GAS Mtwara vs Bandari Tanzania

GAS Mtwara vs Bandari Tanzania

don-mike

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2011
Posts
600
Reaction score
1,178
Miaka michache kabla ya utawala wa JK kufikia tamati kuliibuka swala la GAS Mtwara, kwa maneno ya Wapinzani mkataba wa Gas Mtwara ukapata pingamizi kubwa zaidi ya pingamizi zinazoonekana leo, hata kufikia wakati Jeshi likaingizwa kazini ndio mkandarasi aweze laza mabomba ya gas. Mabomba hayo leo ndio yanayopitisha Gas kwa uchache, inasemekana so far ni chini ya asilimia 15 ya uwezo wa bomba, ila gas hii ndio inayochangia 60% ya uzalishaji wa umeme Tanzania.

Yani isingekuwa haya mabomba kuna uwezekano mkubwa leo Tanesco ingeshakuwa mufilisi kutokana na matumizi ya mafuta ya diezel, kipindi unit moja ya umeme ni Sh 350 kwa bei ya Tanesco, ila ukizalisha umeme kwa mafuta ya diesel unit moja hufika Sh 700, na bei ya mafuta ilivyopanda leo, inawezekana kabisa Tanesco ingekuwa inatumia Sh 900 kuzalisha umeme inaouza Sh 350.

Watu wachache walieneza chuki kwa watu wa kusini, ikawa mtiti kweli kweli. Ila leo hii Gas hii ndio imeliokoa Shirika la Tanesco, na uchimbaji utavyoongezeka basi manufaa yatakuwa makubwa zaidi, sio tu kwa Tanesco bali hata kwenye magari na majumbani.

Leo hii tunaona mkataba wa bandari unavyopigiwa kelele, kuna vitu vingine vinaongewa kishabiki na kwa kupotoshwa kabisa, japo vichache kweli vinaleta mashaka, vitu kama bandari imeuzwa, ukomo wa mkataba, etc ni vitu vinavyoongewa kisiasa zaidi kuliko uhalisia. Mtu anakwambia anataka tukivunja mahusiano na Dubai basi mkataba uwe terminated, Hivi inawezekana vipi tumeingia mkataba na DPW wa miaka 25, wameshusha crane/lift za kutosha za kushushia makontena, then miaka miwili anaingia kiongozi mwingine anavunja mahusiano na Dubai na kuvunja mkataba na DPW, nani atalikubali hilo, na hata akilikubali, mahakama huko South Africa itaamua tofauti na tutapigwa mabiliani ya Shilingi kwenye kesi kama tunavyopigwa sasa kwenye kesi tofauti tofauti. Ikumbukwe kiini cha kesi zote hizi ni kuvunja mikataba kihuni bila sababu za msingi.

Swala la DPW kwa sasa ni swala lililotumika kuwapatia watu milage zaidi kuliko kutafuta ufumbuzi wa vipengele vichache vyenye kuleta walakini. Badala ya kujenga wachache wameamua bomoa kwa manufaa ya kwao kisiasa.

Miradi mikubwa nchini kila mara imekuwa ikipata mapingamizi mengi bila sababu za msingi. Bwawa la Nyerere lilipigwa vita na hao hao leo wanaolalamika mbona linachelewa washa umeme, SGR hii ilipigwa vita na hao hao leo wanaouliza mbona vichwa vya treni vinachelewa wakati wanajua fika Covid-19 ndio chanzo cha uzalishaji duniani kudorola, yapo makampuni ya uzalishaji magari yameshindwa timiza malengo yake na mengine kuuzwa kabisa kutokana na uzalishaji duni ulioletwa na Covid-19 plus vita ukraine.

Tesla Cybertruck ilikuwa iingie sokoni 2021, ila leo hii itaingia barabarani 2024, yote hiyo ni Covid-19 plus Ukraine war, TRC ni nani hata vichwa vya Treni vifike kwa wakati wakati dunia nzima imesimama.

Sitetei CCM, Sipondi Upanzani, ila nataka tu ujue kuna watu wanapotosha sana uhalisia wa mambo ulivyo kwa manufaa yao binafsi.

Kwaheri.
 
Mama asonge mbele asitishwe na yeyote.. Kwenye suala la maendeleo **** watu watakukatisha tamaa ila songa.. Baadae hao hao watakusifia.. Ngoja bwawa la umeme lianze kutoa umeme utasikia wanashangaa
 
Miaka michache kabla ya utawala wa JK kufikia tamati kuliibuka swala la GAS Mtwara, kwa maneno ya Wapinzani mkataba wa Gas Mtwara ukapata pingamizi kubwa zaidi ya pingamizi zinazoonekana leo, hata kufikia wakati Jeshi likaingizwa kazini ndio mkandarasi aweze laza mabomba ya gas. Mabomba hayo leo ndio yanayopitisha Gas kwa uchache, inasemekana so far ni chini ya asilimia 15 ya uwezo wa bomba, ila gas hii ndio inayochangia 60% ya uzalishaji wa umeme Tanzania.

