Gamondi Gamondi Gamondi nakuita mara tatu

Gamondi Gamondi Gamondi nakuita mara tatu

Zile mechi nne za mwanzo kabla ya mechi ya Ihefu ya tarehe 4 mwezi wa 10 kocha alikuwa ni nani tofauti na huyu Gamondi? Huyu kocha si alitumia wachezaji wote kasoro Mshery pekee ndipo kaja kupoteza kwa Ihefu kwa kuwapanga wakina Sureboy? Sasa kama kikosi tu cha pili kinashindwa kumfunga timu ndogo ya Ihefu inayoburuza mkia je utasema mia, na wala sio wakina Musonda na Mzize wanaopata mipira ya counter hawajui wafanye nini zaidi ya kujigonga gonga tu.
Kuna kampeni ya chini chini imeanzishwa Gamondi aonekane mbaya, inatoka FC [emoji2772] na kuna watu wanaingizwa king
 
Sijui nani anafadhili hii kampeni yenu ya kumkataa Gamond. Na ghafla tu imeibuka baada ya mechi za kimataifa dhidi ya Medeama ili kuivuruga Yanga.

Hakuna rotation inayofanyika katika mechi ngumu zinazohitaji matokeo.

Hao wakina Nkane, Kibwana, na Farid Mussa mtawaona taratibu kwenye mechi zisizo na presha. Kila kocha lazima awe na first eleven yake ambayo ndiyo anayoiamini kwenye mechi zake ngumu, unataka kocha ampange Farid Mussa dhidi ya Al Ahly una akili wewe?

Yanga ndio kwanza kacheza mechi tisa tu za ligi kuu kuna mechi 21 zimebakia utawaona hao wachezaji kwenye mechi zingine za ligi na mechi za Azam federation cup ila sio kuingizwa ghafla tu kwenye klabu bingwa acheni ujinga

Nabi kacheza mechi gani ya kimataifa bila uwepo wa Mayele? Mnalinganisha uwezo wa kocha anayetumia Musonda na Mzize vs kocha aliyemtumia Mayele anayegombea tuzo?

Kwani ni kipi kinachokosekana Yanga zaidi ya straika wa maana? Unataka Gamondi aingie akafunge mwenyewe? Mpira unaochezwa na Yanga kwasasa hata Yanga ya Nabi haikuwahi kuucheza soka hili lenye kasi. Kina muangusha hana straika mwenye uwezo kama Mayele, magoli yanafungwa zaidi na viungo ambao inawapasa wafanye kazi zaidi na akili nyingi.

Kama Yanga wangekuwa na straika wa maana leo hii wangekuwa na point 6. Yanga ya Gamond inapiga counter, ina miliki mpira ila wakina Mzize wanajigonga gonga tu, vigugumizi vingi, kujiposition hawajui halafu lawama apewe kocha kwa lipi?

Midomo tu.
Si muende mpeleke CV mpewe Timu mfundishe.

Kuna kitu kinapandikizwa kwa mashabiki wa Yanga, inatengenezwa mazingira ya kuonekana kocha ni tatizo ili mashabiki wa react ili kocha atimuliwe.

Huyu kocha japo ana miezi michache ila aina yake mpira ni mpira wa kisasa, kama mapungufu kadhaa yatafanyiwa kazi ikiwepo mshambuliaji wa maana, na mawinga wa maana na beki kule wa kazi kazi kama Yao Kwasi hakika itakuwa habari nyingine kwenye soka la Africa.

[emoji736][emoji736] you are absolutely right

Nimegundua wamekuja kivingine ili Gamondi atoke baada ya 🖐🏿.

Gamondi Ana mkataba wa Miaka 2 pale yanga na ukiisha ataongezewa , raisi wa yanga sio kipindi kile cha yanga asili na yanga kampuni , sasahivi klabu ipo ki professional zaidi.

Nyambafffff
Leo mmeamua kuiita kampeni za wasioipenda Yanga na kujitoa kwenye sehemu ya wanao laumu mwenendo wa kocha.

