Gari RV4 lina tatizo la kutetema nikiwa nimesimama kwenye foleni au mataa au hata nikiwa nimesimama tu kawaida.

Gari RV4 lina tatizo la kutetema nikiwa nimesimama kwenye foleni au mataa au hata nikiwa nimesimama tu kawaida.

Unaonekana ni mama mkwe wa trump
Nimeshuja Jana tu toka Uchina hata kiswahili sikijui. Kumbe Natakiwa kuwa Mama mkwe wa Xxx ili Gari isitetemeke.. Gari linatetemeka kama genereta (Nitumie Kari au Kali)

mchina.jpg
 
Ni kama historia imejirudia Trump kawa Rais wa 47😂😂😂😂
View attachment 3145361
Sasa kuna Madhara Gani nikiendelea kuitumia Tumia😂😂😂 Maana daaaa gharama kumiliki magari naona niwakatishe tamaa vijana
Mpaka kuhisi huo mtetemo inamaanisha engine na gearbox havijakaza kama inavyopaswa kuwa. Unaweza usione athari kwa haraka ukiacha huo mtikisiko ila kwa muda mrefu inaweza pelekea kuharibu vitu vingine ambayo itakuongezea gharama.
 
Msaada Wadau,

Haka Gari RV4 lina tatizo la kutetema nikiwa nimesimama kwenye foleni au mataa au hata nikiwa nimesimama tu kawaida na Nikiwasha AC ndio kabisa linatetemeka hadi Viti vinatataka kung'ola,


Mlio unatoka kwenye injini na ukiweka gear position ya parking kutetemeka kunapungua,

Niliipeleka kwa mafundi wa garage wakasema ni mountain gear moja imekufa, tumebadilisha baada ya siku moja tatizo limejirudia hadi nahisi wanaotaka tujenge SGR kila kitongoji, Mtaa wamerudi kwa kasi ya Ajabu.

Naomba msaada wandugu mwenye kujua tatizo ni nini!!

Aksante Sana.
Nenda fundi jomba hilo dogo linatibikaaa
 
Kaka hapo kuna mambo matatu

1. Shida kwenye mfumo wa Idle control (Throttle au vaccum leakage kuanzia kwenye airfilter box na maeneo yote yanayo connect mtafute fundi akague)

2. Mfumo wa mafuta kagua kuanzia pump, filter na delivery ya mafuta kwenda kwenye engine kama ipo sawa.

3. Chunguza Spark plugs na ignition coils kama zipo sawa kama zinashida replace.

Mwisho kama una uhakika mounts zipo sawa basi tatizo lako linatokana na mambo hayo hapo juu. Pia ukipata changamoto za gari jaribu kutafuta solution kwenye site mbali mbali kama chat GPT kabla ya kuja huku watu wa huku wanawivu watakukatisha tamaa
 
Back
Top Bottom