GALLERY: What are some rare pictures that you have never seen? Here are some of them...

. Soldiers add height to the Berlin Wall shortly after its construction in 1961



. The Berlin wall was heavily guarded

Huu ukuta ulikua na urefu wa 55Km yan 55Km long na 4m tall, kwasababu kuta zilikua 2, zilitenganishwa na corridor katikati ambayo waliipa jina la 'death strip'. Hakuruhusiwa mtu kupita hapa.

👇👇Hapa walinzi wakiwarudsha watu wasipite mpakan, ilikua April 1961


. Despite its notoriety, the wall was relatively small in height. In most places, it was only about 11 feet tall, so people could clearly see buildings on the other side, as this 1981 picture of the Kreuzberg district shows.

Hapo ilikua 1981,mtoto akichezea mpira karibu na ukuta.

. The wall famously ran in front of Brandenburg Gate, a symbol of post-unification Germany. The gate was actually part of a city wall constructed in the 1700s.

Here is Brandenburg gate in 1961. By that time, the gate was symbol of peace and unity.
Here below is how now the gate looks like


Today, a busy avenue runs where the wall once stood, and buildings populate the once-barren "death strip."



. Berlin wall running through potsdamer platz in 1962

Na hapa chini ni jinsi huu mji wa Potsdamer unavyoonekana in 2014
 
. Dr June Almeida: Mwanamke aliyegundua Corona virus kwa mara ya kwanza.

Mama huyu ni mtu wa scotland, aligundua virusi vya corona mwaka 1964 alipokua maabara ndani ya hospitali ya St thomas mjini London.
Akiwa na miaka 16, aliacha kusoma baada ya kupata kazi kama 'histopathology laboratory technician' (Histopathy is the study and diagnosis of tissue diseases and involves examining cells and tissue under a microscope, according to the Royal College of Pathologists) ila baadaye aliamua kwenda London kujiendeleza kielimu.

Muonekano wa Corona virus kupitia microscope ulikua hiv kwa mara ya kwanza 1964..👇👇👇



Alihama England na kuelekea canada kwa kazi zake. Baadaye alirudi tena England palepale St Thoman hospital ambapo kama unakumbuka hii ndiyo hospitali iliyotumika kumuuguza Boris Johnson waziri mkuu wa uingereza wakati kapata maambukizi ya Covid-19.
Katikati ya miaka ya 80 akiwa hapo London, alisaidia kupata picha za HIV.

Dr June almeida alifariki mwaka 2007 kwa heart attack (london hapo hapo) akiwa na miaka 77. Alizaliwa october 5 1930.
 
pamoja kiongozi
 
Igor Sirkosky, The Man with the Impossible Dream of Helicopter.



Basi mwaka 1889 may 25 mjini Kiev, Ukraine, alizaliwa Igor Ivanovich Sikorsky. Akiwa kijana mwamba huyu ikichangiwa na mama yake ambaye alikua ni medical school graduate kipichi hicho pamoja na baba yake ambaye ni daktari na Professor katika maswala ya saikolojia, alipendelea kusoma ishu za science na hasa mambo ya usafiri wa anga yani Aviation.

Alipokua na miaka 14, katika mji wa Carolina (North) alikuatana na Wilbur na Orville Wright ambao walikua wakijaribu kutengeneza vifaa vya urukaji. Siku hiyo ndipo Igor alipoamua career ya maisha yake. Aliishi St Petersburg( kabla mji haujajitenga kama saiv) miaka 3 ndani ya Naval college ( jeshi la majini) wakati huohuo akiwa mwanafunzi pale Mechanical Engineering College of the Polytechnic Institute mjini Kiev.

Igor alisafiri kwenda Paris kusoma uinjinia ambapo alikutana na wataalamu wa mambo ya anga kama Louis Bleriot,na badaye alirudi nyumbani na kuanza majaribio ya kutengeneza Helicopter yake ya kwanza.

Hivyo alitengeneza Helicopter ya kwanza 1909, ya pili akatengeneza 1910 ambapo sasa pamoja na kuwepo 15-horse power, ya kwanza haikuruka na ya pili iliruka tena aliiendesha yeye na ni umbali mfupi, na pia ya kwanza ilishindwa ku-sustain ile weight ya rubani ndy mana ikashindwa.

Hapo juu kwenye picha ni Igor S akiwa na helicopter yake ya pili aliyotengeneza mwaka 1910.

1913 alitengeneza nyingine ambayo ni 50 horsepower engine na alibaki hewani zaidi ya lisaa kwa altitude ya 450m, na alifanya safari fupi ndani ya nchi hiyo.

