Gari la zimamoto kwenye Uwanja wa Mpira la nini

Mhaiki2022

Senior Member
Joined
Jul 13, 2022
Posts
132
Reaction score
187
Kwa kweli nimekuwa nashangazwa sana kuona gari la zimamoto hapa bongo kila wakati mechi zikiwa zinachezwa, sasa najiuliza la nn badala ya kuweka ambulance nadhani ni chombo husika.

Nasikia kuna timu iliwahi kususia mechi kisa hapakuwa na gari la kuzima moto. Tubadilike wabongo
 
Likitokea tatizo la moto mkuu unadhani hiyo Ambulance ndo itazima?

Haya magari yanapaswa kuwepo kila sehemu yenye mkusanyiko si kwenye mpira tu!,yaani yanapswa kuwepo kwenye majengo yote yanayochukua mikusanyiko ya watu wengi,pia kumbuka hilo Jeshi ni la uokoaji pia si la zima moto pekee,wako hapo kwa ajili ya shughuli za uokoaji pia
 
Wale sio zima moto pekee... Ni jeshi la uokoaji pia, na ukiwaona usiwaze moto tu, ata mikanyagano ina itaji uokoaji!
 
Football hooliganism anything can happen
 
Uwanjaa unatumia gesi kusashataa nk#_&-+++
 
Kazi ya jeshi la zimamoto na uokoaji ni kuokoa na kukabiliana na majanga ya dharura.
Tatizo mnakosea kutaja zimamoto bila kuweka neno uokoaji.
Weka nena uokoaji ndipo uje uulize hilo swali la kipumbavu.
Kuzima moto ni kama 1/3 tu ya majukumu ya jeshi hili
 
Wale sio zima moto pekee... Ni jeshi la uokoaji pia, na ukiwaona usiwaze moto tu, ata mikanyagano ina itaji uokoaji!
Naongezea tu mkuu: Hata jukwaa laweza poromoka na watu wakafunikwa na kifusi bila kusahau shoti ya umeme itakayopelekea moto kutokea.
 
Simba wakishafungwa wachezaji wao wanaweza kulipuka kwa vilio afadhali zimamoto iwepo karibu
 
Trick ya kwenda kuangalia mpira bure, hakuna kitu hapo, mbona kikiwa ba mkutano wa injili hapo uwanjani huwa hawaendi? Hawa baada ya kuona Police wanaingia kwa kigezo cha kulinda usalama na wao wakaa wakabuni nnia ya kwenda kuangalia mpira ndio wakaja na hio staili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…