Fuvu na Mifupa(Skull and Bones) Jamii ya Siri ya Kishetani inayoongoza Matukio ya Duniani

Fuvu na Mifupa(Skull and Bones) Jamii ya Siri ya Kishetani inayoongoza Matukio ya Duniani

Baadhi ya vyanzo vya habari vinasema kwamba Aliens wanakuja kutoka nje ya dunia lakini hiyosiyo kweli.Aliens wapo hapa na hawajawahi kutoka nje ya dunia na hawajawahi kuja kutoka nje ya dunia hata mara moja...

Aliens ni viumbe ambao walitengenezwa mahususi na fallen angels kuwasaidia binadamu katika sayansi ili binadamu awe na uwezo fulani hivi kwasababu maalum....

Aliens wapo kwenye D.U.M.Bs [Deep Underground Military Bases] nyingi zilizoko maeneo mbali mbali duniani ambako kuna majiji makubwa hatari kabisa.robo tatu ya jiji la New York kwa mfano lipo juu ya jiji lingine lililoko chini ya ardhi.Ni watu wachache sana ambao wana access huko lakini majority ya walioko huko ni Aliens na wanafanya mambo mengi sana huko...

Kuna tren inayokwenda kasi kwa speed ya mwanga huko.Kuna majiji makubwa sana kuliko haya yaliyoko huku juu.Kuna silaha za hatari kabisa huko kiasi kwamba huwezi kuamini kama kuna silaha za namna hiyo.Jamaa wana choper ambayo inaweza kuruka umbaliwa mita 3000 hadi 6000 na bado ikaweza kujua ndani ya nyumba yako kuna nani na mko wangapi na wenye jinsia gani na jeshi la Marekani lina chper hizi 60,000 lakini hazijaanza kutumika bado....

Kuna sayansi ya hatari huko acha kabisa na hii inafanywa na Aliens...

Hatuko salama kabisa kama tunavyodhani....
Mmmhhh! Hatari kubwa, sisi binadamu wa kawaida yatupasa tufanye nini ili kuepuka haya? Kimbilio la wengi ni kwa Mungu, ikiwa wao ndo wenye control ya hizi dini tutakuwa na uhakika gani kwamba Mungu huyu ndiye sahihi?
 
Tutazidi kusema secret societies na kufuatilia mengi lakini at the end, tujiulize what's inside? Kwa sababu haiwezekani kikundi cha watu kikaamua kutengeneza taasisi ya kisiri na mafundisho ya siri kama hayo mafundisho are nothing to them. Lazima pia kuna elimu fulani ambayo jamii fulani zimekuwa zikiitafuta na kuificha.

Nasi tuitafute kwanza elimu hiyo. Ndicho kiini na ndicho kinachopaswa sana. Ili mwisho wa safari yetu ya maisha tuwe tumegundua jambo fulani. Kufahamu kuhusiana na chama fulani na mabaya au mazuri haitatosha katika kutupa mwanga wa maisha. Bali pia tufahamu elimu nyingi zilizopo na ambazo tunaweza kuzitumia katika maisha yetu na kujifunza jambo. Siamini kila taasisi ya kisiri ina mabaya ya kujifunza tu katika elimu yake. There must be something.[/QUO lengo la hawa mavmbwana ni kuanzisha kitu kinaitwa new world order dunia iwe chini ya utawala mmoja wa kidini kiserikali na kiuchumi fedha moja (currency) na dini hio moja sio kuwa itakuwa tunasali kanisa moja au msikiti mmoja bali ni siku moja ya ibada ulimwengu mzima ambayo ni sunday (sun - day) siku ya jua ama siku ya Nimrod ambayo waasisi ni wakatoliki chini ya upapa na papa ndiye anakusanya makanisa na misikiti ili wasaini mikataba hio kwa lengo la kisingizio cha uchumi na mabadiliko ya tabia nchi sasa hapa wale wasitaka kutii agizo hilo wataonekana ni wakaidi na wapinga serikali ndio watakaokuwa victims lakini biblia i aeleza wazi wakati huo ndio urakuwa wakati wa Yesu kurudi na kukuta makundi mawili waliokataa ibada ya kweli ya Mungu na walio chini ya ibada ya mnyama 666 ambaye ni shetani kupitia upapa
 
kwa watu wanaoamini dini
Mungu anasema ameumba viumbe wanao onekana na wasio onekana na tusio kuwa na ujuzi nao bali kwa yale aliotufundisha huwenda ni kweli alien wapo ila hatujui kama wana exist kutokana na uhaba wa elimu ya mambo.#Eiyer


