Pre GE2025 Godbless Lema: Mkakati wa Tone Tone ni mpango wa kuchangia fedha kwa chama kwa kutumia mifumo ya kidigitali

Pre GE2025 Godbless Lema: Mkakati wa Tone Tone ni mpango wa kuchangia fedha kwa chama kwa kutumia mifumo ya kidigitali

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Fedha ya chama hicho Godbless Lema ameeleza kuwa mkakati wa Tone Tone ni mpango wa kuchangia fedha kwa chama kwa kutumia mifumo ya kidigitali ambayo utamuwezesha mtu yeyuote kuchangia kwa kutumia mitandao ya simu na malipo ya kurudia rudia.

Soma Pia: CHADEMA wanazindua mkakati maalum wa kidigitali tone tone usiku huu, Februari 27, 2025

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025


Lema ameeleza kuwa kupitia tone tone mtu yeyote ataweza kutoa fedha kidogo aliyonayo na pale zitapounganishwa zitajaza na kufikisha kiasi ambacho kitakiwezesha chama kuweza kuendesha mikakati yake.Mungu
Tone Tone hadi mafuriko
 
Mtanzania atakayetaka kuichangia CHADEMA atakuwa na matatizo makubwa sana kichwani mwake. Ni bora pesa hizo mtu unayejitambua uwapelekee yatima na wajane huko au watu wenye mahitaji maalumu .

Kwa sababu CHADEMA wamekuwa watu wa kuomba michango miaka na miaka lakini matokeo ya michango hiyo huwa ni giza totoro. Chama kinashindwa hata kulipia kodi ya ofisi huku mikoani au hata kujenga tu ofisi za chama.

Kwa sasa chama kinapokea Riziki ya takribani Million 107. Lakini kilipewa kwa mkupuo zaidi ga Billion 2.7 kama Ruzuku. Pesa zote haieleweki zimekwenda wapi na zimefanya shughuli gani. Ni aibu mpaka leo chama kimeshindwa kuanzisha hata Kituo cha redio au Tv . Matokeo yake tuliona akina lissu waking'ang'ania kwenye Tv za watu za Wasafi FM eti wanataka kufanyiwa mahojiano.

Chama hakina kitega uchumi cha aina yoyote ile .yaani hata biashara ya kuuza sindano tu nguo CHADEMA imeshindwa kubuni.

Sasa michango ndio muarobaini wa shida za CHADEMA? Ndio chanzo cha mapato? Ndio njia ya kukifanya chama kujitegemee? Ndio akili za viongozi wa CHADEMA zilipoishia hapo? Chama cha miaka zaidi ya 30 kinataka kujiendesha kwa michango? Hivi huu siyo udumavu wa akili kweli?
Nailed
 
Bado mnachanga hela😅😅😅
.hakuna majitu mapumbavu kama Nyumbu.
Swala ni aliyepo na aliyeondoka wote wezi tu matapeli.
Huyu wa sasa ana kesi ya ukimbizi huko alipo.
Huyo M kiti mstaafu anatengeneza deal mil 107.
90 milion pesa zitapigwa.
Muwe waelewa mkiambiwa mnadaiwa.
Ile office mpya ya Chandema Ni Nyumba ya Grace dada yake malyenge.alishafariki nafkiri.
Nyie endeleeni kuchanga mpk mshituke kumekucha.
 
Back
Top Bottom