Geor Davie ni nani?

Geor Davie ni nani?

Michango ya Kondoo afu walivyo viazi wana shangilia kabisaaa


Sent from my iPad Air using JamiiForums
 
Kwa namn hii mnafikiri kweli akili ya watanzania imekomaa kuweza kutoichaagua ccm tena?
 
attachment.php


ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie' wa Kanisa la Geordavie Ministry ‘Ngurumo ya Upako' lililoko jijini Arusha na Kawe, Dar hivi karibuni alifanya mkutano mkubwa na kutikisa nchi kwa kuwa na magari ya kifahari na ndege aina ya helikopta ‘chopa' iliyokuwa ikirandaranda juu ya anga kulinda usalama wake, Uwazi lina ushuhuda wa kutosha.

attachment.php



Katika mkutano huo uliofanyika Karatu mkoani Manyara, mwandishi wetu alishuhudia msafara wa Geordavie ambaye hutoa huduma ya uponyaji kwa njia za miujiza, ukiwavutia watu wengi kwa kuwa ulikuwa na ulinzi mkali ambao haujawahi kutokea.

GEORDAVIE1.jpg

Mbali ya kuwa na chopa iliyokuwa ikiimarisha ulinzi ambayo ameinunua hivi karibuni, askofu huyo alikuwa na msururu wa magari yenye thamani kubwa yanayomfanya kutajwa kuwa tajiri kuliko maaskofu wengine wanatoa huduma katika makanisa ya kiroho Tanzania.

Akiwa Karatu, mbali na ulinzi binafsi, Geordavie alikuwa akilindwa na askari wa jeshi la polisi, askari kanzu, Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na wale wa usalama barabarani.

attachment.php


Mbali na askari hao wa serikali ambao wamekuwa wakimlinda kila anapofanya mikutano yake, pia Geordavie analindwa na askari wake binafsi hali iliyowafanya baadhi ya watu kuamini kuwa ulinzi wake ni kama ule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK'.

"Sijawahi kumuona JK akilindwa na chopa lakini mtumishi wa Mungu Geordavie analindwa na ndege katika msafara wake! Hii ni mara yangu ya kwanza kuona," alisema muumini mmoja ambaye hakupenda kutajwa gazetini.
attachment.php


Hata hivyo, baadhi ya watu walikuwa wakihoji utajiri wa askofu huyo kutokana na fedha nyingi anazozitumia anapofanya mikutano katika sehemu mbalimbali jijini Arusha.

"Tunajua kuwa ni tajiri, lakini anapata wapi fedha za kutumia hivi?" alihoji muumini aliyejitambulisha kwa jina moja la Julius ambaye naye alihudhuria mkutano wa askofu huyo anayetumia kaulimbiu ya Ngurumo ya Upako katika kutoa huduma yake.
GEORDAVIE10.jpg

Pia, waumini wengine walilalamikia ugumu wanaoupata wanapotaka kumuona mtumishi huyo wa Mungu kutokana na ulinzi mkali anaopewa.

"Kila mtu alitamani kumuona mtumishi wa Mungu lakini haikuwezekana kutokana na ulinzi wake kuwa mkali, utajiri wake hakuna mfano, hata kule nyumbani kwake Arusha, anaishi kama Mfalme Daud," alisema Fred Mushi.
attachment.php


Gazeti hili lilimsaka Askofu na Nabii Geordavie kwa lengo la kutaka kujua sababu ya kuwa na ulinzi mkali na kutumia magari ya kifahari ikiwemo chopa katika mikutano anayoifanya lakini simu yake iliita bila kupokelewa.

attachment.php



Bravo Hongera ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie'

Hivi bongo kila mtu mwenye mbwembwe tu ni bilionea, je huyu mtu akienda mfano USA akataka kuwekeza hapo mradi mkubwa akaambiwa atoe "AUDITED FINANCIAL STATEMENT " ya miaka mitano nyuma iliyokaguliwa na wakaguzi wa kimataifa kama Earns & Young Juu ya mwendendo wake wa ulipaji kodi, makusanyo yake na kila kitu kama TRA wanavyosema, je anaweza kuwa na uthibitisho dhahiri usio na doa/ warakini? coz nchi za wenzetu huwezi kuwa unajiita Bilionea wakati ni mkwepa kodi mkubwa katika nchi na wanaoumia ni watu wa chini wanaofukuzwa kama digi digi kila waendapo kutafuta rizki. Tuacheni sifa za kijinga za kukweza watu mabilionea wakati akienda marekani anajifanya yeye ni mtu hali ya mtu tu. ni mtizamo wangu.... kwani mtizamo wa kumuita mtu bilionea kwa vipicha hivyo vya kuruka ruka ni sawa na yule mkuu wa nchi aliyesema kuwa a na foleni ndefu /jam bara barani hapa dar (msongamano wa magari) ni ishara ya maendeleo... ahaaa wapi.
 
Hivi bongo kila mtu mwenye mbwembwe tu ni bilionea, je huyu mtu akienda mfano USA akataka kuwekeza hapo mradi mkubwa akaambiwa atoe "AUDITED FINANCIAL STATEMENT " ya miaka mitano nyuma iliyokaguliwa na wakaguzi wa kimataifa kama Earns & Young Juu ya mwendendo wake wa ulipaji kodi, makusanyo yake na kila kitu kama TRA wanavyosema, je anaweza kuwa na uthibitisho dhahiri usio na doa/ warakini? coz nchi za wenzetu huwezi kuwa unajiita Bilionea wakati ni mkwepa kodi mkubwa katika nchi na wanaoumia ni watu wa chini wanaofukuzwa kama digi digi kila waendapo kutafuta rizki. Tuacheni sifa za kijinga za kukweza watu mabilionea wakati akienda marekani anajifanya yeye ni mtu hali ya mtu tu. ni mtizamo wangu.... kwani mtizamo wa kumuita mtu bilionea kwa vipicha hivyo vya kuruka ruka ni sawa na yule mkuu wa nchi aliyesema kuwa a na foleni ndefu /jam bara barani hapa dar (msongamano wa magari) ni ishara ya maendeleo... ahaaa wapi.
Acha ubishani wa kitoto!
Mleta Uzi kaeleza wazi kuwa ni Askofu tajiri bongo, hayo ya Amerika yanahusiana na nini hapa???
Watu wengine ni wabishi tangu mnazaliwa!
Huyu jamaa ni tajili na vyanzo vya utajiri wake vinatia shaka na hilo ndilo la kujadili sio issue za huko marekani na matajiri wa huko!
 
Back
Top Bottom