Lakini nani asiyejua emotions za mashabiki wa Bongo kwenye timu zao za ndani?

Siku zote timu inapopata matokeo ndio kipindi ambacho unaweza kushuhudia mshikamano wa mashabiki katika kutoa maoni ya timu.

Lakini timu ikipoteza. Hayo yote mliyosema yanasemwa na wasioitakia mema Yanga mtayasema nyinyi.

Kati yenu hapo wapo waliotoa lawama kwa Kocha kwenye mechi ya juzi na sababu zilizotolewa zilikuwa ni hizi hizi ambazo wengine wakizitoa wanaonekana mamluki.
 
Leo mmeamua kuiita kampeni za wasioipenda Yanga na kujitoa kwenye sehemu ya wanao laumu mwenendo wa kocha.

Lakini nani asiyejua emotions za mashabiki wa Bongo kwenye timu zao za ndani?

Siku zote timu inapopata matokeo ndio kipindi ambacho unaweza kushuhudia mshikamano wa mashabiki katika kutoa maoni ya timu.

Lakini timu ikipoteza. Hayo yote mliyosema yanasemwa na wasioitakia mema Yanga mtayasema nyinyi.

Kati yenu hapo wapo waliotoa lawama kwa Kocha kwenye ya juzi na sababu zilizotolewa zilikuwa ni hizi hizi ambazo wengine wakizitoa wanaonekana mamluki.
Kama kuna mtu ana laumu eti Yanga inashindwa kufanya vizuri mechi za klabu bingwa sababu ya kocha hafanyi rotation basi huyo hajui mpira na hajui rotation hufanywa wakati upi au kipindi kipi. Ningeona wanaakili na wanajua mpira endapo hizi kelele za rotation ningezisikia baada ya kutolewa kikosi cha Yanga vs Mtibwa tarehe 16. Hiyo ndio mechi inayohitaji wachezaji kuwafanyia rotation.

Mtu anakwambia kocha hana mbinu bora ya Nabi, Nabi mbinu zake anazitengeneza kwa kumlenga mshambuliaji mahiri anayewania tuzo kwasasa. Mayele hakukosa mechi hata moja ya kombe la shirikisho na ndiye aliyechochea mafanikio ya Yanga. Ila leo mtu anatoa mlinganyo na mtu anayetumia Musonda na Mzize kama washambuliaji tegemeo. Huyo Nambi kwa mbinu zake mbona kashindwa kuibeba Far Rabat kucheza makundi?
 
Gamondi ni miongoni mwa wale makocha wanao amini the wining team never change...

Hii ubaya wake ni yule anayekaa benchi kila mechi kiwango chake kinadorora tofauti na yule anayecheza kila mechi ambaye kiwango chake huongezeka maradufu...

Tuombe majeruhi yatupitie mbali tusije tukapoteana.
 
Kama kuna mtu ana laumu eti Yanga inashindwa kufanya vizuri mechi za klabu bingwa sababu ya kocha hafanyi rotation basi huyo hajui mpira na hajui rotation hufanywa wakati upi au kipindi kipi. Ningeona wanaakili na wanajua mpira endapo hizi kelele za rotation ningezisikia baada ya kutolewa kikosi cha Yanga vs Mtibwa tarehe 16. Hiyo ndio mechi inayohitaji wachezaji kuwafanyia rotation.

