Gawio la hisa za CRDB

Mimi ndo niliuliza ni kigezo gani walifikia kutoa gawio la Tshs.36 kwa hisa. Pili, natumaini idadi ya Wakurugenzi ni kama 10 na katika taarifa watalipwa kama Tshs.965,0000,000 kwa mwaka na hivyo kila Mkurugenzi atalipwa Tshs.96,500,000 kwa mwaka na hiyo ni nje ya gharama ya safari na inawezekana wanalipwa na malazi kama complimentary na halafu ulinganishe Tshs.36 kwa hisa moja. Pili, ni kwanini ajenda ya malipo ya Wakurugenzi huletwa tu kama taarifa na kupitishwa bila majadiliano. Wanahisa wanatakiwa waelezwe kigezo cha malipo hayo. Tatu, kwa nini vikao vya Wanahisa kusiwe kwa mzunguko?. Mfano leo Arusha, Kesho Mbeya, Kesho kutwa Mwanza nk. Nawashauri Wanahisa wenzangu tusiwe watu wa ndiyooooo tuwe tunauliza maswali na kudadisi taarifa nzima katika vikao vyetu.
 
Mkuu pesa wanayolipwa wakurugenzi ni gharama kama zilivo gharama (liabilities) zingine za uendeshaji wa kampuni, wakati kinachokuja kwa wanahisa ni sehemu ya net profit (baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji). Katika hiyo net profit ndo inaamuliwa na mkutano mkuu wa wanahisa (wakiongozwa na sera ya kampuni husika) kiasi gani kiende kwa wanahisa na kiasi gani kirudi kwenye kampuni kukuza mtaji, hivyo kile kiasi kilichoamliwa kiende kwa wanahisa ndo kitagawanywa kwa jumla ya idadi ya hisa katika kampuni kujua kila hisa itapata gawio la sh. ngapi. Na ktk mkutano huo wanahisa maamuzi yanayofuatwa ni ya wale wanahisa wakubwa (wenye hisa nyingi), hawa wengine ni ndiyo mzee, na ndio utaratibu. Ukiwa top holders unakua sehem ya maamuzi.
 
Na wenye hisa nyingi wengi wao ndio wakurugenzi, yaani ni mwendo wa kula kote kote. Dah wakubwa wanafaidi aisee.
 
Maturity period yake ni lini?
Minimum deposit ni kiasi gani?
Haijafungwa hii Mkuu?
Ninawasilisha na ninatanguliza shukrani zangu za dhati.
NMB na wao wameanzisha jasiri bond fund ambayo nayo wanatoa 8.5% per annum ambayo ni nzuri kuliko. Kupanga ni kuchagua ipi ni bora zaidi.
 
Mleta mada nadhani unahitaji elimu ya kutosha kuhusu uwekezaji kwenye hizi kampuni.

Kama hisa za crdb kwa sasa ni tsh.430, unadhani gawio la faida litaendana na lile la nmb ambao wananunua hisa kwa tsh.3,000?

Kama kiwango cha chini cha hisa kwa kila kampuni ni hisa 100, manake crdb utanunua hisa 100 kwa tsh.430,000 wakati nmb utanunua hisa 100 kwa 3,000,000. Gawio la faida kwa crdb itakuwa 3,600[emoji1787] wakati nmb itakuwa 10,000[emoji1787].

Sijui ninepuyanga!!
 
Unalinganisha investment ya 430,000 dhidi ya 3,000,000 then unataka return iwe sawa. Kwani mtu anashindwa nini kununua hisa tofauti ila za thamani sawa.

Na dividend policy haitegemeani na share price. Kampuni inaweza kuwa na price kubwa na haitoi dividend. Vodacom wana hela kibao, gawio lao hulioni na kipande hisa yake ni chini ya 1000 nadhani. TBL walikuwa 10,800 TZS sijui kama ilipanda, gawio lake kubwa mbali kuliko hiyo NMB
 
Mkuu mimi sina utaalam katika hii kitu, niliwahi kununua shares za dahaco miaka hiyo, sikupata hasara coz nilichoambiwa na broker ndicho nilikuwa nafanya. Nilipata dividends na nilipotaka kuuza shares zangu nilipata faida. It was worth it kuliko ningeweka bank.
 
Swali hapo ni justification ya kuwalipa hao Directors kiasi hicho cha fedha hata kama uamuzi huo umewahusisha major shareholders!
These directors expenses are icluded in the overall operating costs hence their negative effect in reducing the profit! The lower the profit the less will be the dividends to be distributed.
 
Wenye shares chache ndio huwa mnalalamika hivi.
 
Bank haipo kwa ajili ya kusaidia mtu
 
Nimepiga hesabu ukiwekeza NMB sh milioni tano utapata gawio la sh 166000 ukiwekeza CRDB utapata gawio la sh 412800 kama nipo sahihi hakupaswa kulalamika. Swali langu la msingi je hilo gawio wanatoa kwa muda gani ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…