Fuvu la binadamu ndani ya Ofisi ya Diamond

Fuvu la binadamu ndani ya Ofisi ya Diamond

Kama ni kweli sijui.ila kwa kawaida ya watanzania ni kawaida kuwa na back up plan.hiyo ni.power bank ya maisha.aaaaahahahaaaaaaaaaa kwikwiikwiwikikiwwwe
 
Uchawi bila maarifa na kujituma haufanyi kazi! Shauri yenu karieni uchawi mwenzenu anapiga hela.
 
KIMENUUUUUKA>>DIAMOND MCHAWI:....FUVU LA BINADAMU LAKUTWA OFISINI KWA DIAMOND.............FULL MKANDA UPO HAPA NA PICHA ZOTE ZA TUKIO




    • Fuvu la binadamu lakutwa limewekwa kwenye meza ya Diamond pembeni ya picha ya mwanawe Tifah.
    • Diamond asema ni kweli ni fuvu la binadamu, ila ni pambo tu kama mapambo mengine, yeye anamtegemea Mungu.
Diamond-2.jpg

Wakati mwenyewe akikanusha vikali kwamba hatumii ndumba kwenye muziki wake ambao sasa umemfikisha mbali kimataifa, staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’, ameshikwa uchawi kufuatia kukutwa laivu kwa fuvu la binadamu ndani ya ofisi zake.

Fuvu hilo liko mkono wa kushoto mezani kwa Diamond huku jirani yake kukiwa na picha ya mwanaye, Latiffah Nasibu ‘Princess Tiffah’ iliyokuwa kwenye fremu.

Shuhuda mmoja aliyehudhuria hafla ya kusaini mkataba wa dili jipya alilosaini Diamond la Ubalozi wa Tomato Sauce ofisini kwake hapo alilithibitishia kuwepo kwa fuvu hilo lilozua gumzo kwa mashuhuda wachache wa tukio hilo.

“Ni kweli kuna fuvu la binadamu mezani kwa Mond (Diamond) but (lakini) sikufanikiwa kulishika kwa mikono yangu,”

Shuhuda mwingine aliripoti pia:

"Kuna ishu tumeishuhudia kwa macho yetu hapa ofisini kwa Diamond. Hata sisi imetushtua, ...hapa WCB, kwanza Diamond mwenyewe yupo. Ukifika ofisini kwake, tena kwenye meza yake (Diamond) mwenyewe kuna fuvu la binadamu kabisa.”

"Jamani ni fuvu la binadamu kabisa lenye mifupa. Inawezekana ndiyo chanzo cha utajiri wake na skendo inayomkabili ya uchawi katika kazi zake. Ninyi fuatilieni mtapata ukweli."

Mapema wiki hii, wageni mbalimbali waliofika kwenye ofisi za mkurugenzi huyo wa Kampuni ya Wasafi Classic Baby (WCB), Diamond au Mond zilizopo Mapambano-Sinza jijini Dar, walitonya kuwa, wengi walishtushwa na fuvu hilo baada ya kuliona mezani kwa mwanamuziki huyo.

“Hata mimi nimelishuhudia hilo fuvu kwa macho yangu wala sijasimuliwa na nina picha zake kwenye simu yangu (huku akiperuzi kwenye smartphone). Kiuweli limezua sana minong’ono. Baadhi ya watu wanadai ni mambo ya uchawi na wengine wanasema ni moja ya alama ya Freemasons (jamii ya siri inayohusishwa na utajiri). Unajua fuvu la binadamu ni moja ya Alama za Freemasons na kama unavyojua Diamond amekuwa akitajwatajwa."

“Wapo wengine wanadai labda mambo hayo ndiyo chanzo cha utajiri wa jamaa (Diamond) wa
ghafla lakini yeye mwenyewe ndiye mwenye kuufahamu ukweli."

“Lakini unajua kunapokuwa na ishara kama hizi (kukutwa kwa fuvu) ni rahisi sana kwa mashabiki wake ambao ni wengi kuhusisha na huu utajiri wake unaotajwa kufikia (shilingi) bilioni nane kwa sasa,” alidai mgeni huyo.

