Fursa kwa vijana 240 walio hitimu mafunzo ya mifugo

Fursa kwa vijana 240 walio hitimu mafunzo ya mifugo

Joined
Oct 10, 2018
Posts
38
Reaction score
44
Habari kwa wote.

Nimeliona tangazo la wizara toka kwa Mh. Mashimba Ndaki , ni fursa nzuri kwa vijana japo wigo umebanwa kidogo maana wamepewa wahitimu wa mafunzo ya mifugo kwa ngazi ya astashahada,stashahada au shahada kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali. Pia ni fursa kwa raiawaTanzania na kigezo cha tatu ni umri wa miaka 18-30

Naomba kutoa ofa kwa vijana watatu watakaoenda kwenye usaili (mmoja atakuwa wa astashada,stashahada na shahada ), nitawachangia garama za usafiri toka alipo mpaka kwenye kituo chake atamizi. Nitahitaji kuona cheti cha muhitimu husika . Nitafanya mazungumzo na vijana 12 ambao nitawagawa kwa idadi ya wanne wanne halafu nitachukua mmoja atakayekuwa ametetea vizuri kwanini apewe nafasi yeye.

Mmoja kati ya hawa watatu nitamlipia na kumgharamikia nauli,malazi na chakula kwa muda wa wiki moja kama lilivyoelekeza tangazo.

Nipate nakala ya cheti cha mafunzo ya mifugo na mawasiliano ya simu kupitia "bigstep2021@gmail.com"


Wasalaam.
 

Attachments

Habari, mi nimehitimu stashahada ya afya ya mifugo mwaka huu, results bado ila wahusika waturuhusu kuapply, wasema tu attach nakala za cheti cha kuzaliwa, kidato cha 4 au 6 na barua ya uthibitisho toka chuoni
Vip naruhusiwa kua kwenye ofa yako..?
 
Habari, mi nimehitimu stashahada ya afya ya mifugo mwaka huu, results bado ila wahusika waturuhusu kuapply, wasema tu attach nakala za cheti cha kuzaliwa, kidato cha 4 au 6 na barua ya uthibitisho toka chuoni
Vip naruhusiwa kua kwenye ofa yako..?
Omba kwa njia zozote kama watakuita kwenye usaili nafasi utakuwa nayo iwapo utatoa utatetea nafasi hiyo zaidi ya wengine. Karibu
 
Back
Top Bottom