Gharama za mobile banking zinatisha, ni ujambazi kwelikweli

Gharama za mobile banking zinatisha, ni ujambazi kwelikweli

Dah sijui tunaelekea wapi, hizi huduma zilipaswa kutupa unafuu wananchi kufanya miamala bila usumbufu lakini imekua ujambazi hasa hasa.

Niliwahi kuhamisha laki mbili kutoka Benki kwenda mpesa nikakatwa 11,000/= hapo bado sijakutana na Makato ya mpesa, nikajikuta nakatwa karibu 16000/= kupata 194,000 sijui, nikabaki nimeduwa.

Ukitoa hata 40000 wanakata 6000/= Makato ya mpesa/tgopesa/Airtel money utakutana nayo juu kwa juu.

Jana nimenunua vocha ya 2000 kutoka mobile banking naangalia statement wamekataa 700/= anyway sawa tu IPO siku kitaeleweka tu maana washatuona misukule.

Nimefuta app zao zote ila najua hata kwenye atm ni yaleyale.
Nchi limekuwa la kipumbavu sana! Tukome kuongozwa na jike!
 
Simu Banking sijawahi kutumia na hizo App zijawahi kudownload.

Mara chache sana niliwahi kutumia NMB Mobile(zamani kabla App hazijaja) kuhamisha hela kwenda M-Pesa, sijui nilikatwa kiasi.

Natumia tu ATM, kwa sada napata maumivu ya tozo.

Maumivu ninayoyapata sasa ni kuhamisha hela kutoka M-Pesa kwenda Bank. Nikihamisha 789K kwenda NMB nikalimwa 10,833
 
CRDB hao. Makati vile vile tu. Mfano kutoa 50,000 kuleta Mpesa kisha kuitoa iyo upate Cash.

Ni bora uchukue boda uende ATM na kurudi.

Maana unaweza katwa hapo jumla ya 10,000 na kuendelea.
Mi nitaanza tunza kwa kibubu
 
Watanzania wengi wamesoma ila hawajaelimika...

Kutuma hela kutoka benki moja kwenda nyingine, muamala hutambulika kama TISS, gharama yake ni 10,000 hata ukituma 1000 watakukata 10000 ya BOT, afu bado makato ya benki na tozo ya serikali
 
Na ukitaka kujua Kama ni uwizi siku hizi benki nyingi hazijikiti kuweka ATM mashine nyingi, ama branches bali kuwapa mawakala ambako makato ni makubwa
 
Ukilipa usafiri +muda si bora utumie si. Banking ti
Mkuu mimi "muda" huwa siujumuishi kwenye gharama, maana silipwi directly kwa muda
Hujanielewa mkuu,iko hivi mimi ni mdau wa bank (a) sasa kupitia hii app yetu ninauwezo wa kutoa pesa via atm bila kuwa na atm card na pesa nikachukulia kwenye kituo chochote cha atm mashine.
Sasa kama ntaenda kutoa kwe ATM kuna tofauti gani na kwenda kwenye ATM na CARD yangu nikatoa? Au maana natembea nayo popote
 
Watanzania wengi wamesoma ila hawajaelimika...

Kutuma hela kutoka benki moja kwenda nyingine, muamala hutambulika kama TISS, gharama yake ni 10,000 hata ukituma 1000 watakukata 10000 ya BOT, afu bado makato ya benki na tozo ya serikali
We unajua kila kitu mkuu?
 
Enheeee!.... Issue ya wale Panya wa barabarani imepangwa madhubuti kuhaamisha upepo wa mijadala Kama hii,, kwa sasa husikii issue. Za tozo ni Panya Panya kifupi tumesahau na tumekubali kukamuliwa
 
Hali ni mbaya sana sasa hivi. Makato yamezidi mno. Haya si maisha kabisa. Bora tuhamie kule tulikoambiwa.
 
Back
Top Bottom