Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 2,331
- 7,733
Mind gameKama hawatapangwa na game yanga akapoteza basi uongozi wa yanga unatakiwa kuchunguzwa kwa kuhujumu timu
Wachezaji waliocheza game j3 na j4 wanashindwaje kufika Tanzania mpaka siku 3 kutoka ufaransa?
Mikwara tu hii wote watacheza keshoHata me hii habari imenichanganya sana.View attachment 2948077
Toka Mamelodi ilipotangazwa kucheza na Yanga, uongozi wa Yanga ulishaanza kujenga mazingira ya jinsi ya kujitetea na zahma iliyo mbele yao. Mapema sana viongozi na mashabiki walishaanza kuchanganyikiwa.
Walitaka wachezaji wao wasiitwe timu ya taifa wakati huo huo wakalalamika saaana kwa nini Dickson Job hajaitwa, hiyo ni dalili ya watu waliochanganyikiwa. Wakaja kwenye majeruhi ya Pacome mara ishu ikabuma kwa kuitwa na kwenda timu ya taifa, eti anaenda kuangaliwa na madaktari wa timu ya taifa, dalili nyingine ya watu waliochanganyikiwa. Wakaja kwenye vitisho vizito dhidi ya watakaovaa jezi za Mamelodi, baada ya kelele nyingi na barua nzito kutoka CAF, wakanywea.
Sasa hivi wanasema kina Diarra hawajarudi mpaka sasa na wale ambao walisema wameshapona wanadai wanaweza kuwakosa. Dalili za watu waliochanganyikiwa. Hizi taarifa ndiyo kabisa zitafanya mashabiki wao hata wale wa bure wasije uwanjani.
Hii mechi Yanga ingekaza bila kucheza hizi mind games ingeweza kutoboa. Tatizo imefanya mambo yamekuwa mengi.
Yanga na Pacome wasingeweza kuacha hiyo fursa ya kuitwa kwa mara ya kwanza ndiyo maana ishu ikabuma wakaona we nenda tu hii nafasi ni adimu.Mbona umeandika uongo na maelezo yaliyojaa hisia zako?
Yanga wangetaka wachezaji wao wasiitwe kwenda kwenye timu zao za taifa wangetoa statement kwenda kwenye hizo timu kuwa wachezaji wake hawawezi kwenda na hata wangezingizia majeruhi. Kwani kwa akili yako walioitwa wote walienda? Si kuna wachezaji wa vilabu vingine wameitwa na hawakuenda na sababu ikiwa majeraha. Hivyo hata kwa Pacome na wengineo Yanga wangetaka wasiende wangetoa taarifa kuwa Pacome ni majeruhi na hakuna kitu wangefanywa na hizo nchi.
Kuhusu kuvaa jezi za Mamelod aliyekataa ni waziri wako wa michezo na hakukataa za Mamelod pekee bali za timu zote za pinzani (Al Ahly na Mamelod) je wewe ulimsikia kiongozi gani wa Yanga akikataza?
Kuhusu Diarra na Aziz Ki kutofika kama ni kweli bado, huwa inatokana na mazingira magumu ya ndege kuja Tanzania.
Kuhusu majeruhi, pengine mchezo wa mpira umeanza kufatilia juzi hapa. Mchezaji kupona jeraha ni swala moja ila kuwa fit ni swala lingine. Kocha alichokiongelea hapo ni ishu ya fitness ya mchezaji kucheza kwenye ngumu. Nyie mnawaona tu uwanjani Aucho yupo mazoezini au Pacome yupo mazoezini na wenzake ila je anatimamu wa asilimia mia? Hilo ndilo linaloongelewa na kocha.
Kuwa mwanamichezo, sio kila mara unakuwa unatawaliwa na akili za kishabiki shabiki hata kufanya reasoning inakushinda
Yupi umemficha kati yao?Wapo kesho utawaona!