Geor Davie ni nani?

Geor Davie ni nani?

Nimemwangalia Channel 10 juzi Jummane waumini wake walikuwa wanampa zawadi ya mbuzi na yeye akawapa zawadi ya mikate!! Wakafuarahi na kushangilia

hahahaha---an exchange of a cent for a shilling! majanga!
 
inaonekana ni jinsi gani huyu 'nabii' alivyo MPAGANI. kama kweli anamuamini Mungu ni kwanini asimuombe ulinzi mpaka aombe ulinzi wa mwanadamu? angekuwa nabii wa kweli angetegemea ulinzi wa kiroho kuliko ulinzi wa nyama na damu (mwanadamu).

ukiona hivyo ana maadui wengi wa mwilini....utumishi wake mhhh...Maana manguli wa injili kama akina Kulola hawakuwahi kuwa na madudu ya namna hii?
 
Huyu Mtumishi wa Mungu vyeo vyote kampa nani? Hata huyo Papa wa

italy hana hivyo vyeo? Mkuu Ngongo huyu ( Mheshimiwa Dr Nabii na Mtumee Askofu Mkuu Geordavie) alicho kosa cheo kimoja tu na

yeye angelisema kuwa nimwana wa Mungu basi hapo angelifanana na Bwana Yesu kama wenzetu Wakristo walivyo mpa cheo Bwana

Yesu kuwa ni Mwana wa mungu na yeye huyu Mheshimiwa Dr Nabii na Mtumee Askofu Mkuu Geordavie angejipa cheo hicho

angelifanana na Bwana Yesu.Hawa ndio aliowasema Bwana Yesu kuwa Watakuja Manabii wa uongo ndio hawa wamesha kuja

tunawaona kwa maho yetu mwenye maho na akili ajionee mwenyewe kazi kwenu.

kama Mchungaji, Dr, Mheshimiwa, Mkurugenzi, Mchungaji, Askofu Mkuu, Mama Getrude Lwakatare---tapeli mkubwa---yeye hana mume lakini kutwa kucha anawaombea watu waolewe na wadumu kwenye ndoa zao. sijui yeye alipomuasi mume wake anatoa picha gani kwa waumini wake.
 
Kitu kinachonishangaza ni vile watumishi wa Mungu wanasakamwa kila kona! Ni kama watu wote walioandika wana uadui na huyu mtu! Ina maana huyu jamaa hajawahi kufanya jema hata moja! Ni kama yeye kuwa Mtumishi wa Mungu kimekera sana watu. Yeye ni mwanadamu tu kwani yeye ni Mungu! Watumishi wote, Mungu anawatumia kama punda au lorry! hivyo yeye kuanguka au kusimama hakuwahusu! Ikiwa anamwakilisha Mungu, wagonjwa wanapona, Mapepo yanatimuka, wachawi wanatupa vibuyu, watu wanafanikiwa na Mungu anainuliwa shida iko wapi! Msimwangalie mtumishi mwangalieni Mungu! Shida watu hawaamini kama Mungu anaponya wamezoea waganga hivyo wamemweka Mungu chini na kumwinua shetani. Hivi shetani anaponya? Mapepo yangekimbia? wachawi wangejisalimisha? kwa kweli mimi ninatamani kumwona huyu jamaa kama kwa Jina la Yesu mambo makuu yanatokea huyu ndio mganga ninayemtaka kwani hakuna mganga kama Yesu Kristo. Nimemfuatilia sana huyu mtu ndio maana nimeandika yote haya! Mengi mliyoandika ni uongo mtupu, mpaka jina lake, ametokea wapi, cheo chake, mambo anayoyafanya, hilo limenihakikishia wengi hawamjui na wengi hapa ni maadui wanachafua kazi anayoifanya. Tangu lini adui yako akakusifia! au akakusema vizuri! Kama haumwamini achana naye! Acha wale wanaoamini wakamwabudu Mungu na kupokea miujiza yao. Kweli wivu ni mbaya mlitaka awagawie hizo sadaka? Jamani Mungu akimwinua mtu kubalini!!! Mnafikiri Mungu amelala haoni yeye??? angeacha watu wote wapotee?? tena kwa taarifa yenu lol! watu wamejaa full j2 nilienda kuchungulia na ndio kwanza wanazidi kwenda!!! Hawa watumishi wanaojiona wema na wananguvu za Mungu si waombe ache basi! Mwacheni komandoo wa Yesu apige kazi kama mmeshindwa kuruka kwa ungo mseme!!