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila MUNGU JEHOVA ndiyo mwanzo na mwisho wa kila kitu
hahaha watu wanaishi duniani na kuamua kesho na leo ya watu wengine halafu huo mchakato unafanikiwa ....halafu wewe unasema mungu yehova. ...tujitahidi kukukua kifikira walau hata kidogo basi jamani
 
Mkuu hongera sana umeeelezea kwa maelezo yanayoeleweka na si marefu saaaaaana kwa sisi tunaotumia simu. tunataka jamii forums ya namna hii na si ya kutuletea mambo ya kitoto kama baadhi ya comments za watu wanajifanya wajuaji kumbe mahepe tu. kama we faler mwingine unaona hujatosheka anzisha uzi wako
Hahaha eiyar aliteleza aise ...so alikuwa anataka jamaa apost kitabu kizima hapa ... na amejuaje kama guru hajui habari zozote kuhusu hao Pindar
 
Watashindana lakini hawatashinda,,Mungu atabaki kuwa Mungu na atawafukuza katika uso wa dunia,days ago.......
hahaha watashindwa nini sasa watu wanashinda kila siku mkuu ... je haujawahi kusikia masimulizi ya mabomu ya fat man na little boy yale yaliyopigwa japan kule mjini Nagasaki na Hiroshima ...je yale mamilion ya watu walio kufa hawakuwa viumbe wa mungu " Mbona hatujawahi kumuona mungu akiidhibu marekani baada ya marekani kumuulia watu wake " vipi kuhusu ilivyo leo Iraq syria " na mataifa yote yenye machafuko je mungu haoni kuwa watu wake wana angamia au ndio anasubiri msaada toka kwa binaadamu wamsaidie kufanya suluhisho ..... Mimi napinga hiyo kauli ya kusema watashindana lakini hawato shinda wakati tunaona watu wanapigana na kushinda kila siku ..na mifano ipo mingi tu " ....maana hata martin Luther king ijapo kuwa alikuwa ni mchungaji mkubwa lakini aliuwawa tu Vipi mungu alishindwa kumlinda mtumishi wake !? ...aliuwawa.baada ya kuingilia maslahi ya watu wenye nguvu ..watu ambao huwa wanapambana na kushinda pia ...
 
Mkuu Eiyer naona umewaacha wengi kwenye mataa kuhusu Pindar. Kifupi tu, Pindar ni kiongozi mkuu wa Illuminati hapa duniani. Kiongozi huyu anatoka katika familia 13 ambazo ndio waanzilishi wa Illumianti kwa sasa hivi inasadikika kuwa anatokea kwenye familia ya Rothschild. Pindar ni kifupi cha Pinnacle of the Draco, vile vile ikifahamika kama Penis of the Dragon. Kiongozi huyu ndio nguvu ya juu kabisa hapa duniani anayetawala (control) anayehakikisha kupanuka,na kuratibu mashambulizi ya ki-Illuminati na kutia hofu uma. Hizi familia 13 ni familia zenye nguvu ya kifedha na ushawishi mkubwa kwa serikali zote za dunia hii. Asili ya hizi familia si ya kawaida kwani wana vinasaba (DNA) za nyoka (Reptilian DNA)
Damu ya nyoka mkuu !! Mhh hebu fafanua ili tuelewe mkuu
 
Naona sijaeleweka na baadhi ya watu wamechukulia post yangu negatively kiasi kwamba nimejikuta nashangaa sana tena sana na wengine kama wewe wametaka kujua kuhusu nilichoandika,nitaeleza sababu za mimi kuandika post kama ile ili wale ambao wanahitaji kujifunza wajifunze....

Kwanza kabisa ni kwamba nilitaka kuonesha kuwa mtoa mada hakuwa sawa kwa kusema kuwa Skull and Bones ndiyo wanaoiendesha dunia,pili nikaonesha njia kwa kutaja jina ambalo kabla ya mtu kunirushia shutuma alipaswa akafanye utafiti ajue ni jina la nani nililolitaja lakini kama kawaida yetu Wabongo tumerusha shutuma na matusi....

