Tetesi: Genious wa kiafrika Ulaya hufanywa machizi kwa kuchomwa sindano wakibainika

ni kweli mkuu. Basi kwa nini sisi waafrika tunawapenda hao ngozi nyeupe? Tena tunawapapatikia na kuwaheshimu. Kwa nini sasa wanatudharau kwa sisi kuwanyenyekea
 
ni kweli mkuu. Basi kwa nini sisi waafrika tunawapenda hao ngozi nyeupe? Tena tunawapapatikia na kuwaheshimu. Kwa nini sasa wanatudharau kwa sisi kuwanyenyekea
Mpendwa, Tujifunze kuwatafuta wazee wa zamani na kuwa tunakaa nao kuwasikiliza Hekima zao na busara wanayo yasema.. tuajifunza mambo yaa maana!! ila Kizazi cha sasa ni Fasta life !!
Hata wewe huko ulipo wapo wazee wakidhungu ufany ukaribu nao You will learn kwa uzoefu wao!!

Jindal Singh Ntakitafuta kitabu... Shukran !!
 
Yuko wapi siku hizi huyu kaka,maana niliishia kash kash na mkewe ikaweje...?
Ishu ilimpa stress za kufamtu akashuka viwango na kesi ikaamuliwa wagawane mali pamoja na kumlipa mwanamke fidia kubwa
 

Mkuu, kama ni tetesi tu na hakuna ushahidi basi hakuna haja ya kuwa na wasiwasi.

Kwa kuwa Ulaya si kwa mwakfrika ukiondoa wale walokuwa watumwa mwafrika mwingine hana umuhimu isipokuwa kama atakuwa mpole na amekubalika khasa mbele ya jamii wa wazungu.

Nikisema amekubalika namaanisha mzungu anakufahamu kiundani wewe ni nani, unatokea wapi, ukoo wenu, uwezo wa kiakili na utajiri, basi atakuheshimu na kuwa rafiki yako milele.

Wapo wahandisi, na wataalam wengi tu kutoka Afrika huko Ughaibuni lakini wanaendelea na maisha.

Hao unaowasema zitakuwa ni story tu za mitaani maana hata pale UK kuna mji mmoja yupo mtanzania ambae anashabihiana na hao unaowasema ila yeye analala mitaani kabisa yaani ni chizi lakini anangaliwa vizuri kwa malazi, chakula na dawa.

Hivyo waafrika tugangamale fanya kazi kwa bidii hasa kama hujasoma sana na utatoka tu, tusahau mambo ya njia za mkato na tukishindwa tunamtafuta mchawi.
 

Mkuu,

Marekani na Urusi walikubaliana mwaka 1962, Mrusi atoe silaha zake za nyuklia hapo Cuba, na Marekani atoe Uturuki na Italia. US Navy walikizunguka kisiwa cha Cuba na Rais Kennedy alikuwa tayari kupigana vita na Mrusi. Baada ya mwezi mmoja, walikubaliana , isingekuwa hivyo, ingekuwa vita vya tatu vya dunia.

Hao jamaa uliowataja nyuma itakuwa wamezidiwa tu na maisha au ni wagonjwa. Kuwa na elimu ya juu na kazi nzuri haihusiki na hali ya afya ya binadamu.

Kuna wasomi wa hali ya juu kama Waziri Mkuu wa UK, Mama Thatcher, anaamka asubuhi anajikuta ubongo haukumbuki kitu. Ugonjwa huo wa Alzheimer's pia ukampata mbabe, Rais Ronald Reagan wa Marekani.

Kuhusu Tiger Woods, alipenda mchepuko sana. Ukikamatwa na mchepuko Ulaya au Marekani, mke anapewa pesa nyingi sana. Ndiyo maana wajanja wanakuwa na makubaliano ya ugawaji wa mali kabla ya ndoa (pre-nuptial agreement).

Paul McCartney wa Beatles alilizwa sana alipoachana na mke wake wa pili, ($48 million) ila sijui sababu yao ya kuachana.

Marekani na UK siyo sehemu nzuri ya kuachana na mkeo kama ni tajiri sana. Matajiri wa Urusi wanaoishi London pia wanalizwa sana wakikamatwa na mchepuko au wakiachana kwa sababu yoyote.

Abramovich inasemekana kalipa $300 million.
Tiger Woods, amelipa $100 million.

Siasa ya Marekani ipo wazi sana kuhusu issue ya mafuta. Rais Carter alishasema bungeni kuwa watafanya kitu chochote kuweza kuwa na mafuta ya kutosha kuendesha uchumi wa Marekani. (Matter of national security). Iran alibanwa na vikwazo vya uchumi mpaka serikali yao ikakubali makampuni ya mafuta ya Marekani yaruhusiwe kusaka mafuta kama zamani. BP ilianza kama kampuni kubwa Iran siyo UK. Shah Reza alikuwa kibaka wa Marekani na UK.
Iran pia ina natural gas, 1 trillion cubic feet, ya pili baada Urusi.

Korea ya Kaskazini bila ya kuwa mpakani mwa China na kumiliki mabomu ya nyuklia, CIA wangempindua Kim Il Sung siku nyingi. Mjukuu wake asingekuwa anaendesha nchi leo.
 
sasa leo tunabaguana wenyewe kwa wenyewe Waafrica,...
msouth anajiona bora kuliko mnigeria we unategemea wazungu watatuheshimu sisi,..
ila chunguzsa mzungu akikutana na mzungu mwenzie popote pale duniani
wanapendana na kujua kapata ndugu,...
leo watz wananyanyaswa na wasouth unategemea vnini hapo ndugu,....
sisi watz ni ndugu sisi kwa sisi tu,...
wazungu always wanatafuta kutukandamiza Africans tuwe vinferior all days
 
Hizo ni hisia tu na kutokujiamini.

Mi siamini katika hilo na kama ni kweli linafanyika basi kufanyika kwingine lakini sio Sverige
 

Upo sahihi Mkuu.

Waafrika hawana umoja. Viongozi wao wengi wanawakandamiza wananchi wao. Haki za binadamu haziheshimiwi. Wapinzani hawana sauti, wamebanwa koo.

Zaidi ya miaka 50 tangu wakoloni waondoke Afrika, raia wake hawawezi kuvuka mipaka waliochorewa na wakoloni, ili kuwatawala kirahisi, bila ya vizuizi. Lakini, Mkoloni akifika mpakani, anapita kirahisi.

Ndani ya EU, wana matatizo yao mengi lakini wanakaa na kujaribu kutatua bila ya kuharibu umoja wao. Wapolish wanadunda London kama kwao, Waromania wanaona kama wameshinda bahati nasibu ya maisha kukubaliwa kuwa mwanachama wa EU. Kuna nchi nje ya EU kama Switzerland na Norway, raia wao wanaruhusiwa kufanya kazi ndani ya EU. Wananchi wa Denmark wanafanya kazi Sweden, jioni wanarudi kwao Denmark.

Sasa, linganisha na mwendo wa kobe wa maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Viongozi wenyewe ni kina Nkurunziza, Museveni na Kagame. Wanahiari wananchi wao wafe kuliko kung'atuka.

Hapo AU, wameshindwa hata kujichangishia pesa za kujenga Makao Makuu yao, Ethiopia, mpaka China kawapa msaada.

Wanawatukana wakoloni kwenye mikutano yao halafu wanapanda ndege na familia yao kwenda kufanya shopping, kuomba misaada na kufanya matibabu ulaya.

Afrika tutasubiri sana maendeleo.
 
Hahahah rafiki yangu Copenhagen DN najua wasiwasi wako kwamba na wewe ipo siku watakufanya chizi aaagrrr

Nawaunga mkono watoa hoja wa mwamzo pia sio kweli kuna magonjwa mengi yatakua yanahusika hapo ondoa wasiwasi brother
 
mkuu tatizo ni kukosa uzalendo,...waafrika hatuna uzalendo na bara letu
na hii imeshajengeka hadi vizazi vyetu vijavyo kuwa waafrika hatujiwezi,..
tamaa za madaraka kwa viongoz wa afrika ni kutokana na wizi wa rasilimali mkuu,..
mimi ntalala usingizi JPM akiwa rais,...j.kikwete
sasa huu siupuzi mkuu,.kwahiyo mtu anaamua2 kuwa hawaachii dola hadi rais awe mtu flani wa ccm,..
huu wizi ndo unawafanya wawe defensive sana mkuu,...
african leaders they are all the same wezi,.wote wezi2,...
yana tamaa na mali za wananchi kama wataishi milele
wakaTI MAJORITY WANAPATA DHIKI NA HADHA,viriba tumbo,njaa,wanakufa hovyo, wakati Mungu kawapa utajili sana tu waafrika,...mkuu haya mambo yanaumiza sana roho
kama umepata akili ya kutambua haya mambo
maana siwote wenye kuelewa haya
 
W
Wapi ndege ya malaysia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…