Goma: Jeshi la Mamluki kutoka Romania wajisalimisha Rwanda

Goma: Jeshi la Mamluki kutoka Romania wajisalimisha Rwanda

Teknocrat

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2018
Posts
4,967
Reaction score
11,056
Jeshi la kukodiwa la kutoka Romania, wameona moto uliukuwa unatembezwa na M23 na RDF, na kuamua kujisalimisha kwa UN, ambapo, waliombewa kuingiwa Rwanda kwa mipango ya kusafirishwa na kurudi kwa Romania

1738180693465.png
1738180498543.png


 
Propaganda, yaani DRC aache kuomba financial support na weapons aje aombe wanajeshi?!
 
Jeshi la kukodiwa la kutoka Romania, wameona moto uliukuwa unatembezwa na M23 na RDF, na kuamua kujisalimisha kwa UN, ambapo, waliombewa kuingiwa Rwanda kwa mipango ya kusafirishwa na kurudi kwa Romania

View attachment 3218136View attachment 3218133


Hizi nchi za kiafrika zinaongozwa na wezi na mafisadi wakubwa .
Wanajeshi wa Kongo kwa hili walitakiwa wamto rais mpumbavu madarakani waweke demokrasia ya kweli au wakae meza moja na waasi waweke utawala wa majimbo ufanye kazi ipasavyo sio utawala wa majimbo kama halafu kila kitu kinasimamiwa na Serikali kuu .

Rais anayetawala nchi yenye madini na kila kitu anashindwa kuajiri wanajeshi na kuwalipa mishahara mizuri. Ni mpumbavu sana huyo Rais anayeirushia Lawama Rwanda wakati hafai hata kuwa mwenyekiti wa kitongoji . Kwa nini asitoe baadhi ya maeneo yenye dhahabu yanasimamiwa na Jeshi kwa ajili ya kuliwezesha badala yake anawalinda Wezi kutoka Ulaya kwa gharama kubwa . Bora angekaa na Kagame wanajipanga namna ya kutoa huduma kwa watu wa mashariki kwa Kongo na kuweka uhuru kwa wananchi kuishi wanapotaka bila kuulizwa . Yaani wafute pumbavu wa nchi za kiafrika kufungiana mipaka na kudhibiti watu kuhamia sehemu nyingine wanakoona kuna fursa .

Huu ujinga pia upo nchi za Afrika Mashariki watawala wanafunga sheria za kuzuia hata watu kupita kwenda nchi nyingine kama Afrika kusini . Watanzania wanawazuia waethiopia kupita kwenda Afrika kusini . Lakini Afrika kusini haiwakatazi kwenda huko . Huu ni kama uchawi kwa binadamu . Mtu anapita na kujificha kwenye Tanker la mafuta ili aende zake Afrika kusini akatafute riziki lakini mchana kutwa anashindwa kwa gharama kubwa na kupelekwa gerezani kwa gharama ya kodi za watanzania .

Kwa nini asipewe masharti ya kwenda Huko anakokwenda tuu na sio kukaa nchini . Huko ndio wawakatae . Kama Afrika Kusini wangewakataa wasingeenda . Wanaenda kwa sababu wanawapokea .

Sasa sisi kinachotuwashia ni nini ?


Tanzania kama tungekuwa na Watawala wapenda haki tulipaswa tuwasaidie M23 na sio kuwasadia mawakala wa Mabeberu waliojificha kwenye starehe Kinshasa. Nchi yenye wetu zaidi ya mil.100 haina jeshi na rasilimali zinapotosha kuilisha ulaya kwa Karne tano leo tunakwenda kuwasadia kuwaua waafrika wenzao . Tuna akili kweli au ni uhuni wa kutafuta pesa kwa malipo ya Majizi yaliyojificha chini ya UN kulinda utoroshaji na wizi wa madini .


Ikumbukwe kuwa watawala wengi wa duniani ni mawakala wa shetani wapo tayari kugawa na kuuza kila kitu kwa wazungu alimradi wakae madarakani na magari ya kifahari na misafara na ving'ora bila kujali kuwa hao wazungu wanatorosha mpaka waanyama kama wanavyofanya huku kwetu . Kisha Jeshi na polisi wanakaa kimya na usalama wa Taifa na Tanapa lakini wanawabambikia keshi akina Dr. Slaa ili wafie gerezani .Yaani nchi za kiafrika Usalama wa nchi ni madaraka ya mtu mmoja na familia yake . Yaani eti Mgeni kutoka Omani ndiye usalama wa nchi hata kama anapora na kuuza kila kitu kwa wageni bado dola linatumia nguvu kubwa kuhakikisha anatawala hata kama Katiba imetoa fursa kwa wananchi kumkataa kwa sababu ya matendo yake ya wizi na ufisadi na kuuza rasilimali za umma kwa wageni bila huruma kwa kutegemea kuwa dola itamlinda katika uhalifu wake huo wa kuteketeza taifa kiuchumi huku yeye akizidi kuwa bilionea kwa muda mfupi .