Kimsingi,kama nilivyofanya mimi ninapenda sana watu wasipende kuambiwa kila kitu bali wakafanye utafiti wao wenyewe wajue maana ukiambiwa sana uwezekano wa kudanganywa ni mkubwa sana,sasa hapa naona mnataka niseme mimi kile ninacho kijua,siyo jambo baya sana lakini tatizo kubwa zaidi ni kwamba hamjui ninachotaka kusema ni kitu gani.Ukweli ni kwamba ni ngumu sana kuelezea nijuacho kwenye post moja au thread nzima hapa JF kwasababu kuu mbili...

1;Wabongo ni wavivu sana wa kusoma makala ndefu hivyo nikipoteza muda kuandika hapa haitakuwa na maana yoyote ile...
2;Mambo ambayo ninapaswa kuyaandika ni mengi sana kiasi kwamba yatakula muda wangu hadi wa kutafuta mkate wa kila siku hivyo kunisababishia nishindwe hata kununua bando la kuingia hapa JF na kuandika haya,sasa hii ni shida kubwa sana....

Ninachowashauri watu ni kwamba wajitahidi sana kujifunza wenyewe kwa muda ambao wanakuwa free,siku hizi ni rahisi maana tunatoa na key word kabisa hivyo unapata pa kuanzia,nilitaja jina Pindar,huyu ni mkuu wa Illuminati asiyeonekana na hata wanachama wa Illuminati wenyewe hawamjui na inasadikiwa mkuu wa chama hiki cha siri anatoka kwenye familia zile mbili kubwa zinazounda Illuminati ambazo ni Rothchild na Rockerfeller lakini hiyo ni speculation tu,ukifuartilia utajua mengi kumhusu na utakapomfuatilioa huyo atakuongoza kuelekea kwingine ambako ni kupana zaidi ya hapo....

Kwa mimi ambaye nina miaka mingi kigogo ninafuatilia mambo haya nikikutana na mtu anayejadili Illuminati,Freemason au Skull and Bones kama wanaoiendesha dunia namuona kama bado hajajua ukweli kabisa maana hivyo vyama vya siri ndivyo ambavyo watu wanakutana navyo mwanzoni tu wanapofuatilia mambo haya na ndivyo vinavyojulikana mitaani sasa.Wakati mimi naanza kuwafuatilia hawa watu Illuminati na Freemason haikuwa ikijulikana kwa watu kabisa na kuna watu walikuwa wananiona ni kichaa,Skull and Bones ndiyo kabisaa hawakuwa wakijulikana,sasa kitu ambacho nilikifuatilia miaka karibia 15 huko nakuja kuona mtu leo anaona ndiyo cha ajabu nashangaa kidogo...

Kuna vyama vya siri ambavyo havijulikani na wengi,vyama kama Theosophical society,Luci's trust [Lucifer's trust],Rosicrusian [Rose and cross],Club of Rome na vingine vingi ni miongoni mwa vyama vya siri ambavyo viliundwa kwa umakini ili yoyote anayefuatilia ajikute anaamini kuwa hao ndiyo kila kitu na aishie hapo kama mtoa mada wakati kuna mengi zaidi...

Bahati mbaya ukiishia hapo hutawajua watu kama Aliester Crowell,John Dee na kiboko yao Mainly P. Hall na bila kumsahau Hellena Petrova Blavasky au mwanafunzi wake waliyeshirikiana naye kuunda Luci's Trust,Alice Baily.Hellena Blavasky anamahusiano ya kindugu na mke wa Prescot Bush babu wa George W. Bush ambaye ni mtoto wa George H Bush ambaye ni mtoto wa Prescot Bush...

Unapoanza kujadili masuala ya vyama vya siri unakuwa bado kabisa na nakuona kama upo shule ya msingi ya kuelekea kuwajua wanaoiendesha dunia kwasababu huko baado sana ni mbali.Ukifikia kuwajua Nephilims na bara la Atlantis ambalo halipo leo na walipotoka sasa hapo utakuwa upo secondary ukielekea kuwajua akina akina Sananda ni akina nani au Sanat Kumara hapo sasa unakuwa umefika secondary A-Level ukielekea chuo ambako utakutana na wanaoiendesha dunia....

