Geita: Chuo Kikuu cha Utumishi wa Umma kujenga Kampasi yake Wilayani Chato

Geita: Chuo Kikuu cha Utumishi wa Umma kujenga Kampasi yake Wilayani Chato

Why chato, zamani ilikuwa Bagamoyo. Mara gesi bagamoyo. Bandari Bagamoyo.

Ukweli kila zama na kitabu chake, baada ya hapo utashangaa inakuwa Mkuranga na walamba viatu wa wakati huo watakuja na justification zao.

Any way ila Mkulu alisema ni kujipendekeza kupeleka kila jambo chato.
 
Niliona Kwenye Baraza Langu La Mawaziri Ninaloliteua Lisikose Wazee, Nimemteua Captain Rtd, George Huruma Mkuchika. Kuwa Waziri Wa Utawala Bora


Huyu Mzee Haina Maana Awamu Iliyopita Alifanya Vizuri Sana, Laa!! Hashaa! Nataka Sasa Hivi Ukachape Kazi, Bora Ukosee Kwenye Kuamua Lakini Jambo Limefanyika
Siyo Kusitasita

😀😁😂🤣😃😄😅😅😄😃🤣😂
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Unafananishaje Arusha /Mirerani na Chatto kwenye kuchangia pato la taifa?
Ni mbingu na ardhi.

Na kama unadhani CCM ilishinda kihalali basi unahitaji msaada wa tiba ya akili.
Nenda kapimwe akili yako, Chato Ipo Geita. Unadhani mchango wa Geita kwa pato la Taifa ni mdogo?

Kwa mfumo wa nchi hii maendeleo hayapelekwi kwenye eneo kulingana na mchango wake kwa Taifa na ndio maana Arusha juzi hapa imepata 500 Bilioni za maji.

Kuna factors muhimu za kujenga hicho chuo Chato kanda ya Ziwa. Tatizo mnasumbuliwa na wivu wa kike na ukilaza.
 
Serikali isijenge tawi la chuo cha utumishi wa umma - kama inataka kuwasaidia watu ijenge tawi la chuo cha SUA (umuhimu wa kada hii ktk maendeleo ya kilimo ni mkubwa sana hasa kuchochea ukuaji wa sekta binafsi, uchumi, uwekezaji na huduma za kitafiti kwa wakulima)

Tusiharibu fedha za umma
 
Kampasi ya Chuo cha Utumishi wa Umma tawi la kanda ya ziwa kitajengwa wilayani Chato, amethibitisha waziri wa utumishi wa umma George Mkuchika.

Kwa mujibu wa Mkuchika ni kuwa amejiridhisha kuwa Chato inazo sifa zote zinazoiwezesha kujenga chuo hicho ikiwemo ukubwa wa eneo unaoridhisha.

=======

TPSC KUJENGA KAMPASI CHATO KUKIDHI KIU KANDA YA ZIWA

CHUO cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kiko mbioni kujenga kampasi wilayani Chato, mkoani Geita itakayotoa fursa ya mafunzo kwa Watumishi wa Umma na wananchi wa Kanda ya Ziwa.

Akikagua eneo litakalojengwa Kampasi hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni mstaafu George Mkuchika alisema ameridhika na eneo lililotengwa kwani ni rafiki kwa usalama na utoaji wa elimu.

Kampasi itajengwa eneo la Rubambangwe lenye ekari 41.66 na itahudumia mikoa ya Geita, Mwanza, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Mara.

Waziri Mkuchika alisema Kanda ya Ziwa pekee ndiyo ilikuwa haijabahatika kuwa na Kampasi ya Chuo cha Utumishi wa Umma, hivyo fursa hii ni muafaka na itakuwa na manufaa kwa watumishi wa umma na wakazi wa eneo la Kanda hiyo.

Akizungumzia uamuzi wa kujenga Kampasi hiyo wilayani Chato, Mkuchika alifafanua kuwa halmashauri ya wilaya ya Chato imetoa kiwanja hicho bure tofauti na maeneo mengine ya Kanda ya Ziwa ambayo yangekigharimu chuo fedha nyingi kununua kiwanja.

Aliishukuru halmashauri kwa kutoa kiwanja na kumhimiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa hati kwani chuo kiko tayari kuanza ujenzi mapema iwezekavyo.

Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dk Emmanuel Shindika aliwathibitishia wakazi wa Kanda ya Ziwa kuwa fedha za kuanza ujenzi zimeshapatikana, hivyo kinachosubirikiwa ni hati.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Chato, ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Medard Kalemani alimtaka Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo kuwasilisha maombi ya kupatiwa umeme katika eneo hilo ili kuharakisha ukamilishaji wa ujenzi wa kampasi hiyo.

Akizungumzia eneo ambalo chuo kitajengwa, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel alisema ujenzi wa kampasi hiyo ukikamilika itakuwa ni chachu ya maendeleo kutokana na muingiliano wa watu kutoka maeneo mbalimbali watakaokuja kupata mafunzo na utavutia uwekezaji.
Kingewekwa mwanza
 
Hicho chuo kwa nini kisijengwe Mwanza ambayo ni katikati ya kanda ya ziwa kwa maana ya mikoa ya Mara, Simiyu, Shinyanga, Geita na Kagera? Huku kote ni kuipendelea Chato!
 
Back
Top Bottom