Gen Z wa Tanzania wapewe ajira maana ukosefu wa ajira ni chanzo cha maandamano tunayoshuhudia Kenya na sasa Uganda

Gen Z wa Tanzania wapewe ajira maana ukosefu wa ajira ni chanzo cha maandamano tunayoshuhudia Kenya na sasa Uganda

Utajiajirije mwenyewe bila mtaji wala uzoefu Madam?!
Ndo maana ushauri wangu ni kwa wazee wote walioko serikalini, watoke wakajiajiri ili waachie vijana nao waajiriwe na serikali.
Lakini utashangaa wazee wengine licha ya kufikia umri wa kustaafu, bado wanaomba waongezewe muda au wafanye kazi kwa mkataba huko huko serikalini!
Kwani shule ulienda kusomea ujinga?

Mwili na na fikra za binadam hupata uzoefu kwa kutenda siyo kuwaza tu.
 
Wanajitahidi vitisho na drama zao kuogopesha. Wasubiri vijana wetu wamejifunza Bangladesh
Hujatishwa unaogopa, je ukitishwa?

Mnajidanganya sana akili zenu, kafufueni mashamba ya babu zenu siyo mnarundikana mijini tu. Mambo yapo kwa Bashe.
 
Utajiajirije mwenyewe bila mtaji wala uzoefu Madam?!
Ndo maana ushauri wangu ni kwa wazee wote walioko serikalini, watoke wakajiajiri ili waachie vijana nao waajiriwe na serikali.
Lakini utashangaa wazee wengine licha ya kufikia umri wa kustaafu, bado wanaomba waongezewe muda au wafanye kazi kwa mkataba huko huko serikalini!
Unashangaa nini na "umri" ni namba tu?

Badala ya kushangaa shangaa kanunuwe karanga uchemshe na chumvi uuze mitaani, ujipatie uzoefu wa biashara.

Kumbuka; nimetaja karanga kama kigezo tu, inaweza kuwa chochote.
 
Tembelea mkoa wa Pwani uone viwanda vipya, kila sehemu.

Kwani sekta binafsi lazima uajiriwe, kwanini hujiajiri wewe mwenyewe?

SG
Akijiajiri mwenyewe hawezi kujiongoza, kujitawala na hana ubunifu wa kujiwekea Mikakati ya baadaye. Anataka aajiriwe halafu ajipumzikie(Atege kazi) lakini awe active sana kudai mshahara tena kwa nguvu.
 
hiyo serikali itaajiri vijana wangapi katika nchi hii?
Yeah. Idadi ya vijana waliopo na wenye sifa stahiki kuajiriwa serikalini ni kubwa sana i.e. ni wengi mno kuzidi idadi ya nafasi za ajira zilizopo/zinazopatikana. Kwa hiyo LAZIMA watakuwepo tuu watakaokosa ajira Serikalini. Lakini ajira kama ajira, zimejaa tele na hazijatoshelezwa.
Hili vijana hawalikubali na wakiambiwa wajiajiri -sekta binafsi hususan ktk kilimo wanang'ang'ania mijini.
 
🤣🤣🤣 Tz hii au ip sasa ww Gen z unataka utuambie ss wauza chps tuache then tuandamane kuwapigania majitu yaliyo enda kupata elimu ya kukaririshwa kwl nawapa pole sana mmeambiwa mkalime kuna toyo na bajaj sasa we unataka kwenda BOT na wakat umesoma komb mama (HKL)
Ni ukweli kabisa 👆 👆 japo mchungu - unauma..Watakapozinduka watakuta imeenda hiyo.
 
Wadau Asalam aleykum.

Wanasema mwenzako akinyolewa zako tia maji.

Nawashauri viongozi wangu mlioko kwenye vyombo vya kutunga sera, mfanye kuwaajiri vijana walioko mtaani wenye ujuzi na wasio na ujuzi pia watafutiwe kazi za kufanya.

Hii itawafanya kuwa bize na hivyo kuwasahaulisha na ugumu wa maisha wanaokabiliana nao sasa.

Viongozi wangu, msijiamini kupitiliza kwamba nyinyi mna mifumo imara kuliko huko kunakofuka moto sasa.

Wanasema mwenye njaa mara zote huwa na hasira.

Pia wanasema kama huna kazi ya kufanya, basi chochote kinachokuja mbele yako unaweza kujikuta unakifanya! Shetani huwatumia sana wasio na kazi kutimiza agenda zake ovu.

Maandamano ni kama ugonjwa wa kuambukiza. Mara nyingi nchi nyingi zenye matatizo kama vile Libya, Tunisia, Misri, Sudan, na sasa Kenya na Uganda, maandamano huwa yanaanza kidogo kidogo na baadaye kusambaa nchi nzima!

Kama hali ikiendelea hivi ilivyo, basi tusishangae kuwaona Gen Z wetu nao wakiingia barabarani kuandamana.
Naomba kuwasilisha.
Waliandaliwa kuto kuhoji, endapo maandamano yakitokea jibu lake ni madhara ya kuto kuhoji na kuto sikilizwa, (silent society), the question is how long should people keep silent
 
Tembelea www.ajira.go.tz
Hakuna nchi iliyo ajili Wananchi wote
Ipo.
Kwa mfano nchi ya Tanzania (Popn. 62mil.+ )hakuna Mwananchi yeyote anayeshindwa kupata riziki yake ya kila siku kama akijishughulisha. Kumbuka na Kuzingatia kwamba hatupati mahitaji yetu(Riziki zetu)ss Watanzania kwa kupewa na Serikali; HAKUNA- Huo ndo ukweli halisi. Usidanganywe na kikundi cha wachache sana wanaosema eti wamesoma na wanataka waajiriwe na Serikali - wameshasahau kwamba hawakuwekeana Mkataba na Serikali kwamba akimaliza masomo Serikali itamwajiri. Wakiambiwa wajiajiri Sekta binafsi wanatishia kuandamana eti wao ni Gen. Z. Kwa maneno mengine ni kwamba Ajira ya Gen.Z waliojipa wao wenyewe ni kulalamika, kuitishia Serikali kwamba wataandamana na kuwaghilibu (kushawishi/kudanganya) vijana wenzao ambao wanajishughulisha ili wawaunge mkono kwenye ujinga huo.
Wanadhani ajira zipo tuu ila Serikali kwa kiburi na ukatili inawanyima.
Wakitangaziwa Ajira za siri huko Urussi, Israeli, Ukraine, Palestina, Wagner PMC, N. Korea wanazuga eti hawajaziona. Ni watata kwel-kweli hawa jamaa wanaojnasibisha kuwa Gen. Z. Sifa za Gen.Z zipo ila sio za hawa waBongo.
Dah! Wanashindwa basi hata kujiajiri kwenye ile Sekta inayopigwa vita na Mh. RC na hivi karibuni wanategemea kulamba 36 mil. chap.:AnimeLick:
 
Waliandaliwa kuto kuhoji, endapo maandamano yakitokea jibu lake ni madhara ya kuto kuhoji na kuto sikilizwa, (silent society), the question is how long should people keep silent
U go while the going is good.
 
Ipo.
Kwa mfano nchi ya Tanzania (Popn. 62mil.+ )hakuna Mwananchi yeyote anayeshindwa kupata riziki yake ya kila siku kama akijishughulisha. Kumbuka na Kuzingatia kwamba hatupati mahitaji yetu(Riziki zetu)ss Watanzania kwa kupewa na Serikali; HAKUNA- Huo ndo ukweli halisi. Usidanganywe na kikundi cha wachache sana wanaosema eti wamesoma na wanataka waajiriwe na Serikali - wameshasahau kwamba hawakuwekeana Mkataba na Serikali kwamba akimaliza masomo Serikali itamwajiri. Wakiambiwa wajiajiri Sekta binafsi wanatishia kuandamana eti wao ni Gen. Z. Kwa maneno mengine ni kwamba Ajira ya Gen.Z waliojipa wao wenyewe ni kulalamika, kuitishia Serikali kwamba wataandamana na kuwaghilibu (kushawishi/kudanganya) vijana wenzao ambao wanajishughulisha ili wawaunge mkono kwenye ujinga huo.
Wanadhani ajira zipo tuu ila Serikali kwa kiburi na ukatili inawanyima.
Wakitangaziwa Ajira za siri huko Urussi, Israeli, Ukraine, Palestina, Wagner PMC, N. Korea wanazuga eti hawajaziona. Ni watata kwel-kweli hawa jamaa wanaojnasibisha kuwa Gen. Z. Sifa za Gen.Z zipo ila sio za hawa waBongo.
Dah! Wanashindwa basi hata kujiajiri kwenye ile Sekta inayopigwa vita na Mh. RC na hivi karibuni wanategemea kulamba 36 mil. chap.:AnimeLick:
Taka taka izi kaandamane mwenyewe na ujinga wenu
 
Wadau Asalam aleykum.

Wanasema mwenzako akinyolewa zako tia maji.

Nawashauri viongozi wangu mlioko kwenye vyombo vya kutunga sera, mfanye kuwaajiri vijana walioko mtaani wenye ujuzi na wasio na ujuzi pia watafutiwe kazi za kufanya.

Hii itawafanya kuwa bize na hivyo kuwasahaulisha na ugumu wa maisha wanaokabiliana nao sasa.

Viongozi wangu, msijiamini kupitiliza kwamba nyinyi mna mifumo imara kuliko huko kunakofuka moto sasa.

Wanasema mwenye njaa mara zote huwa na hasira.

Pia wanasema kama huna kazi ya kufanya, basi chochote kinachokuja mbele yako unaweza kujikuta unakifanya! Shetani huwatumia sana wasio na kazi kutimiza agenda zake ovu.

Maandamano ni kama ugonjwa wa kuambukiza. Mara nyingi nchi nyingi zenye matatizo kama vile Libya, Tunisia, Misri, Sudan, na sasa Kenya na Uganda, maandamano huwa yanaanza kidogo kidogo na baadaye kusambaa nchi nzima!

Kama hali ikiendelea hivi ilivyo, basi tusishangae kuwaona Gen Z wetu nao wakiingia barabarani kuandamana.
Naomba kuwasilisha.
Maisha ya uhakika ni ya kujihangaikia, serikali inatengeneza mazingira ya kiuchumi lakini kujiajiri ni ubunifu wa mtu binafsi.
 
Back
Top Bottom