Geita. Mjamzito auawa kikatili kwa kuchinjwa, wauaji nao wauawa

Geita. Mjamzito auawa kikatili kwa kuchinjwa, wauaji nao wauawa

Kijana miaka 25 Tamaa ya Mali ya Nini siutafute zako mbona mda unao mzuri
 
Geita. Mwanamke mwenye ujauzito wa miezi saba aliyetambuliwa kwa jina la Renata Elias (27), ameuawa kikatili na mtoto wake wa kambo kwa kuchinjwa shingo huku chanzo kikidaiwa kuwa ni mgogoro wa kifamilia na tamaa ya mali.

Tukio hilo lililotokea usiku wa Februari 17, 2023 linadaiwa kufanywa na vijana wawili ambapo mmoja ni mtoto wa mume wa mwanamke huyo na kwamba baada ya kufanya mauaji hayo nao waliuawa na wananchi wenye hasira kali.

Katika tukio hilo, pia baba wa familia hiyo aliyetajwa kwa jina la Msafiri Renatus alijeruhiwa kwa kuchomwa kisu ubavuni na kichwani na amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Geita kwa matibabu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kwamba aliyetekeleza tukio hilo la kinyama anaitwa Jackson Msafiri (25) ambaye alikuwa na rafiki yake.

Mkuu wa wilaya ya Geita, Cornel Magembe ameitembelea familia iliyoathirika na tukio hilo kulaani vikali huku akitoa pole kwa familia na kuwashukuru wananchi kwa kuonyesha umoja uliofanikisha kumnusuru Msafiri na kumwahisha hospitali baada ya kujeruhiwa.

“Sisi kama serikali tumefika kuwapa pole kwenye jambo hili zito na baya ambalo kwa binadamu yeyote mwenye akili anaona ni tukio baya la kufedhesha utu wa binadamu watu tunatofautiana kwenye kufikiri na kutenda.

“Kilichofanywa ni kitendo kibaya sana, niseme tu nawashukuru wananchi kwa kujitokeza mliposikia na ushirikiano huu uendelee ili kudhibiti matukio ya aina hii,” amesema Magembe.

Mihayo Renatus ambaye ni kaka mkubwa wa Msafiri, amezungumzia tukio hilo akisema majira ya saa 2 usiku, mtoto mkubwa wa Msafiri akiwa na kijana mwenzake walifika nyumbani na kugonga kisha kufunguliwa geti na kuingia ndani kuangalia TV na baada ya muda mfupi walitekeleza mauaji hayo baada ya mwanamke huyo kuingia bafuni kuoga.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Safia Jongo hakupatikana kuzungumzia tukio hilo baada ya simu yake ya mkononi kutopokelewa.
Wasiojulikana wamejaa sana kanda ya ziwa.

Hawa wanaogombea mashamba mpaka wanauana ukimpa Milioni tano tu ananitoa roho mimi Rastaman
 
Geita. Mwanamke mwenye ujauzito wa miezi saba aliyetambuliwa kwa jina la Renata Elias (27), ameuawa kikatili na mtoto wake wa kambo kwa kuchinjwa shingo huku chanzo kikidaiwa kuwa ni mgogoro wa kifamilia na tamaa ya mali.

Tukio hilo lililotokea usiku wa Februari 17, 2023 linadaiwa kufanywa na vijana wawili ambapo mmoja ni mtoto wa mume wa mwanamke huyo na kwamba baada ya kufanya mauaji hayo nao waliuawa na wananchi wenye hasira kali.

Katika tukio hilo, pia baba wa familia hiyo aliyetajwa kwa jina la Msafiri Renatus alijeruhiwa kwa kuchomwa kisu ubavuni na kichwani na amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Geita kwa matibabu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kwamba aliyetekeleza tukio hilo la kinyama anaitwa Jackson Msafiri (25) ambaye alikuwa na rafiki yake.

Mkuu wa wilaya ya Geita, Cornel Magembe ameitembelea familia iliyoathirika na tukio hilo kulaani vikali huku akitoa pole kwa familia na kuwashukuru wananchi kwa kuonyesha umoja uliofanikisha kumnusuru Msafiri na kumwahisha hospitali baada ya kujeruhiwa.

“Sisi kama serikali tumefika kuwapa pole kwenye jambo hili zito na baya ambalo kwa binadamu yeyote mwenye akili anaona ni tukio baya la kufedhesha utu wa binadamu watu tunatofautiana kwenye kufikiri na kutenda.

“Kilichofanywa ni kitendo kibaya sana, niseme tu nawashukuru wananchi kwa kujitokeza mliposikia na ushirikiano huu uendelee ili kudhibiti matukio ya aina hii,” amesema Magembe.

