Fursa za biashara nchini India (tujuzane)

Malick M. Malick

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2013
Posts
658
Reaction score
312
Wanabodi nilikua naomba kupatiwa kuhusu biashara za nywele za kichwani za kina dada,mwenye uzoefu na India nilikua naomba utupatie taarifa,alieniletea aliniambia amechukua BOMBAY(INDIA) ila hafunguki zaidi

  • gharama za viza ya india
  • gharama za nauli
  • gharama za hoteli
  • maduka maeneo gani(ya bei nafuu)
  • kama kuna baadhi ya watanzania wanakwenda kibiahara huko wanaweza kutupatia taarifa zaidi
Maana nimepata soko zuri la nywele kutoka India nililetewa mzigo kidogo, zinakimbia sana

  • kama nitapata mtu aliyehuko itakua vizuri
  • pia naomba na changamoto zilizopo na fulsa zingine zilizopo huko
  • MSAADA TAFADHARI,nategemea dec 15 nianze safari ya kwenda huko
 
Fulsa = Fursa

Ndio ulichojua tu kusahisha lugha Haya nenda kwenye mada husika.

Ila ujue kwamba kiswahili kinatofautiana kulingana na nchi.Kiswahili cha Rwanda,Congo,Burundi, Kenya na Tanzania vinatofautiana usitake watu wafate swahili ya Bongo,JF ina member wa kila nchi.

Kama hauna cha kujibu bora unyamaze tu
 

Cha India mbona umesahau?
 
Ndio ujue kiswahili kinatofautiana .Kiswahili cha Kanjibai hakiwezi fanana na shaban

Kijana, Kiswahili ni kimoja tu zinazotofautiana ni lafdhi. Mombasa, wakikuita wanakwambia "ndoo"" sisi tunasema "njoo" lakini wakiandika wanaandika "njoo" na hawaandiki "ndoo".

Kanjibhai ambae hajakulia na Waswahili, akisema "wewe" atatamka "veve" lakini akiandika haandiki "veve" ataandika "wewe".

Kutofautiana lafdhi si kuwa lugha ni tofauti.

Mfano mwingine ni tofauti ya maneno yanayotumika, mfano, Zanzibar "bomba" wanasema "mfereji" na mfereji huku kwetu kwetu ni kitu kingine kijulikanacho pia kama "mtaro" lakini mfereji kuuandika "mfeleji" au mtaro kuuandika "mtalo" ni kosa la kuandika Kiswahili na si kuwa lugha zimetofautiana.

Soma kijana, una mengi ya kujifunza.
 
kwahiyo hapo ndio unajadili na maada iliyowasilishwa? ndomana naogopa kuzeeka
 
kwahiyo hapo ndio unajadili na maada iliyowasilishwa? ndomana naogopa kuzeeka

Mada si msahafu ambao huwezi kuongelea mengine au kuingiza mengine.

Hizi mada hapa hazina tofauti na vijiwe vyovyote vile, na ndiyo raha ya mnakasha, siyo mkazanie biashara ya India tu bila kuelimishana mengine.
 
Ok basi yameisha tuendelee na mada sababu hili ni eneo la kujifunza business na sio kiswahili. sehemu ya lugha ina mahali pake kwenye jukwaa la lugha.
 

Na wewe hapo kwenye red umemaanisha nini?? usimnyoshee mwenzako kidole wakati we mwenyewe yanakukuta, huo ni uchapiji tu na ni jambo la kawaida!
Cha msingi tujaribu kumsaidia mtoa mada ili aweze kufanikisha haja yake.

lafdhi = lafudhi
 
Na wewe hapo kwenye red umemaanisha nini?? usimnyoshee mwenzako kidole wakati we mwenyewe yanakukuta, huo ni uchapiji tu na ni jambo la kawaida!
Cha msingi tujaribu kumsaidia mtoa mada ili aweze kufanikisha haja yake.

lafdhi = lafudhi
=uchapaji. :teeth: kazi ipo leo. haya jamani tuhamie kwenye mada.....
 
Na wewe hapo kwenye red umemaanisha nini?? usimnyoshee mwenzako kidole wakati we mwenyewe yanakukuta, huo ni uchapiji tu na ni jambo la kawaida!
Cha msingi tujaribu kumsaidia mtoa mada ili aweze kufanikisha haja yake.

lafdhi = lafudhi

Wewe Kiswahili umejifunza kuanzia shule, mimi Kiswahili ni lugha mama. Lafdhi ni sahihi, tena kwa kuringa kabisa.
 
Na wewe hapo kwenye red umemaanisha nini?? usimnyoshee mwenzako kidole wakati we mwenyewe yanakukuta, huo ni uchapiji tu na ni jambo la kawaida!
Cha msingi tujaribu kumsaidia mtoa mada ili aweze kufanikisha haja yake.

lafdhi = lafudhi

Imetosha sasa, msaidieni mleta uzi kulingana na ombi lake. Hayo mashindano ya lugha yatafutieni mahala pake.
Ova
 
Fulsa = Fursa

Cha India mbona umesahau?


Mada si msahafu ambao huwezi kuongelea mengine au kuingiza mengine.

Hizi mada hapa hazina tofauti na vijiwe vyovyote vile, na ndiyo raha ya mnakasha, siyo mkazanie biashara ya India tu bila kuelimishana mengine.

= fursa

= TAFADHALI

Wewe Kiswahili umejifunza kuanzia shule, mimi Kiswahili ni lugha mama. Lafdhi ni sahihi, tena kwa kuringa kabisa.

Kiswahili hukijui na huyo mnaemfata aliyebadili kutoka lafdhi kuwa "lafudhi" pia kachapia.

Unajisikiaje kuwa umeharibu uzi wa mwenzako ambaye ameomba msaada kwa ajili ya kutaka kujikita kwenye biashara?
Hutaki asaidiwe? Hutaki apanuke kibiashara? Unasumbuliwa na roho mbaya na wivu kwa muanzisha uzi? Sijakuelewa kabisa.
Ova
 
Guys tuijadili mada,I have a friend yupo huko maybe I could ask them kuhusu hiyo kitu,ulikuwa unaulizia nywele za inch zipi na zipi coz kuna 16,14,26 inches
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…