Mtu anakwambia kocha hana mbinu bora ya Nabi, Nabi mbinu zake anazitengeneza kwa kumlenga mshambuliaji mahiri anayewania tuzo kwasasa. Mayele hakukosa mechi hata moja ya kombe la shirikisho na ndiye aliyechochea mafanikio ya Yanga. Ila leo mtu anatoa mlinganyo na mtu anayetumia Musonda na Mzize kama washambuliaji tegemeo. Huyo Nambi kwa mbinu zake mbona kashindwa kuibeba Far Rabat kucheza makundi?
We fala ndio hujui mpira, sie tunaongelea comparison ya squad rotation kati ya Nabi na Gamond then wewe unaleta uharo kunuka hapa.
Msimu uliopita wachezaji karibia wote walikuwa wanacheza tena kwa viwango vya juu Sureboy aliupiga mwingi kwa waarab mpaka wakashangaa, moloko, farid mussa na nkane mpaka ngushi wote walicheza kwa zamu na walikuwa wanakiwasha, ilifika wakati yeyote akianza ni sawa na aliye benchi kocha kazi yake ikawa kuangalia match hii nani anaendana nayo anamuingiza na ndio maana timu ikawa kipindi cha pili inabadilika. Lakini huyu Gamond hana hilo yeye mbinu yake ni kuwatumia wachezaji haohao wakifeli siku hiyo ujue mmekwisha, sisi wengine sio mashabiki maandazi kama nyie kila kitu mnaunga mkono.
 
We fala ndio hujui mpira, sie tunaongelea comparison ya squad rotation kati ya Nabi na Gamond then wewe unaleta uharo kunuka hapa.
Msimu uliopita wachezaji karibia wote walikuwa wanacheza tena kwa viwango vya juu Sureboy aliupiga mwingi kwa waarab mpaka wakashangaa, moloko, farid mussa na nkane mpaka ngushi wote walicheza kwa zamu na walikuwa wanakiwasha, ilifika wakati yeyote akianza ni sawa na aliye benchi kocha kazi yake ikawa kuangalia match hii nani anaendana nayo anamuingiza na ndio maana timu ikawa kipindi cha pili inabadilika. Lakini huyu Gamond hana hilo yeye mbinu yake ni kuwatumia wachezaji haohao wakifeli siku hiyo ujue mmekwisha, sisi wengine sio mashabiki maandazi kama nyie kila kitu mnaunga mkono.
Watacheza tu una haraka gani?
 
Juzi tu hapa Nkane , Mdathir , Sureboy , Farid Mussa , Moloko , Kibwana , Walikuwa ni wachezaji hatari sana hata kama walikuwa wanatokea Sub , ukianza kuhesabu magoal ya ushindi au perfomnce zao bora hapa hutoacha kukumbuka

Nkane aliipatia Yanga goli la kuwapa Taji la ASFC 2021/22 , baada ya ku-level Score board 3-3 kisha mikwaju ya penalty ikaamua , Bado Nkane aliendelea kupata nafasi kwenye Kikosi cha Nabi na alikuwa anafanya vyema sana

Mdathir , Aliwapatia Yanga goal la Kuongoza dhidi ya Tp Mazembe CAFCC , na lile goli lilichukua goli bora la group stage CAFCC , bado alikuwa na kiwango bora sana majuzi juzi

Sureboy , Master , Atakumbwa kwa kiwango kizuri alichokionesha kwenye mchezo wa kufuzu Group stage dhidi ya Club African , ugenini lakini mwamba ile match aliwaka sana na bado alikuwa ni mchezaji mzuri sana

Farid Musa [emoji119] Baller anayecheza namba nyingi pale Yanga , Beki wa kushoto , Winger wa kushoto , Middle aliwahi kuwapatia points 3 mhimu Yanga dhidi ya Tp Mazembe ugenini

Moloko , Moja ya winger nzuri kabisa na hatari sana , aliwahi kuwafungia goal la pili Yanga kwenye mchezo dhidi ya Real Bamako kwa mkapa

Kibwana Shomary , Si kulia si kushoto kote kote mdogo wangu anakaba na anashambulia ni kweli kazini kwake kuna kazi ila naye ni mzuri matches dhidi ya Dodoma Jiji , matches dhidi ya Al Merrikh ushashinda tayari na umefuzu naye anastahili kucheza

Ukiifuatilia Yanga , ilikuwa ni team ambayo kila mchezaji alikuwa ni hatari kulingana na Sub aliyokuwa anafanyiwa , lakini Yanga ya sasa et hawapati nafasi kinachoendelea ni niniii ? team ya taifa itarudi kule kule tulipo toka hakuna wachezaji wapya watakao itwa maana kibwana sasa hawezi kuitwa maana sub kila match

Coach wa Yanga ajitathmini na pengine anaweza asifike X-mas au hata mwaka mpya , mwenendo wa Kikosi cha Yanga sasa unafanya Pacome aje achoke sana ,

Japo ni coach wenu siwapangii majukumu ila huyu coach atatuulia vipaji vya hawa madogo ni vyema akasepa mapema , utaniambia nini nikuelewe kwamba Farid Musa hana kiwango cha kumpokea Max dakika za jioni ?

