Gardner achakazwa baada ya kumkuwadia mwanae

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
14,747
Reaction score
24,250
Mitandao ya Kijamii na watu mbalimbali zikiwepo Asasi za Kijamii zimemshika pabaya kama siyo kumchakaza kwa comments mtangazaji Gardner baada ya kutoa kauli isiyo na chembe ya utu uzima.

Nisikuchoshe endelea...

Kati ya kauli iliyoibua mijadala mikubwa kwa sasa ni hii ya kijana mwenzenu Gardner Habash kuwa;



"Natamani mwanangu Karen awe na mahusiano na mtu mkubwa mwenye umri kama wangu 'Sugar daddy' ili amtunze, kwasababu watu wa umri wake hawawezi kumuelewa wala kumsaidia chochote, wao wenyewe wanatafuta maisha, halafu umpe mzigo kama huu ataweza kulipa bill zake?"

Moja ya komenti hii hapa: 👇

Mchango:

Soma:Gardner G. Habash: Sina ugomvi na Jaydee, nimemkojoza miaka 15, Naibu waziri aingilia kati..
 
Kuna watu wengine ni Baba Wazalishaji ila kunawengine ni Baba. Huwezi kumkuwadia binti yako namna hiyo. Au anafanya promo maana wanaojiita ma "Celeb" huwa wana stail zao za kutokea, si nasikia huyo binti ni msanii, au ndo anamtabulisha kwa stail hiyo.
 
Kweli maisha ya kuzoea kulelewa yanakufanya mpaka baba kuwaza na mwanao alelewe na wazee, amefikiria hata magonjwa kweli au anawaza mwanawe awe kitega uchumi chake? Kweli tuna viwanda vingi ni kujiongeza tu!
 
Nilichoona ni huyo msichana wa kwenye anavutia kuliko Halima.
 
Duh basi haka katoto katakuwa mtaani kamekitembeza mpaka mshua wake roho imeuma na hajapata faida yoyote zaidi ya kulipa bill za dogo. Masela wa kitaa watakuwa wanakanega kisela.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…