Hii ni picha ya mwaka 1913 na alipigwa wakati akiwa amesimama mbele ya model yake mpya ya aircraft ila picha ya jumla haikuonekana vizuri.

Na hii ilioelekea kupata leseni na pia tuzo kwa kazi yake👇👇👇👇

Basi March 30 1919, mwamba alihamia Newyork marekani. Kuhama kwake Russia kulitokana na mapinduzi yaliyokuwepo kule (tulisoma sekondori kuhusu Russia Revolution) ambapo kila officer au injinia au tuseme msomi walitaka kumkamata na kumuua hivyo yy hakutaka hilo.

Akiwa US kama mwalimu wa hesabu au lecturer7, alitafuta eneo atakapofungua kiwanda chake na rafiki yake alimpa shamba na kiwanda hiko aliita Sikorsky Aero Engineering Corp,hali ya uchumi ilikua ngumu ndipo rafiki yake mwingine Sergei Rachmaninoff aliwekeza $50000 ili ishu zikae sawa. 1924 alitengeneza aircraft ya kwanza na iliruka, baadaye 1928 akawa citizen wa US, alitengeneza pia aircraft zingn baadaye kama fyling boats zilizopita Atlantic na Pasicif oceans (1929-1937).
Yan hizi hapa chini 👇👇👇


Story ni ndefu, ila rasmi kuanzia 1938 alianza kutengeneza helicopter (practical one), na akiwa kama Engineering Manager wa Vought-Sikorsky Division of United Aircraft Corporation, aliweza shawishi viongozi wa US kuhusu mpango wake.

Hatimaye september 14 1939, alimaliza mission yake na chuma alichotengeneza kilifanikiwa kama alivyotarajia. Helicopter hii aliipa jina la VS-300 (V-Vogous, S-Sirkorsky) na picha hii hapa chini inaonyesha first flight ya hiyo helicopter, mwaka 1939 september 14.

Hapa chini pia ilikua ni public demostration flight, mwaka huohuo 1939.


Hapa akitest mambo👇👇👇





VS-300 ikiwa hewani 👇👇👇


Naam,👇👇


Improvements👇👇👇





👇👇 Huyu ndiyo yule jamaa ake walikutana Paris alipoenda kujiendeleza kielem kuhusu uinjia


Dah Wakuu ninaeza andika mengi sana kuhusu jinsi alivyotengeneza Helicopter na picha zake pia kuweko ila tuishie hapa.

NB: Huyu siyo wa kwanza kutengeneza chombo hicho ila yeye alikua wa tofauti kuliko wengine na ndiyo Helicopter zote zimetengenezwa kupitia innovation yake. Wako wengine walijaribu ila walishindwa.

Baadhi yao ni hawa hapa👇👇👇
1.

Huyu mwamba anaitwa Paul Cornu na hapa ilikua mwaka 1907 kwenye helicopter yake ya kwanza, Ukimwangalia ni amekaa kati ya rotors mbili ambapo zilizunguka uelekeo tofauti yan in opposite direction ili ku-cancel torque. Hii ilikua ni helicopter ya kwanza kunyanyuka kwa kutumia rotor blades badala ya wings



2.
Huyu anaitwa Louis Breguet alitengeneza yake pia mwaka 1907 na ni full scale na pia pilot aliweza kuitumia ila sasa haikua na uwezo wa kua controlled yani namaanisha haikua na 'means of controll'.



3.
Huyu ni Emile Berliner wa ujerumani mwaka 1908


4.
Huyu ni J.C.H Ellehammer mwaka 1912 pale Dernmak na haikuruka zaidi ya 1ft.


Na wengineo wengi!

Basi kila safari ina mwanzo na mwisho wake.
26 Oct 1972 (aged 83)Easton, Fairfield County, Connecticut, USA ndipo alifariki.
 
Nmekaaa nkafikir nkifa ntakumbukwa kwa lini.............Naihurumia nafsi yangu kwa wazungu wajukuu zake watakuwa wanakula bata tu kwa innovation ya babu yao mana hawa jamaa wanawekaga haki miliki mtonyo unaingia tu....Labda utengeneze helkopta panga uliweke ndani[emoji3][emoji3] kama ni juu basi mtonyo unaingia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila mmoja ni potential sema hua hatujijui. Changamoto ipo hapo!
 
Maafisa wa ngazi za jeshini wa umoja kiSoviet wakitazama mabaki ya Vladimir Komarov ambaye alianguka tokea angani April 24 mwaka 1967.


