Gadner Habash anapokula pesa za watu wa Jide


Pole sana, ntajaribu kuongea na DJ choka nimfikishie malalamiko yenu, nadhan ujumbe utafika, ila Mimi kwa experience ndogo ya Ku shoot video za wanamuzik, Mara nyingi video queens ndo at least wanalipwa the rest nadhan wanakuwaga mashabik ambao wanashoot for free, other wise kama aliwa promise kuwalipa...
 

Umesahau kuandika jina lako ili malipo yawe officially.
 
Mpo sahihi kabisa kulalamika, dhuluma sio ishu wala nini....watu walipwe ujira wao

Ni juzi juzi tu mlijikusanya humu jamvini kumtetea alipolalamika eti anadhulumiwa na Ruge, leo mnataka kuunga mkono dhuluma yake......mkuki kwa nguruwe...acheni unafiki wabongo..shame on you.

Na hizi kauli za "kitanzania" kukebehiana..kuona wengine ni wakata viuno...kwa lipi la maana unalofanya wewe kuona wengine hawana la kufanya na wanakata viuno...as long as wewe ni m bongo basi hakuna cha maana unachofanya ni sawa tu na anayekata kiuno.

Au kuosha choo cha ndege au ku repair computer na simu zilizotengenezwa na wazungu ndio shughuli bora kuliko kukata viuno ?....huko nako kwa tafsiri yao wazungu ni kukata tu viuno ila kwa mazingira tofauti...na mtasubiri ku repair daima milele.
 
mafanikio ya jide ndio ya gadna sasa iweje gadna apige hiyo pesa...?labda mtuambie kwamba ni promo....
 
u waka
Yaani sijui nikushukuru vipi ndugu yangu,ulichosema ndo icho .kuna watu humu ndani Jide wanamchukulia kama mungu wao mdogo hakosei wala nini,na ukimgusa tu ama zao ama zako.....eti kukata kiuno tangu lini jide alifanya nyimbo watu wakakata viuno?je nyimbo zake za vile ni za kukata mauno? this is sad News!...nakushukiuru mdau,wenye moyo huo ni wachache wanaoona ukweli na kuusema wazi bila kujali ninini irimradi ni ukweli,kujifanya kumpenda mtu hata akikosea kwako ni sawa ni UTUMWA ZAIDI YA UKOLONI!
 

ULICHOSEMA NI KWELI unajua ingekuwa free sidhani kama kungekuwa na haja ya kulalama,ila kulikuwa na mapatano tena kwa kusema hata izo nguo kama suti na mashati meupe tulijigharamia kwa mapatano kwamba hata kama mtu ni nguo zako ama ulikodi basi yatalipwa pamoja na huo muda...usiku kwa usiku,,na wengi wetu tuliingia hata gharama za tax kurudi nyumbani mana gari la jide liliishia nyumbani lounge,kwani hata gari la jide hulala pale nyumbani lounge dereva wake anaitwa SAID....POA TU DUNIA INA MAJARIBU NDO HAYA!
 
eh...nikiasi gani mnadai...?

Jumlisha kukodi vazi la suti,tax,na kuzungushwa kwa siku mbili tena usiku,na ni kwa masaa 8.uliza kama unamkodi mtu hata ulaya ipo ila hutegemea na nchi na mapatano....
 
Duh, wataje fast jide awarushie mpesa

labda alipe mwenyewe mana akimpa Gadner anakula sasa sijui anashindwa kumcontroo ama ni nini?
Mana sipati picha pesa iwe ya malipo na wewe hapo hapo,au halipwi?kwamba mama ndo anajua pesa niitoe vipi?mana unaweza mlaumu Gadner kumbe nae ana ukata,ndo mana tumesikia majuzi kama alipata kazi nchini kenya ya utangazaji Jide akakataa,sasa kwa miradi ile ukaanze kusaka ajira sehemu nyinine,,,huenda mama anabana.MANA mpaka pale ile ni ajira tosha kushinda hata ile ya kutangaza.
 
Ila mlitokelezea...hakuna sura ya dhiki kwenye hiyo video, mi nilijua wote wa kishua tu, ndo unaanza kunifumbua macho mkuu..kazi nzuri sana mmefanya full white plus na ile range nyeupe ya jide ndo kabisaa mmeuaa
 

Warumi umekunywa maji ya JIDE NA DAMU yaani eti twende POLICE hii ni zaidi ya POLICe..Tumchafue kwa lipi?
we si unampenda tafuta huu ukweli hata kwa kuulizia pale Times Fm KAMA KULIKUWA HAMNA KITU KAMA ICHO,UNADHNI MUMEWE angetupa haki zzzzzzzzzetu YANGEBUMBULUKA?WARUMI vipi dada angu ama ninini tatizo Hii ndo kazi ya Jf!
 
inakuaje udai kitu kisichokuwa na mkataba,ni muda wa watu kuelewa haki ikoje,siku nyingine unaweza kufungwa ukasema umeonewa.
 

Kwa hiyo nimeshakuwa Dada tena? Kweli jide kakuvuruga, pole sana mkuu....
 
kwan we ulikodisha nguo sh ngap?
mbezi makabe ulirudije??
halafu kwenye iyo video umevaaje ili niweze kukutambua???
 
Ila mlitokelezea...hakuna sura ya dhiki kwenye hiyo video, mi nilijua wote wa kishua tu, ndo unaanza kunifu hatambua macho mkuu..kazi nzuri sana mmefanya full white plus na ile range nyeupe ya jide ndo kabisaaa

Unajua hapa siongelei njaa,kiukweli hakuna mwenye dhiki kama mnavyota kuaminisha watu,tuna kazi zetu maisha yetu na
tunasomesha,hapa ni haki kama tulivyopatana.....ivi mwenye dhiki ya ivyo anajua kumiliki hata mambo ya laptop?
Acha izo kuwa na fikra positive kidogo....na ungejua unaongea na nani..anyway ngoja nikupoteze mana nimeshajua tatizo..!unadhani ye alituchukua tu barabarani...nilichohukia ni kwenda kinyume na makubaliano hata angesema bure tungekubaliana kwanza sisi ni wat wazima we unadhani mara nyingi ugonvi unaanzaga na vitu vikubwa?unaweza shangaa hata mia tu ikaanzisha ugonvi,why?sababu mapatano yamevunjwa!....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…