Jitahidini kufuatilia majina niliyoandika ili muweze kujua mengi na siyo kutaka kuambiwa kila kitu.Hapa tu nimewapa hints na mnaona maandiko yamekuwa mengi.Kutaka kuwaelezea tu akina Mainly P. Hall si itakuwa shida?

Niwatake radhi kwa niliowakwaza lakini wito wangu ni kwamba tujitahidi sana kujifunza na kuacha kutukana watu bila sababu za msingi....
Heshima kwako, huyu Manly P.Hall nina kitabu kinaitwa Secret of teaching of all Ages ,si mchezo kaandika yeye

MTC | 101| [emoji769]
 
Nimrodi ni mjukuu wa Ham mtoto wa Nuhu.Alikuwa ni mtuhodari sana na muwindaji mahiri sana.Vyanzo vingine vinaeleza kwamba,kwasababu ya watu kuanza kuenea baada ya gharika na wanyama kuazaliana kuliibuka kitisho kwa binadamu wa eneo la Babeli la kudhuriwa na wanyama wakati na Nimrod alikuwa akipambana na wanyama vilivyo na kuwa mtu muhimu sana katika jamii iliyomzunguka...

Alianza kua mtawala wa Babel hadi Ninawi na maeneo mengine ya jirani.Alimuoa Semiramis ambaye vyanzo vingine vinasema kwamba alikuwa ni mama yake.Alianzisha dini ya kuabudu sayari ambayo ilikuwa maarufu sana maeneo mengi ya dunia baadaye.Imani hii aliipata baada ya kuwasiliana na viumbe wa roho ambao ni wale malaika walioasi.Dini hii ilikuwa maarufu sana katika Babeli....

Baada ya watu kuwa wengi aliamua kujenga mnara ambao kama itatokea tena gharika basi watu wasife.Alijenga mnara mkubwa sana ambao ulikuwa ni mnara mrefu zaidi duniani kwa wakati ule.Pia hakutaka watu wasambae duniani kote bali wabaki pale pale ili kujenga jamii moja na yenye nguvu ikiwa na dini moja.Maelekezo yote haya aliyapata kutoka kwa malaika waasi ambao alikuwa akiwasiliana nao kwa njia mbali mbali kama vile maono na ndoto....

Dhana hii ya kuunda jamii moja yenye nguvu inayozungumza lugha moja na yenye dini moja ndiyo ipo hadi leo na ndiyo maana hata jengo la umoja wa ulaya limejenga likionekana halijamaliziwa wakimaanisha kudhamiria kukamilisha alichoshindwa kukikamilisha Nimrod.Pia,kitendo kilichotokea sept 11 kule Marekani ni ishara ya kuondoa mamlaka mbili zilizokuwa zikishindana na kubakisha moja ya shetani na ndiyo maana likajengwa jengo moja tu na likaitwa One World Trade center...

Turudi kwa Nimrod..
Babu yake ambaye ni Ham hakufurahishwa na imani hii,aliamua kumuua mwanae huyu na kumkatakata vipande vipande na kuvisambaza katika maeneo yote aliyokuwa akitawala Nimrod na kutoa agizo kuwa yoyote atakayeendelea kufanya ibada alizokuwa anazifanya Nimrod basi atafanywa kama kiongozi wao alivyofanywa...

Suala hili liliwafanya wakazi wa Babel wakaogopa lakini kwa muda tu.Mkewe Nimrod ambaye ni Semiramis alikusanya vipande vya mwili wa mumewe na kuvizika lakini kiungo cha uzazi cha Nimrod hakikupatikana na Semiramis akasema kuwa Nimrod amepaa kwenda kuishi juu na alama yake ni jua [Sun] na tangia hapo alama ya Jua ikawa ni alama ya Nimrod na akaanza kuabudiwa kama mungu na ndipo ibada ya kuabudu jua ilivyoanza na ikaonekana kuwa kiungo cha uzazi ni kitakatifu hivyo wakakitengenezea alama ya kukiheshimu kama alama ya imani yao na ndipo ilipotengenezwa Obelsk..

Obelisk hizi zipo maeneo mengi sana duniani kama vile St. Peter's square kule Vatican,Washingnton DC,Paris,Ufaransa na maeneo mengi kuonesha ni imani gani waliyonayo...

