Genius Hayati Magufuli Hakuongeza Mshahara ila Maisha yaliendana na Kipato

Genius Hayati Magufuli Hakuongeza Mshahara ila Maisha yaliendana na Kipato

Hata yeye alikuwa mwizi tu,kama huyu,wapo watu waliumia,makampuni yalifungwa,watu walibambikiwa kesi Ili wanunue uhuru wao,
Hilo la watu kubabikiawa kesi na kununua uhuru wao lilikuwa na bandwidth
Kuna kanda haikuguswa kabisa na hizo mishe , ndo hao wanamlilia kila siku.
 
Binafsi Naona kilichoongezwa kinatosha, na serikali ya awamu ya sita inajitahidi, mambo mazuri yanakuja, tusimtukane mpishi kabla jua jalijafika machweo, mama atafanya makubwa hamtaamini.

Mama kapandisha madaraja na nyongeza juu lakini bado tunamuona mbaya,binadamu Ni watu wabaya sana hata uwapikie moyo wako wale bado watadai chumvi imepelea.
 
Kwa ufahamu wangu, JPM hakufanikiwa kabisa kumanage inflation, zaidi sana vitu kama sukari, mafuta ya kula n.k vilipanda bei mapema sana ktk uongozi wake na havikuwahi kushuka bei. Kwa maoni yangu, JPM alikuwa tu na uthubutu lkn kusimamia uchumi vizuri hata kwake ilikuwa shida. JK ndio ambaye aliweza sana kisimamia uchumi
 
Ukweli ni kwamba watu wengi walimkubali JPM kwa uthubutu,lakin ndo hivyo ameshafariki ,hatuwez kupaki bus tukawa tunalialia lazima nchi iende .. tumempata mama twende nae nchi isonge mbele tujikwamue tulipo,Angekuwa hai tungesema baba rud uendeleze kijiti ,lakin ndo amefariki tuutumie mpini tulionao tutapata mavuno mbele ya safari Inshaallah
Tatizo mama anampiga vijembe mtanguliza wake kila kukicha, wakati JPM ndiye aliyemtoa huko uswekeni. Kama vile Nape na Makamba wanavyo mnanga JPM.
 
Kuna ambaye bado anabisha tu kua Hayati JPM alikua ni Genius? Kwamba Hayati JPM alikua ni Mteule wa Mungu aloletwa Kuwainua Watanzania !!.?

Watumishi wa Umma hao , walimu kama nawaona , Mapolisi kama nawaona ( Hawa watu wawili Wana Maisha ya tabu sana ) Lakini ndio wa kwanza kuimba nyimbo za mapambio Kila kukicha !!

Nirudi kwenye Mada, Niliposikia Vifujo na mayowe kisa Rais Samia kasema 23% nilicheka sanaaaa, nikawaonea huruma, pasipo kujali ni kiasi gan Cha Pesa kingeongezwa,

Swali pekee nilojiuliza lilikua ni hii[emoji116]

[emoji117]Je hiyo 23% itapambana na HII INFLATION TUNAYOISHUDIA ?

Petrol Juu, Diesel Juu, Mafuta ya Taa Juu , Mafuta ya Kupikia Juu, Gas Juu sana, Nauli juu, Vyakula ndo usiguse juuu sana na Kuna Njaaa inakuja Iko njiani haijawah shuhudiwa ( endeleen kuruhusu wakulima wauze nje ) , Sabuni Juu, Sukari juuu sana Umeme Juu,

Nchi hiii Kila kitu kipo juuu Kwa Sasa na vinaendelea kua Juu !!

Haya Sasa Nyongeza hiyo hapo, mnasemaje ??. Mmeacha kubweka ?
bado mna la kusema juu ya Chuma JPM??..

HIi Nchi kama lilivyo Bara la Afrika Kwa ujumla, tunakoswa viongozi wenye Maono, watu ni viongozi sababu wanataka waonekane kwenye Rununga, wapigiwe Saluti, Magari ya bure ,Majumba ya bure, Walindwe ,na watumie Pesa za Umma Kwa faida za familia zao na matumbo Yao wenyewe .

katika Nyakati za Sasa, Kwa hakika, Kiongozi aina ya Hayati MAGUFULI ni mwibaa mchungu Kwa watu wachache lakini Mwenye Maana kubwa Kwa Watanzania walio Wengi !!

Hii Nchi inahitaji Viongozi wenye Maono, Akili zilizokomaa na Pevu, watu wazalendo wenye Kupenda na wapo tayari kuifia nchi Kwa faida ya Wananchi wenyewe kama alivyokua JPM.

Sahizi Nchi Haina hata Bei Elekezi, wafanyabiashara wanajiamulia tu wanavyotaka, MAKODI MENGI YA KIJINGA bahati mbaya MAKODI yenyewe yanadeal na watu wakawaida, Wafanyabiashara wanaambiwa ni wawekezaji wazuri wapewe misamaha ya Kodi !!

Kuanzia Leo mkome kabisa Kumfananisha Hayati JPM , Chuma, Genius , Akili kubwa na Hawa mbumbumbu wenu wa Sasa wasotulia nchini Kila kukicha ni Nje ya Nchi utadhan Nchi inajengwa na Mabeberu !!.

Hata Ukope kiasi gani, kama Hauna Upeo, Maono , Usimamizi na Uadilifu utawaumiza Watanzania tu!!.

Hivi bila JPM Leo hii kweli hata haya machache makubwa ambayo tunayaona kama Alana za uongozi wake, Yangekuwepo?

Watumishi wa Umma nanyie acheni Ujinga, kutegemea Mshahara , achen kua na Akili mgando , wekezeni ,muongezee mzunguko wa Pesa kwenye mifuko yenu !!....bila Ivo mtalia sana ,mtalia sanaaa na ndo kwanza Vita ya ' Ukraine na COVID-19 ' kama ilivyo kisingizo Cha mbumbumbu wetu ,ndo kwanza vinaanza !!.

JPM aliwezaje ?
Huyu aliyeacha nchi haina hata shilingi, wafanyakazi hoi,wakulima hoi na wafanyabiashala hoi kabisa U'Genius kaupataje na kutoka wapi!!?
 
JPM asifiwe ujenzi na ndege.
Jk asifiwe diplomasia na maslahi bora kwa watumishi wake
Mkapa asifiwe miundombinu ya uchumi
Nyerere asifiwe uhuru na kuiunganisha TZ
Mwinyi asifiwe kututoa kwenye pure ujamaa.
 
Mshapata la kusema sasa,kama ni hivyo basi jk ndiyo genius kuzidi wote coz aliongeza miaka yote 10 na bei ya bidhaa ilikuwa cheap
 
Mwaka mmoja wa uongozi hakuna cha maana zaidi ya kuzurura nje ya nchi na kuomba mikopo ya kujenga vyoo. Nani kama mama na bado
 
Ila maza kachemka Sana[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]mba mba mba nyingiii ,buree kabisaaa

Nimeamua rasmi kua mjasiriamali ,utumishi nawaachia wao wanaolipana maposho mpk ya mahawara zao
Na matoto yakifeli wasitulaumu
 
Back
Top Bottom