Tatizo hili COACH CHOYOOO SANA , Yanga ya msimu huu inaweza kuwa ndiyo Yanga nzuri kuishuhudia

@saniti
Mimi ni mwananchi Kwa hili naungana na wewe
 
Sijui nani anafadhili hii kampeni yenu ya kumkataa Gamond. Na ghafla tu imeibuka baada ya mechi za kimataifa dhidi ya Medeama ili kuivuruga Yanga.

Hakuna rotation inayofanyika katika mechi ngumu zinazohitaji matokeo.

Hao wakina Nkane, Kibwana, na Farid Mussa mtawaona taratibu kwenye mechi zisizo na presha. Kila kocha lazima awe na first eleven yake ambayo ndiyo anayoiamini kwenye mechi zake ngumu, unataka kocha ampange Farid Mussa dhidi ya Al Ahly una akili wewe?

Yanga ndio kwanza kacheza mechi tisa tu za ligi kuu kuna mechi 21 zimebakia utawaona hao wachezaji kwenye mechi zingine za ligi na mechi za Azam federation cup ila sio kuingizwa ghafla tu kwenye klabu bingwa acheni ujinga
Jibu hoja yake inamashiko sana mbona wakati wa Nabi walipata nafasi kwanini sasa?
 
Unataka kocha aweke ghafla tu new faces kwenye mechi ngumu za klabu bingwa Unaujua mpira kweli wewe?
Wewe ndo akili huna, Nabi kafanya rotation mechi za nusu fainali hadi fainali na team imecheza vizuri, sembuse mechi za group stage. Me nikwambie kitu, hawa kina pacome wataanza kupata injury muda sio mrefu, fatigue ipo juu sana kwao, washageuka kauka nikuvae.
 
Sijui nani anafadhili hii kampeni yenu ya kumkataa Gamond. Na ghafla tu imeibuka baada ya mechi za kimataifa dhidi ya Medeama ili kuivuruga Yanga.

Hakuna rotation inayofanyika katika mechi ngumu zinazohitaji matokeo.

Hao wakina Nkane, Kibwana, na Farid Mussa mtawaona taratibu kwenye mechi zisizo na presha. Kila kocha lazima awe na first eleven yake ambayo ndiyo anayoiamini kwenye mechi zake ngumu, unataka kocha ampange Farid Mussa dhidi ya Al Ahly una akili wewe?

Yanga ndio kwanza kacheza mechi tisa tu za ligi kuu kuna mechi 21 zimebakia utawaona hao wachezaji kwenye mechi zingine za ligi na mechi za Azam federation cup ila sio kuingizwa ghafla tu kwenye klabu bingwa acheni ujinga
Walikuwa wanacheza dhidi ya mechi ngumu za kimataifa dhidi ya Club Africain, Tp Mazembe na wanafunga
 
Nabi kacheza mechi gani ya kimataifa bila uwepo wa Mayele? Mnalinganisha uwezo wa kocha anayetumia Musonda na Mzize vs kocha aliyemtumia Mayele anayegombea tuzo?

Kwani ni kipi kinachokosekana Yanga zaidi ya straika wa maana? Unataka Gamondi aingie akafunge mwenyewe? Mpira unaochezwa na Yanga kwasasa hata Yanga ya Nabi haikuwahi kuucheza soka hili lenye kasi. Kina muangusha hana straika mwenye uwezo kama Mayele, magoli yanafungwa zaidi na viungo ambao inawapasa wafanye kazi zaidi na akili nyingi.

