Gazeti la The Economist: Rais Magufuli na CCM kuendelea kushika madaraka baada ya Uchaguzi Mkuu

Gazeti la The Economist: Rais Magufuli na CCM kuendelea kushika madaraka baada ya Uchaguzi Mkuu

Hili gazeti limetuharibia kabisa sisi wapinzani kwa wahisani wetu maana tuliwaaminisha kuwa tutashinda uchaguzi ujao kwa kishindo cha msingi watupe tu pesa kwa ajli ya maandalizi sasa sijui tutawashawishi vipi tena watuelewe. Tulisusia uchaguzi wa Serikali za mitaa ili wahisani wasije kujua kuwa sisi bado dhaifu na wasingetupatia pesa tena. Hakika hili ni pigo kwetu sisi wapinzani.
 
Mtu mwenye akili timamu na fikra pana hawezi kuzifanya hisia za mtu fulani kama ndio ukweli!

Wewe kama unazielewa hisia zako, mimi sio jukumu langu kuzielewa au kujifanya sizielewi kwa sababu kufanya hivyo nitakuwa ninatumia akili na fikra zangu vibaya!
Weka sababu za Economist kwanini Magufuli atashinda, wacha kelele..

Au na wewe hapa unataka tujadili hisia za hao wazungu?!

Ziweke hapa halafu tuanze kuzijadili, kama ni positive au negative, but sio kukurupuka tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna sehemu ndani ya maoni yako ninakubaliana nawe lakini pia sehemu nyingine sikubaliani nawe.

Ni kweli kwenye Urais wa Tanzania haina mjadala! Labda Urais wa Zanzibar!

Kumbuka Wabunge na madiwani wengi wa upinzani walishinda kwa sababu ya CCM kuvuruga mchakato wao wa ndani katika kuwapata wagombea kwa tiketi ya CCM. Kama CCM watajirekebisha katika mchakato wa kuwapata wagombea basi wapinzani watakuwa na wakati mgumu sana!

Hata wakati ccm wako vizuri upinzani walipata viti vingi vya ubunge na kila uchaguzi wanaongezeka na hata this time kama chadema wakimsimamisha lissu take my word wabunge watakaa na wengi watarudi
 
Gazeti pia linatoa ujumbe kwa wapinzani kuwa wajiandae kwa ''mafuriko ya kisiasa''!
Nisilo elewa mimi na hii elimu yangu mangungu ni kuwa inakuwaje kwenye uhakika huo wa ushindi bado ccm inakosa confidence?
Haitaki kutoa nafasi sawa za kufanya siasa, imewaamuru Polisi kuwadhibiti wapinzani kila kona, haitaki Tume huru ya uchaguzi na mengineyo ya aina hiyo? Unauhakika wa ushindi inakuwaje uwahonge na kuwatisha marefa?
Nadhani hata hao wabobezi wa Economist wameliona hilo kuwa kwa vile hali ni hiyo basi hakuna namna lazima wajitangaze ushindi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
This is very true, not only CCM will retain a firm grip on power, but for a long time to come, in facts, CCM Itatawala Milele, anayebisha abishe tuu for the sake of kubisha, unless ni kwa msaada wa watu wa Marekani!.
P


Mpaka hapa nilikuwa najiuliza nini hasa lengo la mleta mada kwa suala lililo wazi kabisa (obvious). Wenye interest na siasa za Tanzania hawana shaka kuwa hususan “Under the leadership of John Magufuli, the long-standing ruling party, the CCM, will retain a firm grip on power’’. Huhitaji utafiti wa haja wala kauli ya The Economist kujua hilo. Kwa EIU huo ni mteremko.

Na sidhani kama ni vyema kufurahia kauli ya aina hiyo iliyokaa kikejeli kejeli tena baada ya muda mrefu wa kubainisha uhasama kati ya gazeti hilo na serikali. Hivi kauli ya “a firm grip on power” imeeleweka ipasavyo? Is that something positive?
 