Yani isingekuwa haya mabomba kuna uwezekano mkubwa leo Tanesco ingeshakuwa mufilisi kutokana na matumizi ya mafuta ya diezel, kipindi unit moja ya umeme ni Sh 350 kwa bei ya Tanesco, ila ukizalisha umeme kwa mafuta ya diesel unit moja hufika Sh 700, na bei ya mafuta ilivyopanda leo, inawezekana kabisa Tanesco ingekuwa inatumia Sh 900 kuzalisha umeme inaouza Sh 350.

Watu wachache walieneza chuki kwa watu wa kusini, ikawa mtiti kweli kweli. Ila leo hii Gas hii ndio imeliokoa Shirika la Tanesco, na uchimbaji utavyoongezeka basi manufaa yatakuwa makubwa zaidi, sio tu kwa Tanesco bali hata kwenye magari na majumbani.

Leo hii tunaona mkataba wa bandari unavyopigiwa kelele, kuna vitu vingine vinaongewa kishabiki na kwa kupotoshwa kabisa, japo vichache kweli vinaleta mashaka, vitu kama bandari imeuzwa, ukomo wa mkataba, etc ni vitu vinavyoongewa kisiasa zaidi kuliko uhalisia. Mtu anakwambia anataka tukivunja mahusiano na Dubai basi mkataba uwe terminated, Hivi inawezekana vipi tumeingia mkataba na DPW wa miaka 25, wameshusha crane/lift za kutosha za kushushia makontena, then miaka miwili anaingia kiongozi mwingine anavunja mahusiano na Dubai na kuvunja mkataba na DPW, nani atalikubali hilo, na hata akilikubali, mahakama huko South Africa itaamua tofauti na tutapigwa mabiliani ya Shilingi kwenye kesi kama tunavyopigwa sasa kwenye kesi tofauti tofauti. Ikumbukwe kiini cha kesi zote hizi ni kuvunja mikataba kihuni bila sababu za msingi.

Swala la DPW kwa sasa ni swala lililotumika kuwapatia watu milage zaidi kuliko kutafuta ufumbuzi wa vipengele vichache vyenye kuleta walakini. Badala ya kujenga wachache wameamua bomoa kwa manufaa ya kwao kisiasa.

Miradi mikubwa nchini kila mara imekuwa ikipata mapingamizi mengi bila sababu za msingi. Bwawa la Nyerere lilipigwa vita na hao hao leo wanaolalamika mbona linachelewa washa umeme, SGR hii ilipigwa vita na hao hao leo wanaouliza mbona vichwa vya treni vinachelewa wakati wanajua fika Covid-19 ndio chanzo cha uzalishaji duniani kudorola, yapo makampuni ya uzalishaji magari yameshindwa timiza malengo yake na mengine kuuzwa kabisa kutokana na uzalishaji duni ulioletwa na Covid-19 plus vita ukraine.

Tesla Cybertruck ilikuwa iingie sokoni 2021, ila leo hii itaingia barabarani 2024, yote hiyo ni Covid-19 plus Ukraine war, TRC ni nani hata vichwa vya Treni vifike kwa wakati wakati dunia nzima imesimama.

Sitetei CCM, Sipondi Upanzani, ila nataka tu ujue kuna watu wanapotosha sana uhalisia wa mambo ulivyo kwa manufaa yao binafsi.

Kwaheri.
Kila kitu kina pande mbili, ubaya na uzuri. Mazuri ya mkataba huu yanasemwa na serikali na inatumia gharama kubwa sana, bila kusoma vifungu vinavyo onyesha mazuri hayo. Kibaya zaidi ni serikali kupitia CCM kuwataka wananchi waiamini ili hali serikali ya CCM imekuwa ikiingia kwenye kashfa kubwa ya kuchukua fedha za umma pindi ukaribiapo uchaguzi. Swala la bandari limepita (kesi iliopo mahakamani kupinga ni gheresha kwani hatuna mahakama huru Tanzania), si kwa kuwa lina manufaa, bali kupata hela za uchaguzi kwa masilahi ya wachache.
 
Umeongea bila kufikiria, kwa ulewa wangu hakuna mtu anayepinga uwekezaji bandarini, kinachopingwa ni mkataba. Binafsi nimeuona mkatabata uongo ni dhambi, mkataba unamakosa mengi. Ni vyema urekebishwe ndio mchakato uendelee.
 