Waafrika tumuunge mkono Kagame ,Museveni na M23 ili wazungu wakimbie pale Goma na Afrika kwa ujumla .
Hawa wazungu ndio wanaoleta silaha za kuua waafrika wenzetu .

Mfano uchaguzi unaokuja hapa Kongo ya CCM mabomu ,silaha na risasi na magari ya washawasha yatanunuliwa kwa wingi kama vile suala la uchaguzi ni suala la Vita na uhalifu mkubwa lakini kumbe ni mafisadi yanayolinda ufisadi wao na kusalia madarakani kwa nguvu .
Sasa kama uchaguzi ni vita na vurugu ni bora usifanyike . Kama ukifanyika ni vita na kuuana na kutokana sasa huo uchaguzi ni wa nini ?
Uchaguzi tunaziona waangalizi huru kutoka nje lakini tunataka tuwafurahishe hao hao kwamba tuna demokrasia ya vyama vingi kinafiki.

No Election iwe ni kwa vitendo . Hakuna haja ya kufanya uchaguzi unaoacha wetu na vilema na vifo na watu wengi kufungwa gerezani ni bora nchi nzima wakamatwe wawekwe gerezani siku hiyo ya uchaguzi . Nchi itakua salama zaidi maana CCM watakua wanaendelea na wabunge na madiwani wao waliopatikana kihuni mwaka 2020.
 
Kwanini walipokamatwa wamepelekwa Rwanda na sio Burundi?
Njia hiyo ya kwenda Burundi ipo? Angalia hiyo picha. Rangi nyekundu, ni eneo inalolikalia M23. Airport wanayo. Njia za ardhini kuingia Goma, wanazo wao. Ziwani, walishafunga njia. Rwanda ilibaki tu ndo kimbilio kwa FARDC, FDLR, Wazalendo na Mercenaries. SADC, wapo sehemu safi na salama, wala hawaguswi. M23 ilisema shida ni kati yake na serikali wala si kati yake na hizo nchi. Isimgelikuwa na adabu, kingeumana
 

Attachments

  • IMG_0649.jpeg
    IMG_0649.jpeg
    174.2 KB · Views: 1
Kwanini walipokamatwa wamepelekwa Rwanda na sio Burundi?
Inajulikana wazi, hao M23 wengi wao ni hao RDF, sema wanapewa gwanda tofauti wanaingizwa msituni pamoja na maafisa wao kabisa kuongoza mashambulizi. inakuwaje kama last time waliamua kuachia Goma wenyewe, halafu wakapotea kama upepo, halafu sasa wameibuka tena na sasa ni wengi na vifaa vingi
Kwahiyo jibu unalo nadhani kwanini wamepelekwa Rwanda
 
Njia hiyo ya kwenda Burundi ipo? Rwanda ilibaki tu ndo kimbilio kwa FARDC, FDLR, Wazalendo na Mercenaries. SADC, wapo sehemu safi na salama, wala hawaguswi. M23 ilisema shida ni kati yake na serikali wala si kati yake na hizo nchi. Isimgelikuwa na adabu, kingeumana

Sinema ya kitoto sana hii ya Kagame, kwanini mauzo ya Cobalt na Tantulum nje ya nchi toka Rwanda huwa yanaongezeka kwa kasi sana kila mara M23 inapovamia DRC?

What is the logic behind?
 
Sinema ya kitoto sana hii ya Kagame, kwanini mauzo ya Cobalt na Tantulum nje ya nchi toka Rwanda huwa yanaongezeka kwa kasi sana kila mara M23 inapovamia DRC?

What is the logic behind?
Ndo na wewe ujiulize. Na swali la kujiuliza, hakuna aliewahi kukataa hayo madini kwamba ya wizi. Hao hao ndo wanasema lazima wajue yametoka wapi. Hayo hayo ndo wanayoyategemea kwenye biashara zao. Unategemea nani afunge kiwanda chake kisa watu weusi wanakufa huko!? Hayo makundi mnayoyasema, mengine niya wakubwa huko huko serikalini. Wanawapa watu siraha kulinda mari zao, wachimbaji wakimaliza wenyewe wanaijia mzigo wao. Mzungu muuzie kwa dola 1000, huku anajua mzigo unakotoka!? Thubutu!! Hapo ndo ujue ni foleni ya mafia, ukiingia kichwa kichwa umeisha.
 
