TANZIA Gavana mstaafu wa BoT, Profesa Benno Ndulu afariki dunia

Wapi hasomeki?

Kwamfano ungekuwa mshauri wake ungemshauri afanyeje kwenye suala la corona?
 
Wapi hasomeki?

Kwamfano ungekuwa mshauri wake ungemshauri afanyeje kwenye suala la corona?
Ni muhimu akubali kuwa ipo kwani yeye ndiye mwenye kaya. Pia asiibeze sayansi kwani ina mchango mkubwa sana kwenye ili janga. Si sahihi kuwashauri wananchi washone barakoa za matambara kwani hazitokuwa na msaada. Chanjo haiepukiki, Uingereza wagonjwa wanaolazwa kwa COVID-19 wamepungua kwa asiliamia 90 sawasawa na wales, Scotland n.k. Yako mengi na muda ni mdogo, mengine jazia
 
Wewe ni kapumbavu! Kwahiyo una takwimu za waliokufa hapa tz ni wengi sawa na ulaya? Wote wanaokufa una thibisha kwamba ni corona na si magonjwa mengine?

Hiyo tahadhali unayosema rais achukue ni ipi? Kama huko kwingineko wamefanya yote na wamekufa kwa malaki wewe hapa ulitaka rais akufanyie nini?
 
Akikubali kuwa ipo ndio watu hawafi?
 
Tanzania hakuna korona
 
Wewe unashindana upumbavu na baba yule. Kama huna takwimu za Tanzania unawezaje kusema waliokufa ni wachache kuliko Ulaya? Ulaya wasingechukuwa tahadhari wangekufa wengi mno mno kwa sababu population yake wazee ni wengi. Je unajua kwa mfano UK population ya watu milioni 60 wenye umri wa miaka 65 kwenda juu ni around milioni 13 na nusu wakati Tanzania tukiwa na idadi ya watu kama hiyo ni around milioni 1.8 tu? Kwa maana nyingine ni kuwa wale waliokuwa kwenye hatari ya kufa kwa corona hapa kwetu wameshatangulia mbele ya haki kwa magonjwa mengine. Sasa imagine wangefanya ujinga wa kusema ''tumtangulize Mungu mbele'' na wasichukue hatua wangekufa wangapi. Ndugu wakati mnawaambia watu wamtangulize Mungu mbele mbona ninyi kwenye msafara mnatanguliza mapikipiki na polisi wenye silaha badala ya Mungu?
 
Apumzike kwa amani.


Halafu kuna jitu linasema vifo vipo tu. Afe yeye basi
Kwa matamshi yake hatuna sababu ya kuwa sumbua watu kusomea udaktari (miaka mingi na risk nyingi). kuharibu pesa kujenga zahanati, vituo vya afya na hospitari, kujifukiza nk nk. Ni kweli kifo ni lazima muda ukifika, lakini kufa kwa uzembe ni upumbavu.
 
Mkuu don't waste your time na vichwa vyenye vumbi badala ya ubongo!
 
Utinge usitinge, bado nasema si kila anaekufa amekufa kwa Corona. Kilichomuua Benno sikijui na sijakiona kikitajwa hapo, huenda ni COVID, Huenda sio COVID. Kabla ya Covid watu bado walikua wanakufa
Tena kabla ya Corona sababu za mwanzo ilikuwa ni shinikizo la damu.....kila jambo lazima liwe na sababu
 
Ingekua ugonjwa unambukizwa na mbu ningejikinga na mbu. Ila unasambazwa na punguani wasiotaka kufata masharti. Na wanabwabwaja ovyo kwa ujuaji wa oooh vifo vipo siku zote. Wamejivika roho ya mauti. Mlinde mwenzako hata kama hupendi kuishi. Ujuaji ndani ya vita huangamiza kikosi na taifa.
Umakini kila hatua huponyesha taifa.
Hakuna siasa itasaidia. Sayansi iliyotengeneza kirusi ndio sayansi itakayokiondoa.
Kuna familia zinazika watu 2 na kuendelea ndani ya week 1.
Taifa likituliza akili tutaweza kujua peaks za kila wave na kujilinda na kupunguza vifo na maambukizi.
Tukikaa kwa mizaha na siasa taka tunaumiza wasiohusika. Na hakika hukumu yetu itakua kuu kwa vile tumepewa akili, tumepewa muda wa kujifunza kupitia mataifa mengine. Athari za Corona si katika ugonjwa na vifo tu bali uchumi na maisha ya kila siku.
Tuweni na hekima kwani kila kitu kitapita bali jinsi tunavyoweka dunia salama tutakumbukwa
 
Apumzike kwa amani Baba. Huyu mshua nitamkumbuka sana ndiye aliyenipa scholarship ya kusoma masters ya uchumi pamoja na kazi.

Dr. Likwelile aliyefariki juzi aliyekuwa katibu mkuu hazina alisimamiwa andiko lake la Ph.D na Prof. Benno mwaka 1991 - 1996.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…