Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Jesshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia Said Shabani (39) kwa kosa la kumuua Naomi James (17) mwanafunzi wa kidato cha pili, Shule ya Sekondari Kivukoni, mkazi wa Mtaa wa Nyatorotoro B, Kata ya Nyankumbu wilayani Geita Mkoani Geita kwa kumutuhumu kuiba kuni.
Akizungumza tukio hilo leo, Kamanda wa Polisi mkoani hapa (RPC) Henry Mwaibambe alisema tukio hilo lilitokea januari 18 mwaka huu katika msitu wa shamba la miti lililopo kata ya Nyankumbu ambapo marehemu alikuwa na wenzake wawili wakiwa wanatafuta kuni.
RPC Mwaibambe alisema wakati marehemu na wenzake wakiendelea kazi hiyo kwenye shamba linalomilikiwa na Said Shabani, ndipo mmiliki huyo alianza kuwakimbiza na bahati mbaya marehemu alianguka chini na kuanza kushambuliwa na mtuhumiwa kwa kitu chenye ncha kali na kusababisha kifo chake.
Akizungumza tukio hilo leo, Kamanda wa Polisi mkoani hapa (RPC) Henry Mwaibambe alisema tukio hilo lilitokea januari 18 mwaka huu katika msitu wa shamba la miti lililopo kata ya Nyankumbu ambapo marehemu alikuwa na wenzake wawili wakiwa wanatafuta kuni.
RPC Mwaibambe alisema wakati marehemu na wenzake wakiendelea kazi hiyo kwenye shamba linalomilikiwa na Said Shabani, ndipo mmiliki huyo alianza kuwakimbiza na bahati mbaya marehemu alianguka chini na kuanza kushambuliwa na mtuhumiwa kwa kitu chenye ncha kali na kusababisha kifo chake.