Hata shetani sehemu kadha wa kadha kwenye makusanyiko ya wanaomwabudu ana watu wamejaa kibao. Ujazo wa watu usikupe uhakika kuwa Mungu amemwinua sana au kuwa ni kweli ameitwa na Mungu. Inawezekana ameitwa na mungu na sio Mungu. Jifunze kupitia maandiko. Acha ushabiki.
Kila kazi itapimwa maandiko yanasema.
 
ukiona hivyo ana maadui wengi wa mwilini....utumishi wake mhhh...Maana manguli wa injili kama akina Kulola hawakuwahi kuwa na madudu ya namna hii?

Hakuna muhubiri aliyetikisa nchi hii kama kulola.lakini hakuwahi kuwa na ulinzi mkali kama huu
 
Ni nani anayemjua vyema huyu ndugu?
Nasikia ni Nabii
je huduma yake ipo wapi ?

GEORDAVIE1.jpg


=============


============[/QUOTE
ALIMPORA MKE WA MUUMINI WAKE, KIJANA MOJA DEREVA WA TOURS, MTOTO WA MZEE LOTA PALE SAKINA, MKEWE ANAITWA PAMELA
 
sasa kumekuchaaaaaa vp na source of INCOmeee ni sadalka tu ana ana biashara ingineee:A S-eek:
 
mkuu, umetumia maneno makali sana. ni kweli tunapaswa kuwa makini hawa 'manabii' wanaoibuka kila kukicha kwa 7bu ya matendo yake.

Wacheni uongo kufilisika wapi?kwa taarifa yako huyo unayemsema anaitwa Sekela ni mtumishi mkubwa kwenye huduma ya ngurumo ya Upako ,na Mungu anamtumia sana,..maisha yake ni mazuri na anamtumikia Mungu katika roho na kweli,acha ushambenga
 
Kwanza ni Utajiri halafu Neno la Mungu litakuja baadae Twende Nigeria tukajifunze mambo ya kufanya Miujiza unasemaje? kule kuna Askofu anayefanya miujiza na ni Tajiri sana si unamjuwa yule Askofu mkuu Tajiri wa Ki Nigeria?
Mungu ndiye anaye fanya Miujiza. Mtu ambaye anafanya miujiza halafu anatoza pesa huyo sio Mtumishi wa Mungu. Mungu huwa hatozi pesa kwasababu miujiza ni sehemu ya attribute yake.
 
Mungu ndiye anaye fanya Miujiza. Mtu ambaye anafanya miujiza halafu anatoza pesa huyo sio Mtumishi wa Mungu. Mungu huwa hatozi pesa kwasababu miujiza ni sehemu ya attribute yake.

Wakati wa kufanya Miujiza umeshapitwa na wakati huu ni wakati wa kufanya Toba turudi kwa Mwenyeezi Mungu tutubu madhambi yetu . Mambo ya Miujiza aliyafanya Bwana YESU. Muujiza

Uliobakia ni kwa ndugu zetu Waislam wao wanao Muujiza Mkubwa kupita yote Miujiza ya duniani nao ni Muujiza ya kitabu cha Waislam Quran ni kitabu kile kile alichokiacha kiongozi wao Mtume

Muhammad S.A.W. Miaka 1600 iliyopita mpaka hii leo kitabu chao Waislam Quran hakija chakachuliwa na mtu yoyote yule Hongera ndugu Waislam kwa Mwenyeezi Mungu amekilinda

kitabu chenu kitakuwepo mpaka siku ya hukumu. Mkuu@Ishmael funguwa Kanisa tutafute pesa na sisi tuwe Matajiri kama walivyo Matajiri Wachungaji wengine.
 
Watanzania wamekata tamaa na maisha thus why wakiambiwa uokovu huko huko wanakimbilia tu hii inatokana na ugumu wa maisha,ajira hakuna,maisha bora kwa kila mtanzania yamekuwa magazetini,gap kati ya matajiri na masikini ni kubwa,ndio maana watu wanajitafutia njia ya kupata riziki ukiondoa mpira,kucheza filamu na music ajira nyingine pekee iliyobaki ni kuanzisha kanisa,tumuombe mungu awaoneshe watu haki na batili yupi nabii wa ukweli na wa uongo,mungu ibariki tanzania

Excellent point.
 
Better nislimu niwe muislamu kuliko kuwa katika dini za kipumbavu kama za huyu tapeli.
 
Better kuzunguka jiwe kuliko kumpelekea jasho lako na la familia yako huyu tapeli. Islamu ni dini vile vile.
 
kama Mchungaji, Dr, Mheshimiwa, Mkurugenzi, Mchungaji, Askofu Mkuu, Mama Getrude Lwakatare---tapeli mkubwa---yeye hana mume lakini kutwa kucha anawaombea watu waolewe na wadumu kwenye ndoa zao. sijui yeye alipomuasi mume wake anatoa picha gani kwa waumini wake.

mume wake ndio alioasi
 
Back
Top Bottom