DIAMOND AFUNGUKA
Baada ya kupokea ushuhuda na madai hayo mazito ya Diamond kuhusishwa na uchawi na Freemasons kufuatia kukutwa kwa fuvu hilo ofisini kwake, gazeti hili lilimfuata Diamond ofisini kwake lakini alikuwa ametoka.

Alipotafutwa kwa njia ya simu alifunguka kwa kifupi huku akidai kuwa fuvu hilo ni pambo tu kama mapambo mengine.

“Ni urembo au pambo kama mapambo mengine, hakuna kitu kama hicho,” alisema Diamond na alipobanwa kueleza alikolitoa na gharama zake alisema:
“Usidanganyike, hakuna anayeweza kumuweka mtu juu zaidi ya Mwenyezi Mungu.

“Mimi naswali sana na namtegemea Mungu kwa kila kitu na kweli ananipigania.
“Unajua watu wengi wamekuwa wakizungumza oooh…natumia uchawi lakini ukweli ni kwamba maombi, ubunifu, juhudi na heshima ndivyo vitu vinavyoweza kumfanya mtu yeyote kupata mafanikio katika kitu akifanyacho au jambo alifanyalo.”

HUKO NYUMA
Mara kadhaa Diamond amekuwa akihusishwa na matumizi ya nguvu za giza katika kufanikiwa lakini amekuwa akisisitiza kuwa siri ya mafanikio yake ni kujituma, kutafuta fursa na kuipenda kazi yake ya muziki ili sanaa ya Bongo ifike mbali.

chanzo.KIMENUUUUUKA>>DIAMOND MCHAWI:....FUVU LA BINADAMU LAKUTWA OFISINI KWA DIAMOND.............FULL MKANDA UPO HAPA NA PICHA ZOTE ZA TUKIO - bongospy
 
Aliye mkuta ni nani? Na sheria inasemaje? Na hatua gani imechuliwa au magazeti ya ukadu ili wauze?
 
Najua wengi mnampenda huyo mwanamziki kupitiliza, fuvu ni masonic symbol wanatumia kwenye chama Chao cha skull and bones.
 
Kijana ana sema ni pambo kama mapambo mengine yaweza kuwa kweli na mimi simtizami kwenye uchawi ila kwa mshangao kidogo ni kama mwaka huu ame uanza na mapambo yasiyo na muonekano wa kawaida mara Kifuvu,mara kipini cha puani na sijui nini kitafuata ila huu mwelekeo ndio unao nishangaza kidogo na sijui kama utakuwa na mwisho mzuri.
Kinachofata ni mikolabo mikali.
 
Kwa vile watanzania tumezoea kuwa wa mwisho kila jambo akitokea mmoja kujitutumia basi ni UCHAWI, Lulu pia aliambiwa amefanya kafara, TUSIWALAUMU WAANDISHI WETU NA HATA WATANZANAI WENGINE, HAWAJAZOEA KUWA JUU, Tumezoea kushika mkia tu, Diamond fanya yako, kama uchawi unakuweka juu basi na hao wengine si wangefanya wakabaki juu, Na Diamond kama wanayohisi ni kweli, ujue unamkosea Mungu kwa kiwango kikubwa, Mungu hasamei dhambi ya Ushirikina.
 
Je wawajua waovu chimbuko la uovu duniani?