Nisilo elewa mimi na hii elimu yangu mangungu ni kuwa inakuwaje kwenye uhakika huo wa ushindi bado ccm inakosa confidence?
Haitaki kutoa nafasi sawa za kufanya siasa, imewaamuru Polisi kuwadhibiti wapinzani kila kona, haitaki Tume huru ya uchaguzi na mengineyo ya aina hiyo? Unauhakika wa ushindi inakuwaje uwahonge na kuwatisha marefa?
Nadhani hata hao wabobezi wa Economist wameliona hilo kuwa kwa vile hali ni hiyo basi hakuna namna lazima wajitangaze ushindi

Sent using Jamii Forums mobile app
Sumu hailambwi kwa ulimi
 
T
INTELLIGENCE UNIT ni sehemu ya kitengo ndani ya Gazeti la The Economist ambacho hufanya uchunguzi na utafiti wa kisiasa na kiuchumi kwa nchi mbali mbali duniani na kutoa matokeo au matarajio.

Kitengo hiki cha kiuchunguzi kina wafanyakazi wabobezi zaidi ya 100 duniani ambao hutoa tafiti na utabiri baada ya uchunguzi kuhusu masuala ya kiuchumi kwa nchi mbali mbali kila mwanzo wa mwaka kulingana na mazingira halisi.

Ikumbukwe kuwa gazeti la The Economist limekuwa mwiba mkali hasa kwa Rais Magufuli kwa sababu linaamini sera za kisiasa na kiuchumi za Rais Magufuli zinaenda kinyume na mtazamo/msimamo wa kisiasa na kiuchumi wa gazeti hili.

Kwenye suala la kiuchumi, The Economist linaamini katika Ubinafsishaji na kuachia uchumi huru bila ya serikali kuingilia kati. Kwenye suala la kijamii, The Economist linaamini katika ndoa za jinsia moja na kuhalalisha utumiaji wa baadhi ya madawa ya kulevya kama bangi.

Ukitaka kujua msimamo wa Gazeti la The Economist kuhusu masuala ya kisiasa na kiuchumi;
GONGA LINK HII>>>Is The Economist Left or Right Wing

Hata hivyo linapofika suala la uchambuzi na utafiti, gazeti la The Economist hutoa matokeo ya tafiti na utabiri kama ambavyo jopo la wachunguzi wake limeona na kufikia hitimisho.

Kwenye masuala ya kisiasa nchini, jopo la wachunguzi wa INTELLIGENCE UNIT limesema baada ya Uchaguzi Mkuu, Rais Magufuli na CCM wataendelea sio kutawala tu bali pia watahodhi kwa kiwango kikubwa madaraka ya nchi.

Kwenye masuala ya kiuchumi limesema pamoja na kwamba serikali ya Rais Magufuli imeonesha mipango na nia ya kuboresha uwajibikaji katika sekta za umma na kuboresha maisha ya wananchi lakini inakabiliwa na uwezo mdogo kifedha.

INTELLIGENCE UNIT imebainisha kuwa, kutokuwa na utungaji sera ulioeleweka nchini kutawafanya wawekezaji kuogopa kuwekeza nchini, hata hivyo matarajio kwa nusu ya mwaka yanaonekana kuwa imara kutokana na kukua kwa sekta ya utoaji huduma nchini na uwekezaji kwenye miundombinu kitaifa.

Ukitaka kusoma repoti yote;
GONGA LINK HII>>>ENTELLIGENCE UNIT: Tanzania political and economic forecast

The economist hawa wanafiki tu!
Sasa ndo wanajifanya kuanza kubalance story sio?
Too late, tulishawastukia siku nyingi sana. Maleongo yao na wanayemtumikia tunayajua hata mkijifanya leo mnakuwa neutral na kuanza kuuona ukweli.
 
Kwahiyo nawe umekubaliana na hili gazeti kwamba serikali ya Meko INA uwezo mdogo kifedha?