Baada ya miaka kupita Semiramis alipata ujauzito kwa namna ambayo hadi leo haijulikani lakini yeye akasema kwamba alikuwa amekwenda kumtembelea Nimrod mawinguni na akampatia ujauzito kwa njia ya ajabu hivyo hata atakachokizaa kitakuwa ni kitakatifu.Baada ya muda alimzaa mwana aliyejulikana kama Tamuz....

Tamuz,kama alivyokuwa "baba yake" naye alikuwa muwindaji mahiri sana lakini alikuja kuuawa na nguruwe pori siku ya ijumaa na waumini wa dini ile wakaamua kila ikifika ijumaa hiyo kwenye mwaka walikuwa hawali nyama kabisa kuenzi kifo cha Tamuz.Tamuz alichukuliwa kama |mwana wa mungu" [son of god] kwasababu ya maelezo ya mama yake ambaye alisema kuwa alikwenda mawinguni na kupewa ujauzito na Nimrod hivyo naye wakawa wanamuabudu...

Semiramis alikuja kufa na waumini wake waliamini naye kama ilivyokuwa Nimrod alikuwa ameenda kuishi na mumewe mawinguni na kuanzia hapo alama yake ikawa ni mwezi,mwezi ukawa kama mke na jua likawa kama mume kwakuwa lilikuwa linawakilisha watu hao muhimu mawili katika imani ya Babeli na ndipo ilipozaliwa ibada ya kuabudu vitu hivyo na kuviweka kwenye majumba ya ibada.....

Walitengeneza utatu wao ambao ulikuwa ni wa Nimrod,Semiramis na Tamuz,semiramis akajulikana kama malkia wa mbingu [queen of heaven]

Baadaye ilipoanguka mamlaka ya Babeli imani hiyo ilisambaa duniani kote na watu hao watatu walikuwa wakiabudiwa kwa majina tofauti tofauti.Mfano kule Misri waliitwa Isis [Semiramis] Osiris [Nimrod] Horus [Tamuz]....

Ni hayo kwa ufupi sana mkuu...
Aisee leo nimejua maana ya Isis
 
mimi naona kama kuna Ibada inayoweza kumpa mtu utajiri, haiba,kukubalika na jamii, power na mali halafu usidhuruke mwili wala kudhuru wengine inafaa. Bora tu hao kwa sababu kila binadamu anataka afya, utajiri, madaraka , mali, haiba na kukubalika. Maisha ni hapa hapa duniani kwingine ni imani tuu.
Nakubaliana nawewe
 
Duniani hakuna kazi rahisi kama kupinga,lakini kusema sababu ya kupinga kwa kujenga hoja ni kazi ngumu sana,Tangu umekuwepo hapa wewe unakansha tu....

Yaani wewe umechagua tu kusema hakuna hiki wala kile bila kujenga hoja....

Kwanini hakuna?

Unaweza kukanusha wewe siyo binadamu lakini kusema ni kwanini wewe siyo binadamu ndipo penye shida...
hahaha
 
Suala au dhana ya kwamba wana wa Mungu ni watoto wa Seth ni assumption ambayo haina back up ya Biblia hata sehemu moja.Dhana hii naifahamu sana na kuna watu wengi wanadhaniahivyo lakini ukweli ni kinyume kabisa kwasababu zifuatazi...

1;Hakuna mahali Mungu aliwakataza wana wa Seth kuoana na wana wa Kaini
2;Hakuna anayeweza kueleza ni kwanini baada ya kuingiliana kwa wana wa Seth na Kaini kingono kukasababisha kuzaliwa viumbe wa ajabu kuliko binadamu
kwasababu Seth na Kaini wote walikuwa ni binadamu wa kawaida kabisa

Kwa upande wangu mimi madai yangu kuwa wana wa MUNGU ni malaika yana back up ya maandiko...

Ayubu 1:6
6 Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao
.

Hao hapo malaika wanaitwa wana wa Mungu.Dhana ya Seth na uzao wake kuwa ni wana wa Mungu ni ya kutunga tu....

Hakuna mahali ambapo biblia inasema kuwa malaika hawana jinsia,andiko uliloleta linasema "hakuna kuoa wala kuolewa kama malaika",kusema hakuna kuoa na kuolewa haimaanishi huna jinsia.Kwa upande mwingine inathibitisha kuwa wana jinsia maana kama wasingekuwa na jinsia wasingetaja kuu ya kutokuwepo kuoa na kuolewa.Mapadri hawaoi,je hawana jinsia kwasababu wamekatazwa kuoa na kuolewa?