Mihayo Renatus ambaye ni kaka mkubwa wa Msafiri, amezungumzia tukio hilo akisema majira ya saa 2 usiku, mtoto mkubwa wa Msafiri akiwa na kijana mwenzake walifika nyumbani na kugonga kisha kufunguliwa geti na kuingia ndani kuangalia TV na baada ya muda mfupi walitekeleza mauaji hayo baada ya mwanamke huyo kuingia bafuni kuoga.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Safia Jongo hakupatikana kuzungumzia tukio hilo baada ya simu yake ya mkononi kutopokelewa.
mtoto tangu anamiaka 5 anachunga mifugo anafikisha miaka 30 babake anachukua sehemu ya mali hiyo kuolea mke mwingine unadhani matokeo yake nn?
 
Kijana miaka 25 Tamaa ya Mali ya Nini siutafute zako mbona mda unao mzuri
Hizi familia na tamaduni za ki-tz mambo huanzia mbali.

Unakuta kuna uvumi kwenye famili na mtaa mzima kwamba Mama wa kambo ndiye aliyemuua Mama au alisababisha mama aachwe

Hivyo kunakuwa na mlundikano wa chuki za muda mrefu sana
 
Mzee hakumpa kijana wake usalama wa mali...
Huenda kijana yuko well aware walivyozitafuta pesa hizo kwa taabu labda na mama yake mzazi ila mzee kachukua binti anayelingana naye..

Who knows!!! Huenda huyu bi mdogo alimweka kati baba akawa boya na akajimilikisha mali zote..

Si bure..

Kuna somo hapa.
Kwahiyo unatakiwa uue
 
Labda huyo mzee mke wake wa kwanza amekufa, kwanini asioe tena wakati ana nguvu, au unataka aanze kuimba pambio la vijana wa hovyo, " KATAA NDOA"?
Wazee wengine wako hovyo sana. Unakuta familia ina maisha magumu sana badala ajijenge kwanza anakimbilia kuoa.
Vijana wamekuwa kwa shida na hata kile kilichopo Baba anachukua kutoa mahari.

Sasa unakuta vijana hawamwezi baba wanakimbilia kwa wanayemuonea.
 
Mali hizi hizi tunazokaa nazo kwa miaka isiyozidi 90 huku tukiwa na uwezo wa kuzifurahia si zaidi ya miaka 70?!!!!!! Dunia ina miaka billion kadhaa tangu iundwe na hata haijulikani kuna miaka mingapi kabla ya kuisha.

Ikifikia eneo hili, napenda sana nasaha za dini ya Kiislamu ya kutoihangaikia kupitiliza dunia na kwa nasaha hizi wamefanikiwa sana kuepusha vitendo kama hivi maeneo yao!
Madaraka ya Ubunge na Urais tu wa miaka mitano watu wanaalipuana Risasi na kubambikiziwa kesi za ubakaji mtu akaozee jela unazungumzia Mali za mtu maskini anazotegemea kukunja mkono kinywani??
 
Yaani habari ipo hovyo hovyo, haieleweki, huyu kamchinja huyu, huyu kamuua yule, mara mtoto wa kambo, mara baba sijui nini, khaa
 
Vijana wawili wa familia moja wakazi wa kitongoji cha Kilimahewa kata ya Ludete mkoani Geita, wameuwawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kumuua mama yao wa kambo Renatha Elias ambaye alikuwa mjamzito wa miezi saba kwa kumkata shingo.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Kilimahewa amesema vijana hao pia walimjeruhi baba yao mzazi kwa kumchoma na visu na kwa sasa yupo hospitali anapatiwa matibabu.
 
Habari haijakamilika kabisa maana chanzo change cha taarifa kinasema vijana hao walikuwa wanne na walliua mama yao wa kambo & hosegirl
 
Wazee wengine wako hovyo sana. Unakuta familia ina maisha magumu sana badala ajijenge kwanza anakimbilia kuoa.
Vijana wamekuwa kwa shida na hata kile kilichopo Baba anachukua kutoa mahari.

Sasa unakuta vijana hawamwezi baba wanakimbilia kwa wanayemuonea.
Umeongea point, sema kufikia kuua ni maamuzi yasio faa ila na sisi wazazi tujitafakari kuhusu mstakabari wa wanetu kuliko kujari nafasi zetu tu
 
Madaraka ya Ubunge na Urais tu wa miaka mitano watu wanaalipuana Risasi na kubambikiziwa kesi za ubakaji mtu akaozee jela unazungumzia Mali za mtu maskini anazotegemea kukunja mkono kinywani??
Ndo unafyeka watoto, wanawake!! Bado kuna namna nyingine ingeweza kufanyika zaidi ya kuchukua hizo nafsi.

Hao wanasiasa mi nimewatoa kitambo katika kundi la binadamu wa kawaida hivyo sishangai wakifanya lolote.......kuua albino n.k
 
Back
Top Bottom