Gerson Msigwa Siku nyingine Rais akikupa Pesa za Kuwapa Yanga SC mwambie asaidie pia na Maiti zilizozuiliwa Mochwari Mahospitalini

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Gharama ya Tsh Milioni 20 kwa kila Goli na kutoa Ndege ya bure kwa Yanga SC iliyookoa Tsh Milioni 200 nina uhakika zingepelekwa pia Kulipia Maiti nyingi zilizozuiliwa Kutolewa katika Mochwari za Hospital Kubwa mbalimbali nchini Tanzania zingetosha na angepata Sifa zaidi kuliko anakozipeleka sasa.
 

Kipindi Simba nayo inachukua hizi hela Maiti ziilikuwa hazizuiliwi?
 
Huyu mama anatapatapa na Udhamini uchwara anaofanya.

Kimsingi kuna vitu vingi angefanya hata kupeleka huko kwenye hospital au watoto wa Maria ophanage wamelala njaa siku 2 za nyuma kisa msosi mdogo.


Hata atoe ngapi bado hana mvuto wa kisaisa na watanzania tunaombea muda wake uishe harakaharaka tupumue
 
Unakurupuka sana, Serikali ilishapiga marufuku kuzuia maiti kama Bado wanafanya ndio wale wapuuzi a TRA waliomwambia PM hawafanyii kazi maagizo ya siasa ila hili agizo lilitolewa..

Mwisho Yanga ndio Bingwa wa CAF
 
Michezo Ina fungu lake kwa rais
 
We kumpinga Rais kazi kweli kweli, Yale Yale ya ndungai, hapo ni nyuzi za kumponda tu kwa watu tusiojulikana, maana wanaojulikana Kama kina ndungai unatumbuliwa au kuzongwa achia ngazi.
 
Maria orphanage wamelala njaa wewe na pimbi wenzio mnashindana kunyweshana bia bar...hapo mtaani hakuna wenye pesa wachangie maria orphanage?
 
Kwani rais ndio aliwaambia wafe?
Nimerejea tu maneno ya yule jamaa aliyesema hawezi kuwasaidia wahanga wa tetemeko kwa kuwa kwenye kampeni zake hakuahidi kuwaletea tetemeko
 

Dah
Wanasema kila jambo na wakati wake
Huu ni wakati wa Yanga
 
Kama kuna maiti wako mochwari sema tukuchangie ukaikomboe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…