Umenifanya nimecheka sana kwa maelezo yako haya.Unatakiwa ujifunze sana juu ya historia ya dunia hii,hapa sizungumzii hiztoria uliyosoma shuleni,nenda zaidi ya hapo...

Usichojua ni kwamba wakazi wa hilo eneo unaloliita wewe kuwa ni mashariki ya kati halikuwa na watu weupe bali weusi na halikuwahi kuitwa "mashariki ya kati" bali lilikuwa linaitwa "North east Africa".Weupe unaowaona eneo hilo walitokea Ulaya na Uturuki na hawakuwa wakazi wa eneo hilo tangu mwanzo na walipofika huko walikuwa wakiwaua sana watu weusi ambao ndiyo walikuwa wakazi halisi wa eneo hili.Historia ya eneo hilo inafanana na ya Misri.Misri haikuwa ya watu weupe bali hao ni watu wa kuja tu..

Kwanza ni kweli kabisa kuwa Hamu alitenda kosa ulilolisema hapo juu na alipewa laana na hao ni wana wake.Sasa jibu hoja zifuatazo...

1;Hao ambao umesoma historia unayoikubali wanakataa kuwa Misri haikuwahi kukaliwa na watu weusi,kama huyo mtoto wa Hamu ambaye ni Misri hakuwa mweusi? Kama alikuwa mweusi inakuwaje hao walioandaa hiyo historia yako wakataa jambo hilo?

2; Kama Misri ilikuwa na watu weusi kama unavyosema halafu Yesu alikuwa mtu mweupe kama unavyodai,inawezekanaje Yesu aje kujificha Misri wakati ule alipokuwa akitafutwa na Herode auwawe wakati akiwa mtoto mchanga ambapo alikimbilia huku yeye na wazazi wake?Inawezekanaje mtu mweupe aje kujificha katikati ya watu weusi na asifahamike?

3; Kama Misri ilikuwa na watu weusi kama ambavyo unadai,iweje mtoto Musa ambaye alikuwa mweupe kwa mtazamo wako aende akalelewe kwenye nyumba ya Farao na asijulikane kuwa ni Muisraeli?

4; Kama Misri ilikuwa inakaliwa na watu weusi ni kwanini ndugu zake Yusuph walishindwa kumtambua ndugu yao walipokwenda Misri kutafuta chakula wakati kwa unavyodai wewe walikuwa ni weupe? Yaani inakuwaje washindwe kumtambua mtu mweupe katikati ya weusi?

5;Kama unakataa kuwa Wamisri wa kale walikuwa siyo weusi maswali yote hapo yanajifia,lakini linazaliwa swali lingine kubwa zaidi ambalo linasambaratisha hoja yako yote ya laana na dhana ya kuwa watoto Hamu walikuwa ni weusi kwasababu kama utasema kuwa Misri hakuwa mweusi ni kwanini udai wengine ni weusi?

6; Kama unadai watoto wa Hamu walikuwa ni weusi,vipi kuhusu mtoto wa Hamu anayeitwa Kanaani ambaye ni baba wa Wakanaani?Waisraeli walipokuwa wanarudi nchi hiyo ya ahadi ambayo ilikuwa inakaliwa na watoto wa Hamu ambao ni Kanaani,walipambana nao,je walikuwa weusi kama watoto wengine wa Hamu? Kama walikuwa weusi ni kwanini unadai watu wa mashariki ya kati walikuwa weupe wakati hao walikuwa weusi? Kama hawakuwa weusi ni kwanini watoto wengine wa Hamu wawe weusi na wengine wasiwe weusi?

Mkuu maswali ni mengi sana na sidhani kama utaweza kuyajibu yote lakini ninachotaka kukueleza tu ni kwamba dhana ya watu weusi kuwa ndiyo watoto wa hamu tu inajifia yenyewe ukiangalia hoja zote nilizokuuliza na nyingine nyiingi sana ambazo sijakuuliza....

Na hoja hizo zinasambaratisha hizo hoja zako zoote ulizoandika hapo juu...

Hoja ya umaskini wa Africa ina majibu yake mengine lakini siyo hiyo dhana yako ambayo ililetwa na hawa hawa weupe ambao wamekufanya na wewe kudhani kuwa Yesu alikuwa mweupe....

Acha nikuchape na haya maneno ya Suleiman hapa kwanza...

Songs of songs 1:5
5 I am black, but comely, O ye daughters of Jerusalem, as the tents of Kedar, as the curtains of Solomon.


Nikutakie tafakari njema....
hahaha tukiwaambiaga hivi huwa wanapinga
 
1. Mnasema watu weusi ndo viumbe halisi wa Mungu.
2. Watu wenye ngozi nyeupe ni wanefili na wamefanya jitihada nyingi kumaliza watu weusi na "soon lengo lao litatimia".
3. Kama viumbe weusi ndo watu wa Mungu na watamalizwa soon na hao "immortals" ina maana watamshinda Mungu huyu aliyeumba dunia na hao watu weusi?!!

Sasa Mungu anashindwaje wakati tunaambiwa nguvu zake hazina ukomo na ni kubwa sana? Je, hao immortals hawafanyi kazi kwa niaba ya Mungu ambaye naye ni immortal? Inakuwaje Mungu aumbe viumbe dhaifu kama sisi halafu aache viumbe vyenye nguvu kuliko alivyoumba yeye vinyasenyase viumbe vyake?

Imesemwa huku kuwa jamii hizi za siri ndo huweka wakuu wa nchi madarakani kwa makusudi yao. Kwenye kitabu cha Daniel tunaambiwa Mungu ndiye huweka falme na mamlaka za dunia kwa wakati wake kwa makusudi yake. Mungu pia ndiye "ultimate controller" wa kila kinachochotokea hapa duniani kwa hiyo shetani hafanyi uharibifu unaozidi kiasi Mungu alichomruhusu. Tunaona mfano wa hilo kwenye kisa cha Ayubu - kwamba amvuruge anavyotaka ila asiguse roho yake.

Kwa jinsi ninavyomuogopa Mungu swali kubwa nililotaka kuuliza limefanya moyo uende mbio. Niishie tu hapa.
Hahaa Mungu ana contractions kibao .....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hahaha watashindwa nini sasa watu wanashinda kila siku mkuu ... je haujawahi kusikia masimulizi ya mabomu ya fat man na little boy yale yaliyopigwa japan kule mjini Nagasaki na Hiroshima ...je yale mamilion ya watu walio kufa hawakuwa viumbe wa mungu " Mbona hatujawahi kumuona mungu akiidhibu marekani baada ya marekani kumuulia watu wake " vipi kuhusu ilivyo leo Iraq syria " na mataifa yote yenye machafuko je mungu haoni kuwa watu wake wana angamia au ndio anasubiri msaada toka kwa binaadamu wamsaidie kufanya suluhisho ..... Mimi napinga hiyo kauli ya kusema watashindana lakini hawato shinda wakati tunaona watu wanapigana na kushinda kila siku ..na mifano ipo mingi tu " ....maana hata martin Luther king ijapo kuwa alikuwa ni mchungaji mkubwa lakini aliuwawa tu Vipi mungu alishindwa kumlinda mtumishi wake !? ...aliuwawa.baada ya kuingilia maslahi ya watu wenye nguvu ..watu ambao huwa wanapambana na kushinda pia ...
Vita vyetu si vya damu na nyama ,wala hatutawaogopa wanaoua mwili ili_hali hawawezi kuua roho Mungu atabaki kuwa Mungu milele na milele Amen,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hahaha watu wanaishi duniani na kuamua kesho na leo ya watu wengine halafu huo mchakato unafanikiwa ....halafu wewe unasema mungu yehova. ...tujitahidi kukukua kifikira walau hata kidogo basi jamani
...ahahahaaaa watu hawajui hata hizo hadithi za huyo Mungu ndio wao wamezi_frem na kuwakaririsha ...sad

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naam!! Kundi hilo ni ishara tosha kwamba shetani amefanikiwa mno katika 'mission' yake.Genge la namna hii ni mazezeta/mazuzu peke yao ndio wanakua wanachama ingawa wao wanajiona wana akili sana.Shambulizi baya na la hatari analofanya shetani kwa mwanadamu ni kukorokochoa 'mind set'.Akifaulu eneo hili,hata uprofesa hauna kazi maana hapo usiku na mchana huwa sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom