Gari ipi itanisaidia kubana matumizi



senkyu mkuu nafanyia kazi ushauri
 
Mi nishasahaugi siku nyingi kuangalia gari based on fuel consumtion! Mi naona yote sawa tu. Bora ufike unapotaka

mwenzio mi mtoto wa mkulima,hela nimezikutia ukubwani, in short kwetu mi ndio nimebutua natakiwa nikomboe wengine...
 

Kamata VW mgongo wa chura utadumu nayo kwa muda mrefu
 
...Tafuta Suzuki Sierra,iko na cc 660 halafu ni 4wd,una engage kama Hardtop!!lita 1 waweza kwenda mpk km 35,lol!!vitz,duet,swift pia s0i mbaya.

ubarikiwe for this info.
 
Sister choose Cami kama bustani zako zinakubidi kuingia barabara mbovu, sababu ipo juu na hakili mafuta,, Wataalamu wa magari mngenisaidia na mimi pia Kuna kigari nimekiona mtandaoni CIF DAR imenivutia kinaitwa Suzuki Aerio kina cc kama 1500 hivi, price yake na shape kamenivutia sana kwa routes zangu za Dar, but wasiwasi upo kwenye spare parts zake zinapatikana dar? au zinaingiliana na Swift,, msaada jamani nataka nikiwahi kabla hakijauzwa kwenye hiyo website
 
Cami naona kama ni nzuri iko juu hata kwa shep inapendeza, vtz imekaa kidada sana hata Mr ataogopa kutoka nayo

duu kumbe nilitakiwa nilimkumbe na mr pia kwenye kuchagua gari senkyuuu
 
hatimaye ng'ombe wamerudi zizini..!!! mtu angeambiwa akachonge tairi za kimasai


Kweli angalau siku hizi watu wamekuwa wastaarabu. Mwenzio anauliza unajibu utumbo.., si utoto huo, tena afadhali utoto huo unakuwa ni u~#^-/x . Tuendelee kuwa wastaarabu namna hiyo ili mtu akifika JF akute waerevu watupu. Wale wapumbavu wachache wanaojibu ujinga wataokoka nao pia.
 
Mi nishasahaugi siku nyingi kuangalia gari based on fuel consumtion! Mi naona yote sawa tu. Bora ufike unapotaka

Nyie mafisadi wa CCM si mnachukua mafuta ya bure kwenye vituo vya kuuzia mafuta kwa kuwasaidia hao jamaa kukwepa kulipa kodi!
 
kama unaweza ku-afford mafuta ya mawazo - why to buy a car? get one stroke ki-Bajaji -- the point is to move from point A to B: as i do.

nahitaji gari ili iweze kunisaidia kufanikisha baadhi ya malengo yangu, ni kweli nina pesa ya mawazo ndio maana nikaomba ushauri kwa hiyo pesa yangu ndogo gari ipi nitaimudu? bajaji sawa lakini bajaji haiwezi kunitoa mbezi ya kawe to mkuranga au mlandizi thanks anyway.
 
Cami ndio "mwake"
1) Iko juu so vibonde uchwara inapeta tu.
2) CC ndogo so ni economical kwenye mafuta.
3) 4WD so matope na vijimlima mshenzi havikusumbui.
4) Ni Toyota ambapo spare bwerere.
5)Kwa we mdada itakutoa kidogo, manake nacho kana sura nzuri tu.
Ila sasa Cami ana pacha wake anaitwa Daihatsu Terios, huyu sina uhakika sana nae kama wanafanana kila kitu na Cami pamoja na kuvaliana spares.
 
rav 4 nyingi zinaanzia cc 2000, nahitaji gari isyozidi cc 1300

Yeah RAV4 4 zinaanzia 2000 cc - 2400 cc na ni full time 4WD kwahiyo zinatafuna zaidi mafuta. Cami ni nzuri ina cc 1300 na ina part time 4WD so itakufaa kwa sehemu korofi.
 

Hapo kwenye red mkuu siyo kweli. Toyota Cami ni sawa na Daihatsu Terios. Walichofanya ni kuondoa tu nembo ya Daihatsu na kuweka nembo ya Toyota. Kwahiyo spare zake haziingiliani kabisa na Toyota zingine and they are expensive japo ni imara sana ukinunua unasahau.
 
Mtu anafahamu kabisa kuwa consumption ya mafuta ktk gari hutokana na engine cc, hapa huwa sipati tabu kuona kuwa hii ina kuwa kama show off!
 

asante kwa ushauri mkuu, lakini je hali ya hewa ya UK ni sawa na DAR??? leo dar in 28 c wakati Uk yote ni kati ya degree 13-17 C , london ndio wana 20 C , natokea maeneo ya mbezi ya tegeta then unaniambia niendeshe baiskel to nyerere road mahali nafanya kazi? sinitafika nimelowa jasho mwili mzima? au niende na baiskeli mkuranga? ntafika saa ngapi na kurudi saa ngapi? wakati naomba ushauri niliweka pia na concern zangu nadhani ungezingatia mahitaji yangu wakati wakunishauri, vinginevyo sio kila kitu wafanyacho wazungu kinafaa kwa mazingira ya kwetu,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…