Goodluck Gozbert sio mwimbaji wa Gospel

Goodluck Gozbert sio mwimbaji wa Gospel

Mkuu Author, Unachokifanya hakiakisi hata tone ya vile unavyojiita. Niliposoma kichwa cha uzi wako na jina lako nilihamasika sana kufungua huu uzi wako lakini nimesikitika sana baada ya kuona na kusoma ulichoandika kwa sababu kadha wa kadha.

Kwanza, Umeshindwa kuchunguza na kuelewa kuwa Gospel ambayo anaimba msanii wa Tanzania ni Bongo Fleva pia. Kwa lugha nyepesi umeandika bila kuelewa undani wa hicho unachokiandika. Pole sana.

Pili, Gospel sio lazima iimbwe juu ya biti za vinanda. Hio ni kwa sababu Gospel ni ujumbe na sio uzuri au ubaya wa biti. Swali ni kwamba ujumbe aliouonyesha Gozbert humo unahamasisha injili au unapinga injili??

Naomba unielewe kuwa sikatai kuwa unachokisema ni sahihi. Unaweza kuwa sahihi au usiwe sahihi. Ninachoshangaa ni kwamba umeshindwa kuthibitisha malalamiko yako. Ni kama watu wanaotaka bangi ihalalishwe - huwa wapo sahihi, ila hawajui kuitetea hoja yao.

Anyways, Ukijibu hayo maswali hapo juu naomba nikupe home work. Nenda uisikilize Album ya Kanye West, Jesus is King.
Mkuu Chachasteven, Gozbert mimi mwenyewe nilikuwa namtilia mashaka sana mara niliposikia nyimbo zake kwa mara ya kwanza, lakini wimbo huu alioutoa ndio ulithibitisha kwamba huyo hakiki sio Mtumishi, yaani sio muimbaji wa Nyimbo za Injili bali huyo ni wale wanaoitwa wasanii wa nyimbo za injili, itoshe tu kutambua na hakuna haja ya kubishana hapa, naamini hata yeye mwenyewe analijua hilo, na anashangaa anapoona kuna watu wanamtetea, Kuimba Injili inataka Mtu uwe na Wito na pia Ushuhuda, sio kujiimbia tu kwa sababu unaweza kuimba, sijajua wewe msimamo wako kiimani ni upi, yawezekana unaweza kuwa unamtetea ukifurahi kuona jinsi anavyowapoteza watu wengi watakaochagua kumfuata, lakini kama wewe unatamani kuona watu wanapewa iliyo kweli kwenye Injili nadhani tusaidiane kuwakosoa watu kama Gozbert waache mara moja kusaidia wanaoutukana Ukristo kwa sababu ya style zao za Uimbaji, nakuhakikishia asipokemewa atakuja kufanya vituko sana kwenye aina hiyo ya uenezaji wa Injili.
 
Mkuu Author, Unachokifanya hakiakisi hata tone ya vile unavyojiita. Niliposoma kichwa cha uzi wako na jina lako nilihamasika sana kufungua huu uzi wako lakini nimesikitika sana baada ya kuona na kusoma ulichoandika kwa sababu kadha wa kadha.

Kwanza, Umeshindwa kuchunguza na kuelewa kuwa Gospel ambayo anaimba msanii wa Tanzania ni Bongo Fleva pia. Kwa lugha nyepesi umeandika bila kuelewa undani wa hicho unachokiandika. Pole sana.

Pili, Gospel sio lazima iimbwe juu ya biti za vinanda. Hio ni kwa sababu Gospel ni ujumbe na sio uzuri au ubaya wa biti. Swali ni kwamba ujumbe aliouonyesha Gozbert humo unahamasisha injili au unapinga injili??

Naomba unielewe kuwa sikatai kuwa unachokisema ni sahihi. Unaweza kuwa sahihi au usiwe sahihi. Ninachoshangaa ni kwamba umeshindwa kuthibitisha malalamiko yako. Ni kama watu wanaotaka bangi ihalalishwe - huwa wapo sahihi, ila hawajui kuitetea hoja yao.

Anyways, Ukijibu hayo maswali hapo juu naomba nikupe home work. Nenda uisikilize Album ya Kanye West, Jesus is King.
umejibu kama goodluck, au manager wake! Umeeleza Vyema
 
Habari wana JF,
Moja kwa moja kwenye mada, kama tujuavyo neno Gospel maana yake ni Habari njema kwa watu wote (kutokana na imani ya kikristo). Na kuna waimbaji wengi (hatuwaiti wasanii maana hamna usanii kwenye dini) wanaimba kama njia ya kumtumikia Mungu.Wapo wengi kama kina Bahati Bukuku, Rose Muhando,Christina Shusho n.k

Mwanzo nilikuwa nasita kupinga kuwa Goodluck gozbert sio muimbaji wa Injili ila ni mziki wake ni wa Bongo flavour tu. Hili linajidhirisha vyema kupitia nyimbo yake ya 'Nibadilishe' ambayo ndani yake mahadhi ya nyimbo na style za kucheza hazitofautiani na zile za kina Harmonise, Diamond, Burna Boy n.k. Hii inaniaminisha kuwa huyu si muimbaji wa gospel bali anafanya Bongo flavour kwa kivuli cha dini. Kama hujaona wimbo huo...Angalia kwenye link hapa chini....



Sent using Jamii Forums mobile app

Vigezo vya kujua huyu anaimba GOSPEL ni vip ?
 
Vigezo vya kujua huyu anaimba GOSPEL ni vip ?
Hili ni swali zuri sana, ila najua mleta uzi hawezi kulijibu kwa sababu hajafanya tafiti za kutosha juu ya malalamiko yake. Simlaumu, hata hivyo, kwa sababu ni haki ya kila mtu kuhoji ingawa maswali aliyonayo kayaweka kama mtazamo na hali halisi. Yaani hajataka kuuliza ila amekuja kutuambia Gozbert sio muimba Gospel na anataka tukubali. Kigezo alichokitumia sasa! Ni taabu tupu.

Pia hii ni mada ngumu na yenye mjadala mrefu sana, ila nitajitahidi kuifanya iwe fupi na inayoeleweka na nitapokea mapendekezo na nyongeza yeyote kutoka kwa mtu yeyote.

Kigezo cha kujua kwanini wimbo unaweza kuwa gospel na mwingine hauwezi kuwa gospel ni mashairi yanayoimbwa ndani ya wimbo husika na sio aina ya mdundo na vitendo vilivyoonekana kwenye video. Naamini kama mwenye wimbo amesambaza injili basi hiyo ni gospel music.

Uzuri wa Gospel ni kwamba imejigawa mara mbili, yaani kuna praise and worship, au kwa kiswahili, Kusifu na kuabudu au vyote kwa pamoja vikachanganywa kwenye wimbo mmoja. Kwa kutumia wimbo wa Gozbert huo wa nibadilishe ni ladha ya kuabudu. Kuwa mnyenyekevu na kuomba kwa Mungu. Mashairi yanajieleza vizuri... Nadhani mdundo ulitumika kwa maksudi kuweka hisia ya utambuzi kwa watu. Hakuna kilichotokea bahati mbaya. Na bahati nzuri hata biblia inatutaka tuseme ukweli na Gozbert alisema ukweli mule ndani. Shida ni kuwa tumekariri, hatutaki ku evolve. Hii ni 2020 watu bado wanataka tuishi kama 1950.. Inashangaza maana hata biblia zina matoleo mapya kila siku. Kwanini kwaya zisiwe na mfumo mpya?? 🤔
 
Back
Top Bottom