We mwehu kweli. Goma hakuna mzungu aliyevamia, na hana haja ya kuvamia, M23 wanaipa Rwanda madini yote anayohitaji mzungu, na yasafirishwa tokea Rwanda kwa raha mstarehe
 
Njia hiyo ya kwenda Burundi ipo? Angalia hiyo picha. Rangi nyekundu, ni eneo inalolikalia M23. Airport wanayo. Njia za ardhini kuingia Goma, wanazo wao. Ziwani, walishafunga njia. Rwanda ilibaki tu ndo kimbilio kwa FARDC, FDLR, Wazalendo na Mercenaries. SADC, wapo sehemu safi na salama, wala hawaguswi. M23 ilisema shida ni kati yake na serikali wala si kati yake na hizo nchi. Isimgelikuwa na adabu, kingeumana
Kwanini kila wanapopigwa wanakimbilia Rwanda na kulindwa badala ya kukamatwa na kupelekwa mahakama za uhalifu wa kivita?
 
Ndo na wewe ujiulize. Na swali la kujiuliza, hakuna aliewahi kukataa hayo madini kwamba ya wizi. Hao hao ndo wanasema lazima wajue yametoka wapi. Hayo hayo ndo wanayoyategemea kwenye biashara zao. Unategemea nani afunge kiwanda chake kisa watu weusi wanakufa huko!? Hayo makundi mnayoyasema, mengine niya wakubwa huko huko serikalini. Wanawapa watu siraha kulinda mari zao, wachimbaji wakimaliza wenyewe wanaijia mzigo wao. Mzungu muuzie kwa dola 1000, huku anajua mzigo unakotoka!? Thubutu!! Hapo ndo ujue ni foleni ya mafia, ukiingia kichwa kichwa umeisha.
USA, France ndio wapokeaji wakuu ya hizo blood minerals. Ni chain ndefu inayoishia kwa watu kama Elon Musk , Iphone nk.
 
USA, France ndio wapokesji wakuu ya hizo blood minerals
Ndo sasa uniambie! Wao wataleta majeshi yao kulinda machimbo!? Jibu ni hapana. Wanachokifanya ni kumtafuta nani anaweza kusimamia masrahi yetu! Haya yupo huyu. Anahitaji nini na nini!? Chochote atapewa. Jaribu kuingilia sasa uone litakalokukuta!!! Hadhalani watajifanya wanakemea, nyuma ya pazia wanawekana sawa. Kwenye hivi vita, Rwanda imepoteza raia 9. Kwa mabomu yaliyorushwa kutoka DRC. Na inasemekana yamerushwa na FDLR. Hiyo ni tiketi ya kuingilia tayari. Lakini, silaha za kudungua makombola, zimefanya kazi ajabu. Je, kama hakukuwa na maandalizi, zilinunuliwa kufanya nini!? Hizo ni zilizowekwa wazi. Ambazo hazipo!?
 
USA, France ndio wapokeaji wakuu ya hizo blood minerals. Ni chain ndefu inayoishia kwa watu kama Elon Musk , Iphone nk.
Hao sasa ndo uambie kwamba lazima nchi ziende kutoa msaada nini na nini! Inasemekana South Africa ina mgodi huko. Na washikaji wanaumendea sana. Kitatokea nini!? Haya, kosa dogo sana, linawagharimu. Raisi alitaka kula na mrusi, wakaona isiwe tabu. Wamechoma balozi za watu! Ni hapo wababe wanaenda kuwekana sawa. China ipo na migodi kibao. M23 ukisikia wanaenda mpaka Kinshasa, unadhani hawajui waliongealo!?
 
Hao sasa ndo uambie kwamba lazima nchi ziende kutoa msaada nini na nini! Inasemekana South Africa ina mgodi huko. Na washikaji wanaumendea sana. Kitatokea nini!? Haya, kosa dogo sana, linawagharimu. Raisi alitaka kula na mrusi, wakaona isiwe tabu. Wamechoma balozi za watu! Ni hapo wababe wanaenda kuwekana sawa. China ipo na migodi kibao. M23 ukisikia wanaenda mpaka Kinshasa, unadhani hawajui waliongealo!?
Sawa, wana backing toka kwa mataifa makubwa, na ndio maana inabidi wote tulaani uporaji huu wa bila aibu na wa kimalaya kabisa!
Ni kama nyumba inavyovamiwa na panya road.., ndio kinawapata DRC
 
Back
Top Bottom