Kama Yanga wangekuwa na straika wa maana leo hii wangekuwa na point 6. Yanga ya Gamond inapiga counter, ina miliki mpira ila wakina Mzize wanajigonga gonga tu, vigugumizi vingi, kujiposition hawajui halafu lawama apewe kocha kwa lipi?
Nabi hakuwa na Pacome au Nzengeli
 
We fala ndio hujui mpira, sie tunaongelea comparison ya squad rotation kati ya Nabi na Gamond then wewe unaleta uharo kunuka hapa.
Msimu uliopita wachezaji karibia wote walikuwa wanacheza tena kwa viwango vya juu Sureboy aliupiga mwingi kwa waarab mpaka wakashangaa, moloko, farid mussa na nkane mpaka ngushi wote walicheza kwa zamu na walikuwa wanakiwasha, ilifika wakati yeyote akianza ni sawa na aliye benchi kocha kazi yake ikawa kuangalia match hii nani anaendana nayo anamuingiza na ndio maana timu ikawa kipindi cha pili inabadilika. Lakini huyu Gamond hana hilo yeye mbinu yake ni kuwatumia wachezaji haohao wakifeli siku hiyo ujue mmekwisha, sisi wengine sio mashabiki maandazi kama nyie kila kitu mnaunga mkono.
Ambaye hamjui mpira ni nyie mnaongea upumbavu na ujinga. Nabi alikaa na Yanga kwa misimu mingapi? Kitendo cha kocha kukaa muda mrefu kinamfanya ajue kila mchezaji ubora wake na madhaifu yake. Wewe unataka kocha aingie hata mwaka hajamaliza ajaribishe kila mchezaji wakati jambo lilishamuadhibu dhidi ya Ihefu.
Halafu malalamiko yamekuwa mengi utafikiri kwenye ligi Yanga imecheza michezo mingi ndio kwanza imecheza michezo 9 tu hapo kuna michezo kibao ya ligi kuu bado game 21 na hapo bado mechi za Azam federation kwanini mnaharaka ya kumpangia kocha?

Yanga kacheza mechi ngumu back to back nne kwenye ligi kuu, hakuha kocha anayehitaji point atacheza kamari ya kumueka nje Aucho ili Sureboy acheze.

Unasema kipindi cha Nabi hadi Ngushi alikiwasha, embu niorodheshee mechi alizochesha Ngushi wakati wa Nabi ni zipi wewe ni wakufata mkumbo usiyejua mpira. Huyo Ngushi kaonekana chini ya Gamond mpaka watu wakamsifia kwenye mechi ya Yanga vs Kaizer chief kuwa alinyimwa nafasi bure chini ya Nabi ila anakitu. Gamond akampanga tena kwenye mechi za ngao ya jamii akageuka mchezaji mwenye kifafa. Haya niambie ni mechi zipi uliona Nabi akimpanga huyo Ngushi?
 
Nimegundua wamekuja kivingine ili Gamondi atoke baada ya [emoji1616].

Gamondi Ana mkataba wa Miaka 2 pale yanga na ukiisha ataongezewa , raisi wa yanga sio kipindi kile cha yanga asili na yanga kampuni , sasahivi klabu ipo ki professional zaidi.

Nyambafffff
Hata Nabi alipigiwa kampeni kama hii mwanzoni, ili atolewe. Kwa hiyo hakuna jipya hapa.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Kuna kitu kinapandikizwa kwa mashabiki wa Yanga, inatengenezwa mazingira ya kuonekana kocha ni tatizo ili mashabiki wa react ili kocha atimuliwe.

Huyu kocha japo ana miezi michache ila aina yake mpira ni mpira wa kisasa, kama mapungufu kadhaa yatafanyiwa kazi ikiwepo mshambuliaji wa maana, na mawinga wa maana na beki kule wa kazi kazi kama Yao Kwasi hakika itakuwa habari nyingine kwenye soka la Africa.
Inawezekana hizi chokochoko zinaanzishwa na wachezaji wanaokosa namba
 
Back
Top Bottom