Mcqueenen
JF-Expert Member
- Nov 2, 2019
- 6,843
- 11,702
Kwa hapa Mwanza kituo cha kuweka hizo gesi kwenye gari yangu kipo wapi?Ni kwasababu hawana elimu ya kutosha kuhusu matumizi ya gesi asilia kwenye magari yao.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa hapa Mwanza kituo cha kuweka hizo gesi kwenye gari yangu kipo wapi?Ni kwasababu hawana elimu ya kutosha kuhusu matumizi ya gesi asilia kwenye magari yao.
Gharama ya kuweka huo mfumo ikoje?Boss una gari, ilete tukuongezee huo mfumo. Magari yanabadilishwa kila siku na yanatumia gesi.
Kwa Mwanza bado bossKwa hapa Mwanza kituo cha kuweka hizo gesi kwenye gari yangu kipo wapi?
Kwahyo ukiweka huo mfumo kwenye gari yako itakulazimu uishi mkoa gani?Kwa mwanza bado boss
Dunia nzima sijawai ona gari ya gas ila naona gari ya umeme na
Mafundi wa bongo wanaobadilisha gar ya mafuta kitumia mfumo wa gas weng ni matapeli na wanaharibu na kupunguza uwezo wa gari
Kwasasa ni magari ya Dar es Salaam tu boss.Ukiweka huo mfumo kwenye gari yako itakulazimu uishi mkoa gan?
Sawa boss, sisi ngoja tuendelee kutumia gesi yetuBora nijipange ninunua Hybrid mafuta nanusa tu 1litre natembea 25km
Na ukiwa Dar, itakulazimu kuwekea wapi gesi?Kwasasa ni magari ya Dar es Salaam tu boss.
Kwa sasa vituo vya kujaza gesi vipo Tazara and Ubungo tu. Unaweza kuiona fursa wazi ya kuwekeza hapa sio? Jenga kituo chako cha kujaza gesi.Na ukiwa dar, itakulazimu kuwekea wapi gesi?
Au hata ukiwa Chanika unapata
Kitagharimu kama shngap?Kwa sasa vituo vya kujaza gesi vipo Tazara and Ubungo tu. Unaweza kuiona fursa wazi ya kuwekeza hapa sio? Jenga kituo chako cha kujaza gesi.
Kwani gesi ya kupikia inatoka hapa kwetu..?Kiukweli gesi bado haija tufaidisha kabisa, gesi ya kupikia tuu Kila siku inazidi kupanda kana kwamba tunaitoa south Africa
Upo tayari nikuletee langu? Maana nimekaa na hela nimesugua benchi na hela yangu ya kufungia mfumo mpaka imekatika yote.Boss una gari, ilete tukuongezee huo mfumo. Magari yanabadilishwa kila siku na yanatumia gesi.
Lilete boss ubadilishiweUpo tayari nikuletee langu?,maana nimekaa na hela nimesugua benchi na hela yangu ya kufungia mfumo mpaka imekatika yote.
Ndio tuitumie boss, badilisha gari yako boss.Ni rasilimali muhimu sana tumepata ila tatizo bado hatujakua tayari kuitumia
Ahsante kwa ushauri wako boss, hili litafanyiwa kazi.Naomba mamlaka husika za juu hili swala la ufungaji wa gesi asilia kwenye vyombo vya moto ufatiliwe,kuna mbung'i linapigwa kimya kimya bila ya wengi kufahamu, haiwezakani vifaa vya kufungia viwe ghali sana na hata kupatikana kwake ni mtiti.
Tanzania inakadiriwa kuwa na mita trilioni 230 za ujazo za gesi asilia, ingawa zilizothibitishwa mpaka sasa ni futi trilioni 57.5, hivyo kuiweka kwenye ramani ya dunia ikishika nafasi ya 82.
Gesi hiyo tayari imeanza kuzalishwa katika visiwa vya Songosongo wilayani Kilwa, mkoani Pwani na eneo la Msimbati mkoani Mtwara, ikitumika kuzalisha umeme na kuendesha mitambo ya baadhi ya viwanda nchini.
Pamoja na wingi wa hazina ya gesi hii muhimu, kwa kiasi kikubwa Tanzania bado inategemea mafuta kuendesha mitambo ya viwanda vyake pamoja na magari ya mizigo na abiria na pia baadhi ya majenereta ya kuzalisha umeme unaosambazwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).
Uhalisia wa hali ukiwa hivyo, Shirika la Petroli Tanzania (TPDC) kwa upande wake lina mkakati wa kuanzisha vituo vya kujaza gesi kwenye magari yaliyoongezewa mfumo unaotumia gesi.
Bei ya mafuta imeathiriwa sana na vita vya Russia na Ukraine vinavyoendelea. Mafuta yalipanda bei na jinsi yalivyopanda, bidhaa nazo zilipanda bei na nauli zilipanda. Thamani ya vitu vingi ilionekana kupanda bei kwa sababu mafuta yalipanda.
Hivyo gesi hiyo ndiyo suluhisho la tatizo la mafuta nchini. Kwa wastani kg 1 ya CNG inakufikisha km 15 wakati lita 1 ya petroli inakufikisha km 10. Lakini pia unaokoa 33.5% ya gharama unapotumia CNG hata kama bei ya CNG ni sawa na ya petroli.
Julai 2020, TPDC, ilisema Sh28 bilioni zilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya kujaza gesi kwenye magari. Vituo vya CNG vinatarajiwa kujengwa katika kituo cha mabasi yaendayo haraka kilichopo Ubungo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na pembezoni mwa Barabara ya Sam Nujoma na vituo vidogo vya kupokelea na kusambaza gesi asilia vingejengwa Soko la Samaki Feri, Hospitali ya Taifa Muhimbili na katika kiwanda cha dawa cha Kampuni ya Kairuki Pharmaceutical kilichopo Zegeleni mjini Kibaha.
Hivyo kutokana na hilo, uelewa wa umma juu ya matumizi ya gesi asilia unapaswa kuongezwa ili kuikomboa nchi kutokana na matatizo ya kupanda kwa bei ya mafuta duniani.
Na hilo ndilo ninalolifanya sasa kuhakikisha Tanzania inaelewa umuhimu wa kutumia gesi asilia iliyoshindiliwa kama nishati kwenye magari kwa kuendelea kuandika makala kwenye mitandao ya kijamii.
Hivyo kubadilisha magari ya Tanzania ili yatumie vyanzo mbalimbali vya nishati imekuwa ikiongezeka kila siku. Watanzania wengi zaidi wabadilishe magari yao yatumie gesi asilia ili wanufaike na maliasili nono zinazopatikana katika taifa letu.