa ingawa kwa upande fulani ile
ni biashara ya Kamari.
Maisha kwa ujumla ni kamari kuna kupata na kuna kuchana mkeka.mwezi mmoja kabla ya msimu kuanza nitakuwa huko kusini kwa ajili ya kubeti.
 
GAZETI nikumbushe kidogo kama hutajali,hivi ulikuwa unafuga kuku wa kienyeji? kama ndio uliwafuga kwa njia ipi? binafsi baada ya kuwa well equiped na elimu yenu ile na Kubota naanzisha mradi wa kuku 50 mitetea ifikapo JULY na projection yangu mwakani mwezi JULY niwe na kuku wa kuuza wasiopungua 1500.
 
Kwanza niweke wazi, sijawahi kufuga wa kisasa. Niliwafuga kwa mfumo mchanganyiko
wapo niliowafuga Nusu huria, huria na wa kuwafungia moja kwa moja. baada ya mavuno
ya ule mradi mkubwa nikaanza kamradi kadogo sana, nilianza na kuku 11... Niamini
kuku ni kuku tu hawadanganyi, huko walikuwa wananiambia nina mkono wa Kuku lakini
si kweli ni uangalizi tu. kuku 11 ambao niliwanunua kwa Tsh Elfu 10 mpaka Elfu 14 nilikuja kuvuna
Kuku 378. kuna mtetea mmoja huyo alikuwa balaa, watoto wake niliwaweka humu Jf nikiwa
nimewapaka Rangi. Yaani huyo sijamuuza nimempa tu mtu amfuge na asipoteze mbegu yake.
Alikuwa na uwezo wa kutotoa vifaranga 16 na vyote vikapona na kizazi chake kilikuja
na mtindo huohuo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…