LGE2024 Geita: Utata majina ya wapiga kura, mkurugenzi atoa ufafanuzi
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mpiga kura Mtaa wa Mwatulole katika kituo cha kupigia kura Mwatulole Center ambaye awali alilalamika kutoona jina lake, hatimaye amekiri mbele ya msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Geita Mjini, Yefred Mnyenzi kuwa jina lake limeonekana na ametimiza haki yake.
 
Baadhi ya Wananchi na Wapiga Kura wa Kituo cha Kupigia Kura Mwatulole, Halmashauri ya Mji wa Geita wamelalamikia kuhusu majina yao kutoonekana hali iliyowafanya kutokupiga kura, wametoa malalamiko hayo mbele ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Yefred Miyenzi ambaye ndiye Msimamizi wa Kituo

Akizungumzia hali hiyo, Miyenzi amesema “Inawezekana kuna walioangalia harakaharaka, wakihitaji usaidizi tupo hapa kuwasaidia, maoni ya kuboresha kuwa tupange kwa herufi tumeyachukua kwa ajili ya Uchaguzi ujao. Hakuna sintofahamu yoyote.”

 
Mkurugenzi hana shida na wapiga kura halisi tayari ana majina ya wanafunzi mfukoni anasubiri kituo kifungwe amalize kazi
 
Mwananchi mmoja kutoka kata ya Buhala halmashauri ya Mji wa Geita, aliyejitokeza kupiga kura kwenye kituo cha Mwatulole alilalamika awali kwamba jina lake halikuwepo kwenye orodha ya wapiga kura.

Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa haraka uliofanywa na maafisa wa uchaguzi, jina lake lilionekana kwenye orodha rasmi.

Tukio hilo limesababisha sintofahamu ya muda mfupi, ambapo mwananchi huyo ameomba radhi kwa msimamizi wa uchaguzi wa halmashauri ya Mji wa Geita kwa lawama alizotoa kabla ya kufahamu ukweli wa jambo hilo.

Msimamizi wa uchaguzi ameeleza kuwa changamoto kama hizi hutokea mara chache kutokana na baadhi ya wapiga kura kushindwa kufuatilia taarifa zao za usajili kwa wakati, huku akibainisha kuwa Tume ya uchaguzi imejipanga kuhakikisha kila mpiga kura aliyejiandikisha anapata haki yake bila vikwazo.

Mwananchi huyo amemaliza kwa kuwataka wananchi wengine kuhakikisha wanakagua majina yao mapema kwenye orodha za wapiga kura ili kuepuka sintofahamu kama hiyo siku ya uchaguzi.
 
Mwananchi mmoja kutoka kata ya Buhala halmashauri ya Mji wa Geita, aliyejitokeza kupiga kura kwenye kituo cha Mwatulole alilalamika awali kwamba jina lake halikuwepo kwenye orodha ya wapiga kura.

Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa haraka uliofanywa na maafisa wa uchaguzi, jina lake lilionekana kwenye orodha rasmi.

Tukio hilo limesababisha sintofahamu ya muda mfupi, ambapo mwananchi huyo ameomba radhi kwa msimamizi wa uchaguzi wa halmashauri ya Mji wa Geita kwa lawama alizotoa kabla ya kufahamu ukweli wa jambo hilo.

Msimamizi wa uchaguzi ameeleza kuwa changamoto kama hizi hutokea mara chache kutokana na baadhi ya wapiga kura kushindwa kufuatilia taarifa zao za usajili kwa wakati, huku akibainisha kuwa Tume ya uchaguzi imejipanga kuhakikisha kila mpiga kura aliyejiandikisha anapata haki yake bila vikwazo.
View: https://x.com/Jambotv_/status/1861750282520068433?s=19
 
Wananchi wawili Wakazi wa Mtaa wa Mwatulole Kata ya Buhalahala Halmashauri ya Mji Geita Mkoani Geita wamemlalamikia Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi Halmashauri ya Mji Geita , Yefred Myenzi mara baada ya kufika kituo cha Mwatulole Senta na kushindwa kuona majina yao

Yefred Myenzi alimtaka Mwananchi huyo kuangalia kwa makini jina lake ambapo baadaye aliliona huku akiswma mwingine hakujiandikisha katika kituo hicho lakini amefika kupiga kura huku akisema hali iko shwari katika vituo vyote vya kupigia kura.

 
Back
Top Bottom