Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 182,097
- 1,099,383
Sielewi kwanini mkuu wa wilaya ya kinondoni hatumii rav4Hivi hawa watu, wakitumia magari ya bei za kawaida ila imara, je nini kitatokea? Mbona naona kwa nchi inayojikongoja ingekuwa vema kutumia magari imara ya bei rafiki.
Ili pesa nyingi, zielekezwe kwenye huduma za kijamii hasa mikoa iliyo nyuma kimaendeleo.
Mkoa mmoja tu, unakuta wakuu wa wilaya wanatumia 840m kwa magari tu, je uki-extraplotate nchi nzima ni pesa kiasi gani inaunguzwa kwenye magari tu- zaidi ya 20b. Halafu magari hayo hununuliwa karibu kila baada mwaka mmoja, yaani baada ya miaka miwili au mitatu, ma DC hao hao watapata magari mengine mapya bila kuuliza yale ya zamani yalikwenda wapi.Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela amekabidhi magari matatu mapya kwa Wakuu wa Wilaya ya Geita, Mbogwe na Nyang’hwale yenye thamani ya zaidi ya Tsh. milioni 840.
Akikabidhi magari hayo katika Kata ya Bombambili Halmashauri ya Mji wa Geita, Shigela amewataka Wakuu wa Wilaya kuyatumia vizuri magari hayo ambayo yamenunuliwa kwa fedha za Serikali sambamba na kuwataka Madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani.
“Shukrani kwa Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kuwezesha mazingira ya Wafanyakazi na Ofisi ya Viongozi ambao wana jukumu la kumsaidia katika ngazi za Wilaya na Mkoa, tunamshukuru sana Mh. Rais kwa sababu fedha ambazo zimeletwa zaidi ya Tsh. milioni 840 ni fedha nyingi ambazo Mh. Rais ameona kuna haja ya kuleta fedha tununue magari”
Shigela amesema Wakuu wa Wilaya walikuwa wakihangaika kupata usafiri wa kwenda kutatua kero za Wananchi na kusema magari hayo yatakuwa mkombozi kwa Viongozi hao.
MillardAyoUPDATES
Mama yenu alielekeza kula urefu wa kamba sasa wanakula kote koteHivi hawa watu, wakitumia magari ya bei za kawaida ila imara, je nini kitatokea? Mbona naona kwa nchi inayojikongoja ingekuwa vema kutumia magari imara ya bei rafiki.
Ili pesa nyingi, zielekezwe kwenye huduma za kijamii hasa mikoa iliyo nyuma kimaendeleo.
Inasikitisha sana, Mtanzania wa kawaida hayajui haya. Yeye bora kala mlo mmoja, kalala basi. Kila siku nasema humu, kuanzia kodi, mikataba na mikopo vyote hivyo, ni kwaajili ya maisha yao ya anasa. Wala si kwa maisha ya Mtanzania. Ushahidi huo hapo!Bajeti ya magari ya viongozi na viburudisho vya viongozi ni kubwa kuliko ya baadhi ya wizara muhimu zinazogusa maisha ya Watanzania wengi. Hii tu inatosha kukupa taswira juu ya taifa tulilonalo; na jamii tunayojaribu kuijenga!
SAD 😭
View attachment 3041338
View attachment 3041339
Na hayo watauziwa kwa madai ya kupunguza gharama za matumizi.Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela amekabidhi magari matatu mapya kwa Wakuu wa Wilaya ya Geita, Mbogwe na Nyang’hwale yenye thamani ya zaidi ya Tsh. milioni 840.
Akikabidhi magari hayo katika Kata ya Bombambili Halmashauri ya Mji wa Geita, Shigela amewataka Wakuu wa Wilaya kuyatumia vizuri magari hayo ambayo yamenunuliwa kwa fedha za Serikali sambamba na kuwataka Madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani.
“Shukrani kwa Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kuwezesha mazingira ya Wafanyakazi na Ofisi ya Viongozi ambao wana jukumu la kumsaidia katika ngazi za Wilaya na Mkoa, tunamshukuru sana Mh. Rais kwa sababu fedha ambazo zimeletwa zaidi ya Tsh. milioni 840 ni fedha nyingi ambazo Mh. Rais ameona kuna haja ya kuleta fedha tununue magari”
Shigela amesema Wakuu wa Wilaya walikuwa wakihangaika kupata usafiri wa kwenda kutatua kero za Wananchi na kusema magari hayo yatakuwa mkombozi kwa Viongozi hao.
MillardAyoUPDATES
Mno mnoMama anaupiga mwingi.
Ela ya kujengea zahanati ya kisasaSio Geita tuu Bali Mikoa yote wanagawiwa.
Land cruiser Prado TX Moja ni 280Mln
Hizo wanauziana wao kwa wao tena kwa bei ya kutupa!Gari za zamani zimekwenda wapi ?