Ni jamii siri ya Jamaa nyingi za siri wa wazao uovu Kwa kujinufaisha binafsi. Jamii hizi zipo nyingi mno ila pia sio zote zenye mipango ya kutumia vibaya usiri wa jamii zao siri yaani secret societies,Kwani wapo wenye nia nzuri tuu ila shida huja pale tusipoweza kuusemea moyo na kwa zana ya usiri wengi wamekuwa wakijificha kwenye jamii hizi siri na kutenda maovu.
Mfano ni jamii siri ya jamii ya freemasonry ambao wapo na makundi mengi tuu na baadhi waongozwao na hofu ya Mungu wamejitolea kuuenzi uumbaji na kutenda mema ya uumbaji(yang/positivity/mema/mianga) na wapo waliotekwa na giza na kuliishi giza la uumbaji wao na mkuu wao shetani waishio giza lao(ying/negativity/uovu/giza).
Kutokana na usiri wa jamii zao imekuwa no vigumu kuusemea moyo kwa kuwa usiri huu sio tuu kwa wasio wa vikundi vya jamii zao bali hata wao kwa wao ndani ya vikundi vyao na ngazi zao.utumkuta kiongozi wako kwenye kikundi moyo na siri zake ni uovu nae huishiriki madhabahu ya uovu ila we we wa chini yake kamwe usijue ila ukiwa na shauku ya uovu wake wawezi mshawishi kukukuza kwenda nngazi za juu na kuuishi uovu na madhabau yake huku wachini yako akiendelea kuumini kwamba yupo sahihi mahali sahihi akitumikia madhabahu sahihi ila kiukweli yeye huwa chambo ya kuwavuta walio vuguvugu na siku wakikomaa na kufanya maamuzi hujikuta kupanda cheo na kuwa kiongozi kwa malengo na makusudio yao yapewayo nguvu kwa usiri wao wauliao kiaopo na hata kuwa radhi kuuawa kuitunza siri yao.
Swali langu kwa Diamond, je anatambua kwamba Mafuvu ni ishara ya jamii hizi maalum kwa jina la SKULLS AND BORNS?
Skull and borns
ni jamii siri yeye maovu lukiki nao huutumia mziki kwa manufaa ya uovu wao kwa madhabau zao za kishetani na ushetani wao.
Huenda asilijue hili kwa sababu tajwa hapo juu,ila akawa muhanga adhaniae kikawaida kawaida kwamba ni jambo la kikawaida kutumia fuvu nae apatapo msaada wa hapa na pale toka kwenye jamii hii na kujikuta amelowea na kuitoa kafara jamii yetu ya Tanzania kwa faida za malengo ya jamii hizi ambazo kwa usiri wao ngazi zao za juu huwa sio salama kwa madhabawu zao za kishetani.
Napenda kumuasa Diamond kama kweli alikuwa alijui hili asiwe muhanga wa ujinga wao bali arudi kuijenga jamii ya mianga na asiwe na ya kinyago cha chapa ya mnyama(Pesa),kwakuwa alikuwa na uwezo wa kuwapiga chapa(Fahamu) watanzania basi na ashirikiane na mema na tusaidiane kuwapiga watanzania chapa ya mema wa uungu wa kristo(777)kwa fikra huru na kuwaweka huru kweli kweli,badala ya kufanya ujinga wa ujinga wa uovu na kuwapiga wanadamu chapa ya mnyama 666 kwa kuteka fikra za wanadamu na kuwa mateka kuwaweka wanadamu kwenye magereza ya fikra za ufahamu wao na kuabudu kinyago cha mnyama yaani pesa,kwakuwa hatuna mda tena kwa kuwa fahamu za uungu zimeingia duniani kuuleta ufalme wa Mungu(888) kuishi na wanadamu hadi ukamilisho wa utukukufu wa ufahamu wake 999 ulioibiwa na uovu na kuubadilisha kwa kuuufanya kinyume chake,yaani miguu juu kichwa chini na kuwa 666 yaaani gereza la ufahamu wa mwadamu iongozwayo kwa uovu badala ya kusudio la uumbaji yaani mema ya ufalme wa uungu wa utukufu had I utukufu na hata ukamilisho wa miisho take 999.
 
Kamanda Siro tumavijana wakahakikishe halafu utoe mrejesho kwa jamii. na kama ni kweli basi sheria ichukue mkondo, na kama ni sanamu kaweka tuambiwe. maana ukiona moshi pana moto waja!!
 
Back
Top Bottom