Vladmir Komarov alikua ni mmoja wa watu wenye ujuzi katika kurusha vyombo angani yaani spaceflight, na alizaliwa 16 march 1927 nchini Russia.

Mazingira ya kifo chake yaliyotokea kipindi umoja ule wa kiSoviet umepanga kusherekea miaka 50 tangu msingi wake na serikali ya kipindi kile chini ya Leonid Brezhnev, walipanga kusherekea kwa namna ya pekee.
Ni ipi? Ni kupitia kutengeneza space vehicles 2 (Space Capsule) ambazo baada ya kufika angani, yani kwenye outer space, zitaenda mwendo sambamba yani Orbital docking na kisha aliyeko ndani ya chombo kimoja atahama na kuhamia chombo kingine, wakiwa angani wote mda huo.

Space vehicle ya kwanza iliitwa Soyuz 1 ambayo ndiyo Vladimir aliondoka nayo kwa siku ya kwanza na ya pili iliitwa Soyuz 2 ambayo ndiyo ingeondoka siku ya pili yake ikiwa na watu wawili ambapo sasa zitakutana na zitaenda sambamba yani orbital docking halafu Vladimir atahama kupitia kutambaa yani crawling kutoka aliko na ataenda kwenye hicho chombo kingine Soyuz 2 halafu ndicho atakachorudi nacho duniani.

Sasa Vladimir alichaguliwa huku mbadala wake akiwa ni Yuri Gagarin ambaye wamekua wote tangu udogoni na walifanya mambo mengi pamoja kama uwindaji n.k

Yuri G ni huyo wa upande wa kushoto.

Sasa kila mmoja aliyehusika kutengeneza kile chombo walijua hakiko salama kwaajili ya hiyo safari na huenda kifo kikawepo. Sasa Komarov hakutaka rafiki yake aende na hicho chombo kwani alijua fika kua hatorudi akiwa hai na lazima atakufa. Hivyo ndivyo alivyoamua.

Kadri siku zilivyokua zinasogea, wataalam walibaini matatizo ya kiufundi 203 na jamaa hakujali kwasababu ilikua ni lazima kwa amri lasivyo Yuri ataenda na yey hataki.

Sasa Komarov aliondoka na hicho chombo na dakika 8 badaye alikua kwenye orbit tayari, sasa kashehe ikaanza kwenye Solar Panels kufunguka ambazo hua zinapokea mwanga wa jua na kutengenza umeme, na kadri muda ukivyoenda ndivyo shida zikazidi.
Komarov ikabidi ajitahidi kubadilisha orbit aliyokuwepo ili nafuu iwepo ila haikufanikiwa. Alivyotaka kufanya usahihisho ndivyo ambavyo kile chombo kilizunguka dunia kwa spidi isiyo ya kawaida.

Ndani ya masaa 5 alijaribu bila mafanikio kufanya astro-orientation, kukirudisha kwenye njia iliyotakiwa na kwa shida aliyopata ilifanya afanye trip 2 zaidi kuzunguka dunia na kufikia 18.

Maafisa wa anga baada ya kuona hivyo ikabidi waghairi mpango wao wa kutuma Soyuz 2 ambayo ndiyo ilikua ifanye orbital docking na Komarov ahame kwenye Soyuz 1 aje 2 hivyo ikabidi wapambane na yeye pia waweze kurudisha chombo duniani na Komarov alifanikiwa kuingia kwenye earth's atmosphere.
Wakati sasa anarudi huku akiwa na spidi kubwa, ilibidi atumie parachute ili atue salama na pia spidi ipungue ya hicho chombo. Ile Drogue parachute (hua zinatumika kupunguza spidi kwa vitu vinavyotembea angani na pilot anaweza itumia pia) haikufunguka na hata zile za akiba nazo hazikufunguka ipasavyo.

Kwa spidi kubwa sana huku kikionyesha dalili za kuungua, Komarov alianguka na hicho chombo na alifariki dunia.

Baadhi ya picha za sehemu alipodondokea ni kama hivi hapa chini:


Hapa chini ni maafisa wa jeshi ngazi za juu waliwasili





Mwisho: Inaaminika kifo cha Vladimir Komarov kilipangwa hasa ukizingatia tangu awali space capsule haikua sawa ila sababu ya anniversary ilibidi itokee.

Space Capsule ni nini?
Hiki ni kifaa ambacho kina uwezo wa kufanya safari za anga kwenda kwenye outer space na bado kikarudi duniani. Hiki ni tofauti na satellite na kinaizunguka dunia na bado taarifa zinapatikana kama kawaida.
Kiko hivi:


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…