Mwenyewe (Meko) si ndiye amekuwa akituaminisha kwamba serikali yake ni ya kitajiri na kwamba nchi hii ina uwezo hata wa kutoa misaada kwa nchi nyingine!

Tukisema Meko kaharibu uchumi wetu mnapinga.
Hii nchi uchumi uko hoi tofauti na ilivyokuwa enzi za Kikwete na Mkapa.

Standard ya maisha ya watu inazidi kushuka kila iitwapo leo. Watanzania hawana uhakika hata wa milo miwili kwa kutwa.

Si watumishi wa umma, wafanyabiashara, wakulima, wamachinga na hata wavuvi wanaofurahia maisha, wote wamepigika. Leo nyanya moja inauzwa kwa sh. 500 lakini bado Meko na serikali yake ya kidhalimu wanataka kutuaminisha kwamba maisha ya watanzania ni mazuri.

Nakuhakikishia kwamba CCM na huyo dikteta wenu mtapata taabu sana kwenye kampeni za uchaguzi 2020. Sijui mtawaambia mini wananchi hawa waliopigika.
Wafikishie ujumbe wale wanaowaita mabeberu kuwa Gazeti la The Economist limeandika,‘’Under the leadership of John Magufuli, the long-standing ruling party, the CCM, will retain a firm grip on power’’.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
T

The economist hawa wanafiki tu!
Sasa ndo wanajifanya kuanza kubalance story sio?
Too late, tulishawastukia siku nyingi sana. Maleongo yao na wanayemtumikia tunayajua hata mkijifanya leo mnakuwa neutral na kuanza kuuona ukweli.
Ukweli UPI wameuona ambao hawaujui? Wanajua kila kitu kuhusu sisi. Na wanatujua kuliko tujijuavyo wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
This is very true, not only CCM will retain a firm grip on power, but for a long time to come, in facts, CCM Itatawala Milele, anayebisha abishe tuu for the sake of kubisha, unless ni kwa msaada wa watu wa Marekani!.
P
Huu ujinga sasa paschal Mayala

Wewe hiyo milele utakuwepo wewe utaishi milele change your Mind

Mtu unayeweza kudead hata baada ya leo unajuaje CCM itatawala milele



Sent using Jamii Forums mobile app
 
MsemajiUkweli,

Swala la idadi ndogo ya wabunge wa upinzani me sitaki kuamini Coz kila uchaguzi huwa tunahisi hivyo na matokeo yake ndio kwanza wanajaa,

Me nadhani watanzania wanawaamini sana upinzani kwenye ubunge kuliko kwenye urais

Na la urais linakuwa gumu sana hasa kwenye kuunda serikali bcoz upinzani hawana watu ambao wanaweza kusema wanaunda serikali
Hiyo paragraph yako ya mwisho sio kweli. Watanzania wanakaribia milioni sitini halafu unadai unafikiri wapinzani hawana watu wa kuweza kuunda serikali.

Ina maana malioni woote hao ni ccm au wewe unafikiri chama kingine kikija madarakani ndio Civil Service yoote inaoondolewa.

Watanzania kwa kuwa ni chama kimoja tu ndicho kinatawala siku zote hamuelewi chama kingine kikishika dola hali inakuwaje, mnafikiri kitapashwa kutafuta hata watendaji kata na ma-das kutoka nje ya nchi. Very sorry.
 
Mkuu Pascal Mayalla huhitaji kuomba ruhusa lakini hata hivyo umeonyesha unyenyekevu kitaaluma kwa kuomba ruhusa!

Tumia utakavyo hasa kwa manufaa ya kuelimisha wajinga wa hapa Jamiiforums!
I believe wewe ndie mjinga namba moja kuleta vitu visivyo na sababu halafu unataka werevu wajadili, considering ulivyoisifia hiyo Intelligence Unit ya hao jamaa zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom