Gachagua amepoteza stahiki za N/Rais Mstaafu (kwa kufukuzwa kazi na Senate)

and 300

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2012
Posts
26,398
Reaction score
36,406
Baada ya kufukuzwa kazi Naibu Rais Mstaafu wa Kenya Rigathi Gachagua anapoteza stahiki zifuatazo ambazo alizistahili endapo angejiuzulu.

1. Pensheni ya kila mwezi Ksh. 720,000.
2. Malipo ya mkupuo Ksh 8.2m.
3. Posho ya mafuta Ksh. 108,0000(?).
4. Gari 2 (saloon cars).
5. Gari 4WD (1).
6. Msaidizi wa ofisi (PA).
7. Mlinzi mwenye silaha.
8. Madereva watatu.
9. Mhasibu (1).
10. Wafanyakazi wa ndani (2).
11. Wafanyakazi wasaidizi (support staff).
12. Wafanya usafi (2).
 
Huu ni uchafu kwa Gachagua...

Huyu amepoteza...status za unaibu rais pekee.

Pesa anayo ndefu sanaa
 
Gachagua Is filthy rich, ana mahela sana hizo pesa Wala sio chochote kwake


Ila kwa upande mwingine, waafrica akili zetu sijui ziko wapi, mtu anastaafu analipiwa mpaka mafuta na kubadilishiwa magari, yaani uongozi unakua kama ufalme, ila sisi Wanatuambia penshen zetu watatupa kwa awamu, wameleta kikokotoo kwamba tukipewa kwa pamoja tutazichezea😃😃
 
Mwenyezi mungu atatulipia wala tusichoke kumuomba .........waache waishi na kutumia watakavyo ila mwisho upo.........kire ambacho kinaumiza ni kuona wanavyojitoa ufahamu kwamba watu wasipate stahiki zao eti watatumia vibaya ilihali wao wanatapanya mali hovyo hovyo
 
jamaa ameonekana anadunda kitaa na wanabodaboda...huku anampagia ruto mikakati
 
Tanzania hakuna wa kukufukuza, waanaandika barua ya kujiuzuru kwa niaba yako halafu stahiki zote unaenda nazo.
Hata ukifukuzwa bado stahiki utaenda nazo hadi kaburini, hata kaburi litapewa ulinzi.
 
Wanasiasa ni wabinafsi sana,wanajipakulia minyama tu
 
Tanzania hakuna wa kukufukuza, waanaandika barua ya kujiuzuru kwa niaba yako halafu stahiki zote unaenda nazi.
Hata ukifukuzwa bado stahiki utaenda nazo hadi kaburini, hata kaburi litapewa ulinzi.
Huruma nzuri. Kwa nini watu wafukuzane kama wanyama!? Tanzania watu wake wanahekima.👍🏼
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…