LGE2024 Godbless Lema: Land Rover Festival ni mkakati wa watu wasijiandikishe

LGE2024 Godbless Lema: Land Rover Festival ni mkakati wa watu wasijiandikishe

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Uandikishaji kwenye Daftari la Wapigakura wa Serikali za Mitaa umeanza rasmi leo, tarehe 11 Oktoba, 2024, na utaendelea hadi Oktoba 20, 2024. Hatua hii inampa fursa kila Mwananchi mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024. So ni vizuri kutumia siku hizi kumi kujisajili ili kila mmoja aweze kutimiza haki yake ya kikatiba.
Hata hivyo, jana huko Arusha, Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, alitoa onyo kwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha John Kayombo kuhusu kufanyika kwa tamasha la Land Rover Festival ambalo litafanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Oktoba Katikati ya zoezi la uandikishaji.
1728635692054.png
Lema, ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Arusha Mjini, alidai kuwa tamasha hilo linaweza kuwa na athari kwa zoezi la uandikishaji. Na kueleza wasiwasi wake kwamba tamasha hilo linaweza kuwakwamisha baadhi ya wananchi wasijiandikishe, na hivyo kushindwa kutimiza haki yao ya msingi ya kupiga kura ifikapo Novemba 27.
Pia, Soma:
+
Godbless Lema: Kanuni za Uchaguzi 2024 ni za Kihuni, Hatuwezi Kususa, Kamati Kuu Imeazimia Kupambana na Kushinda Uchaguzi
+ Huyu Nabii Geordavie ana utajiri kiasi gani? Ampa Paul Makonda Land Rover zaidi ya 10 huko jijini Arusha!
+ Team Land Rover wapita Mwenge kwa Mbwembwe kuelekea Arusha kwa Makonda kwenye Land Rover Festival
 

Attachments

  • 1728635645225.png
    1728635645225.png
    1.2 MB · Views: 6
Uandikishaji kwenye Daftari la Wapigakura wa Serikali za Mitaa umeanza rasmi leo, tarehe 11 Oktoba, 2024, na utaendelea hadi Oktoba 20, 2024. Hatua hii inampa fursa kila Mwananchi mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024. So ni vizuri kutumia siku hizi kumi kujisajili ili kila mmoja aweze kutimiza haki yake ya kikatiba.

Hata hivyo, jana huko Arusha, Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, alitoa onyo kwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha John Kayombo kuhusu kufanyika kwa tamasha la Land Rover Festival ambalo litafanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Oktoba Katikati ya zoezi la uandikishaji.

Lema, ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Arusha Mjini, alidai kuwa tamasha hilo linaweza kuwa na athari kwa zoezi la uandikishaji. Na kueleza wasiwasi wake kwamba tamasha hilo linaweza kuwakwamisha baadhi ya wananchi wasijiandikishe, na hivyo kushindwa kutimiza haki yao ya msingi ya kupiga kura ifikapo Novemba 27.
Sasa yeye Lema si aanzishe tamasha la kuhamasisha watu wakajiandikishe.

Kufilisika kisiasa ni kitu mbaya sana aise, kuna mfanya mtu awe na makasiriko na kila kitu wanachofanya wengine dah 🤣
 
Hata saa mbovu kuna muda inasema kweli, ule upotoshaji wa Upinzani wanaibiwa kura kumbe sio kweli ila Lema kaonesha ukweli kwamba Upinzani huwa hawajiandikishi. 2025 ni kilio kikubwa mno kwa upinzani
 
Hata saa mbovu kuna muda inasema kweli, ule upotoshaji wa Upinzani wanaibiwa kura kumbe sio kweli ila Lema kaonesha ukweli kwamba Upinzani huwa hawajiandikishi. 2025 ni kilio kikubwa mno kwa upinzani
Unaota halafu unajitafsiria ndoto, taabu kwelikweli.
 
Sasa yeye Lema si aanzishe tamasha la kuhamasisha watu wakajiandikishe.

Kufilisika kisiasa ni kitu mbaya sana aise, kuna mfanya mtu awe na makasiriko na kila kitu wanachofanya wengine dah 🤣
Kama wewe tu ulivyo, kutwa kuchwa kukasirikia yale wayafanyayo chadema. Utaugua ugonjwa wa moyo ndugu. Kubali tu kuwa Mungu alituumba kuwa wenye mitazamo tofauti kuhusu mambo mbalimbali, na hiyo ndio afya kwa maendeleo ya mwanadamu. Huwezi kubadili chochote, vinginevyo ujinyonge tu pale makasiriko yanapozidi.
 
Kama wewe tu ulivyo, kutwa kuchwa kukasirikia yale wayafanyayo chadema. Utaugua ugonjwa wa moyo ndugu. Kubali tu kuwa Mungu alituumba kuwa wenye mitazamo tofauti kuhusu mambo mbalimbali, na hiyo ndio afya kwa maendeleo ya mwanadamu. Huwezi kubadili chochote, vinginevyo ujinyonge tu pale makasiriko yanapozidi.
kwani chadema wanafanya nini gentleman na walivyo filisika na mikopo namna ile? 🤣

siwezi kubadili mihemko na ghadhabu zenu wala tabia yenu ya kuporomosha matusi mazito mazito kwa mpangilio, kwasabb huo ndio utamaduni na utambulisho wenu kwa jamii 🐒

kwanini ni babaike na kitu kama hicho sasa?🤣
 
Mwanaume ukiwa mtu wa kulalamika hadi unaboa.

Na yeye afanye yake
 
kwani chadema wanafanya nini gentleman na walivyo filisika na mikopo namna ile? 🤣

siwezi kubadili mihemko na ghadhabu zenu wala tabia yenu ya kuporomosha matusi mazito mazito kwa mpangilio, kwasabb huo ndio utamaduni na utambulisho wenu kwa jamii 🐒

kwanini ni babaike na kitu kama hicho sasa?🤣
Usingebabaika ungepiga kimya kuhusu mambo yao. Nimeobserve na kuona kuwa una negativity ya hatari juu yao. Hii sio poa.
 
Usingebabaika ungepiga kimya kuhusu mambo yao. Nimeobserve na kuona kuwa una negativity ya hatari juu yao. Hii sio poa.
aah sasa unakaaje kimya na ukweli? huo si uchoyo wa kiwango cha juu sana gentleman?

ni sawa tu gentleman ikiwa ukiambiwa au kuelezwa ukweli ni negativity 🤣

ndiyo inayokufanya upate mihemko, ghadhabu na makasiriko, right ?🤣
 
Sasa yeye Lema si aanzishe tamasha la kuhamasisha watu wakajiandikishe.

Kufilisika kisiasa ni kitu mbaya sana aise, kuna mfanya mtu awe na makasiriko na kila kitu wanachofanya wengine dah 🤣
Kwakweli kabisa lema amepotea kabisa

Hana tena agenda
 
Kwakweli kabisa lema amepotea kabisa

Hana tena agenda
Kumsikiliza Lema mtu inabidi kwanza upitie Mirembe madaktari wakuhakikishie kuwa kweli akili huna na wakupe cheti cha uthibitisho kuwa hazimo ndipo uende kumsikiliza Lema
Mwenye akili hawezi msikiliza Lema
 
Back
Top Bottom