Kwani unapingwa uwekezaji bandarini, au mkataba wa Kimangungo?
Naongelea upotoshwaji wa baadhi ya vifungu kwa wanaopinga mkataba wa bandari.

Upotoshwaji wa makusudi unaofanywa na watu ambao dhahiri shairi wanajua kuwa wanapotosha, ila huo upotoshaji unawanufaisha wao kisiasa.
 
Mama asonge mbele asitishwe na yeyote.. Kwenye suala la maendeleo **** watu watakukatisha tamaa ila songa.. Baadae hao hao watakusifia.. Ngoja bwawa la umeme lianze kutoa umeme utasikia wanashangaa
Unajua ulichoandika au ndio wale wale machawa?........
 
Hizo takwimu za kwamba umeme unazalishwa na gas asilimia 60 umezipata wapi

Generation Planning
Total installed capacity in the country is 1,602.32 MW which comprises of interconnected Grid System (1,565.72 MW) and isolated Grid System (36.60 MW). The National Grid System comprises of hydro and thermal generation units owned by TANESCO and IPP’s with total capacity of 1,565.72 MW (base year 2019) out of which hydro 573.70 MW (36.64%), natural gas 892.72 MW (57.02%), liquid fuel, 88.80 MW (5.67%) and biomass 10.50 MW (0.67%). The highest system Maximum Demand (MD) recorded was 1,120 MW reached on 30th November 2019.
 
Mama asonge mbele asitishwe na yeyote.. Kwenye suala la maendeleo **** watu watakukatisha tamaa ila songa.. Baadae hao hao watakusifia.. Ngoja bwawa la umeme lianze kutoa umeme utasikia wanashangaa
Unaandika vitu mpaka kama huna kichwa hadi JF inaamua kukusitri.
 
Umeongea bila kufikiria, kwa ulewa wangu hakuna mtu anayepinga uwekezaji bandarini, kinachopingwa ni mkataba. Binafsi nimeuona mkatabata uongo ni dhambi, mkataba unamakosa mengi. Ni vyema urekebishwe ndio mchakato uendelee.
Naamini tupo mtumbwi mmoja, na mtumbwi wetu sio ule wa vibwengo anaousema Prof. Tibaijuka.
Nachoongelea hapa ni upotoshwaji wa wazi kabisa unaofanywa na wapinga mkataba. Sijabisha kwamba kuna vifungu vina walakini, ila vifungu vingi vinatumika kupotosha, mfano mmoja ni kifungu cha kuuza bandari. Kwajinsi mkataba ulivyo hakuna mahala pameandikwa au maanisha bandari imeuzwa, ila leo watu wanakimbia nchi nzima wakisema bandari imeuzwa.
 
Tanzania to sign Sh70 trillion LNG project
umeleta article iliyoandikwa 2018 wakati Magufuli ameamua weka mradi wa Mtwara kwapani kwa kuogopa tu nufaisha waliomtangulia maana tayari walishajiwekeza kunufaika na mradi wa gas..... kwa taarifa yako tayari makubaliano yanaenda fikiwa, uwekezaji wa trilion 70 unaenda fanyika Mtwara.

Maendeleo hayana chama.
 
Tanzania to sign Sh70 trillion LNG project
umeleta article iliyoandikwa 2018 wakati Magufuli ameamua weka mradi wa Mtwara kwapani kwa kuogopa tu nufaisha waliomtangulia maana tayari walishajiwekeza kunufaika na mradi wa gas..... kwa taarifa yako tayari makubaliano yanaenda fikiwa, uwekezaji wa trilion 70 unaenda fanyika Mtwara.

Maendeleo hayana chama.
Mkuu,

Unajua kusoma?

"Tanzania’s gas boom that never was – when local hopes are dashed by global realities

Published: July 12, 2023 10.36am EDT"
 
Kwamba unadhani kelele ndo zitazuia uwekezaji kwenye bandari?
 
Mkuu,

Unajua kusoma?

"Tanzania’s gas boom that never was – when local hopes are dashed by global realities

Published: July 12, 2023 10.36am EDT"
last paragraph author anasema
Since this research has taken place, there has been considerable change in the energy landscape. Russia’s invasion of Ukraine has pushed up gas prices, and European leaders have begun to see Africa as a potential source of natural gas. There is once again the “potential” to create Mtwara into a true resource frontier. But it remains to be seen if such rising prices recreate excitement on the ground.
sasa mwandishi mwenyewe wa West Africa, utaamua mwenyewe unachagua habari ya West Africa au The Citizen ya hapa hapa Bongo.
 
Back
Top Bottom